< مرقس 1 >

ابتدا انجیل عیسی مسیح پسر خدا. ۱ 1
Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
چنانکه در اشعیا نبی مکتوب است، «اینک رسول خود را پیش روی تو می‌فرستم تاراه تو را پیش تو مهیا سازد. ۲ 2
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
