< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
Or Josaphat son fils régna en sa place, et se fortifia contre Israël.
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
Car il mit des troupes dans toutes les villes fortes de Juda, et des garnisons dans le pays de Juda, et dans les villes d'Ephraïm qu'Asa son père avait prises.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
Et l'Eternel fut avec Josaphat, parce qu'il suivit la première voie de David son père, et qu'il ne rechercha point les Bahalins.
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
Mais il rechercha le Dieu de son père, et marcha dans ses commandements, et non pas selon ce que faisait Israël.
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
L'Eternel donc affermit le Royaume entre ses mains; et tous ceux de Juda apportaient des présents à Josaphat, de sorte qu'il eut de grandes richesses et une grande gloire.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
Et appliquant de plus en plus son cœur aux voies de l'Eternel, il ôta encore de Juda les hauts lieux et les bocages.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
Et la troisième année de son règne, il envoya de ses principaux gouverneurs, [savoir], Benhajil, Hobadia, Zacharie, Nathanaël, et Micaia, pour instruire [le peuple] dans les villes de Juda;
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
Et avec eux des Lévites, [savoir] Sémahia, Néthania, Zébadia, Hazaël, Semiramoth, Jéhonatham, Adonija, Tobija, et Tob-adonija, Lévites; et avec eux Elisamah et Jéhoram, Sacrificateurs;
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
Qui enseignèrent en Juda, ayant avec eux le Livre de la Loi de l'Eternel; et ils firent le tour de toutes les villes de Juda, enseignant le peuple.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
Et la frayeur de l'Eternel fut sur tous les Royaumes des pays, qui étaient tout autour de Juda, de sorte qu'ils ne firent point la guerre à Josaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
On apportait aussi à Josaphat des présents de la part des Philistins, et de l'argent des impôts; et les Arabes lui amenaient des troupeaux, [savoir], sept mille sept cents moutons, et sept mille sept cents boucs.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
Ainsi Josaphat s'élevait jusques au plus haut degré de gloire; et il bâtit en Juda des châteaux, et des villes fortes.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
Il eut de grands biens dans les villes de Juda, et dans Jérusalem des gens de guerre forts et vaillants.
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
Et c'est ici leur dénombrement selon la maison de leurs pères. Les Chefs des milliers de Juda furent, Hadna capitaine, et avec lui trois cent mille hommes forts et vaillants;
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
Et après lui Johanan capitaine, et avec lui deux cent quatre-vingt mille;
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
Et après lui Hamasia fils de Zicri, qui s'était volontairement offert à l'Eternel, et avec lui deux cent mille hommes forts et vaillants;
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
Et de Benjamin, Eliadah, homme fort et vaillant, et avec lui deux cent mille hommes armés d'arcs et de boucliers;
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
Et après lui Jéhozabad, et avec lui cent quatre-vingt mille hommes équipés pour le combat.
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
Ce sont là ceux qui servaient le Roi, outre ceux que le Roi avait mis dans les villes fortes dans tout le pays de Juda.

< 2 Nyakati 17 >