< لوقا 19 >

پس وارد اریحا شده، از آنجا می گذشت. ۱ 1
Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
که ناگاه شخصی زکی نام که رئیس باجگیران و دولتمند بود، ۲ 2
Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
خواست عیسی را ببیند که کیست و از کثرت خلق نتوانست، زیرا کوتاه قد بود. ۳ 3
Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
پس پیش دویده بردرخت افراغی برآمد تا او را ببیند. چونکه اومی خواست از آن راه عبور کند. ۴ 4
Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
و چون عیسی به آن مکان رسید، بالا نگریسته او را دید و گفت: «ای زکی بشتاب و به زیر بیا زیرا که باید امروز درخانه تو بمانم.» ۵ 5
Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
پس به زودی پایین شده او را به خرمی پذیرفت. ۶ 6
Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
و همه چون این را دیدند، همهمه‌کنان می‌گفتند که در خانه شخصی گناهکار به میهمانی رفته است. ۷ 7
Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
اما زکی برپا شده به خداوند گفت: «الحال‌ای خداوند نصف مایملک خود را به فقرامی دهم و اگر چیزی ناحق از کسی گرفته باشم، چهار برابر بدو رد می‌کنم.» ۸ 8
Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
عیسی به وی گفت: «امروز نجات در این خانه پیدا شد. زیرا که این شخص هم پسر ابراهیم است. ۹ 9
Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
زیرا که پسرانسان آمده است تا گمشده را بجوید و نجات‌بخشد.» ۱۰ 10
Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
و چون ایشان این را شنیدند او مثلی زیادکرده آورد چونکه نزدیک به اورشلیم بود و ایشان گمان می‌بردند که ملکوت خدا می‌باید در همان زمان ظهور کند. ۱۱ 11
Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
پس گفت: «شخصی شریف به دیار بعید سفر کرد تا ملکی برای خود گرفته مراجعت کند. ۱۲ 12
Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
پس ده نفر از غلامان خود راطلبیده ده قنطار به ایشان سپرده فرمود، تجارت کنید تا بیایم. ۱۳ 13
Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
اما اهل ولایت او، چونکه او رادشمن می‌داشتند ایلچیان در عقب او فرستاده گفتند، نمی خواهیم این شخص بر ما سلطنت کند. ۱۴ 14
“Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
و چون ملک را گرفته مراجعت کرده بود، فرمود تا آن غلامانی را که به ایشان نقد سپرده بودحاضر کنند تا بفهمد هر یک چه سود نموده است. ۱۵ 15
“Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
پس اولی آمده گفت، ای آقا قنطار تو ده قنطار دیگر نفع آورده است. ۱۶ 16
“Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
بدو گفت آفرین‌ای غلام نیکو. چونکه بر چیز کم امین بودی بر ده شهر حاکم شو. ۱۷ 17
“Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
و دیگری آمده گفت، ای آقاقنطار تو پنج قنطار سود کرده است. ۱۸ 18
“Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
او را نیزفرمود بر پنج شهر حکمرانی کن. ۱۹ 19
“Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
و سومی آمده گفت، ای آقا اینک قنطار تو موجود است، آن را در پارچه‌ای نگاه داشته‌ام. ۲۰ 20
“Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
زیرا که از توترسیدم چونکه مرد تندخویی هستی. آنچه نگذارده‌ای، برمی داری و از آنچه نکاشته‌ای درومی کنی. ۲۱ 21
Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
به وی گفت، از زبان خودت بر توفتوی می‌دهم، ای غلام شریر. دانسته‌ای که من مرد تندخویی هستم که برمیدارم آنچه رانگذاشته‌ام و درو می‌کنم آنچه را نپاشیده‌ام. ۲۲ 22
“Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
پس برای چه نقد مرا نزد صرافان نگذاردی تاچون آیم آن را با سود دریافت کنم؟ ۲۳ 23
kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
پس به حاضرین فرمود قنطار را از این شخص بگیرید وبه صاحب ده قنطار بدهید. ۲۴ 24
“Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
به او گفتند‌ای خداوند، وی ده قنطار دارد. ۲۵ 25
“Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
زیرا به شمامی گویم به هر‌که دارد داده شود و هر‌که نداردآنچه دارد نیز از او گرفته خواهد شد. ۲۶ 26
“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
اما آن دشمنان من که نخواستند من بر ایشان حکمرانی نمایم، در اینجا حاضر ساخته پیش من به قتل رسانید.» ۲۷ 27
Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
و چون این را گفت، پیش رفته متوجه اورشلیم گردید. ۲۸ 28
Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
و چون نزدیک بیت‌فاجی وبیت عنیا بر کوه مسمی به زیتون رسید، دو نفر ازشاگردان خود را فرستاده، ۲۹ 29
Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
گفت: «به آن قریه‌ای که پیش روی شما است بروید و چون داخل آن شدید، کره الاغی بسته خواهید یافت که هیچ‌کس بر آن هرگز سوار نشده. آن را باز کرده بیاورید. ۳۰ 30
“Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
و اگر کسی به شما گوید، چرا این راباز می‌کنید، به وی گویید خداوند او را لازم دارد.» ۳۱ 31
Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
پس فرستادگان رفته آن چنانکه بدیشان گفته بود یافتند. ۳۲ 32
Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
و چون کره را باز می‌کردند، مالکانش به ایشان گفتند چرا کره را باز می‌کنید؟ ۳۳ 33
Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
گفتند خداوند او را لازم دارد. ۳۴ 34
Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
پس او را به نزد عیسی آوردند و رخت خود را بر کره افکنده، عیسی را سوار کردند. ۳۵ 35
Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
و هنگامی که او می‌رفت جامه های خود را در راه می‌گستردند. ۳۶ 36
Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
و چون نزدیک به‌سرازیری کوه زیتون رسید، تمامی شاگردانش شادی کرده، به آوازبلند خدا را حمد گفتن شروع کردند، به‌سبب همه قواتی که از او دیده بودند. ۳۷ 37
Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
و می‌گفتند مبارک باد آن پادشاهی که می‌آید، به نام خداوند سلامتی در آسمان و جلال در اعلی علیین باد. ۳۸ 38
“Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
آنگاه بعضی از فریسیان از آن میان بدو گفتند: «ای استاد شاگردان خود را نهیب نما.» ۳۹ 39
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
او درجواب ایشان گفت: «به شما می‌گویم اگراینها ساکت شوند، هرآینه سنگها به صداآیند.» ۴۰ 40
Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
و چون نزدیک شده، شهر را نظاره کرد برآن گریان گشته، ۴۱ 41
Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
گفت: «اگر تو نیز می‌دانستی هم در این زمان خود آنچه باعث سلامتی تومیشد، لاکن الحال از چشمان تو پنهان گشته است. ۴۲ 42
akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
زیرا ایامی بر تو می‌آید که دشمنانت گرد تو سنگرها سازند و تو را احاطه کرده از هرجانب محاصره خواهند نمود. ۴۳ 43
Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
و تو را وفرزندانت را در اندرون تو بر خاک خواهند افکندو در تو سنگی بر سنگی نخواهند گذاشت زیرا که ایام تفقد خود را ندانستی.» ۴۴ 44
Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
و چون داخل هیکل شد، کسانی را که درآنجا خرید و فروش می‌کردند، به بیرون نمودن آغاز کرد. ۴۵ 45
Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
و به ایشان گفت: «مکتوب است که خانه من خانه عبادت است لیکن شما آن را مغاره دزدان ساخته‌اید.» ۴۶ 46
Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
و هر روز در هیکل تعلیم می‌داد، اما روسای کهنه و کاتبان و اکابر قوم قصدهلاک نمودن او می‌کردند. ۴۷ 47
Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
و نیافتند چه کنندزیرا که تمامی مردم بر او آویخته بودند که از اوبشنوند. ۴۸ 48
Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.

< لوقا 19 >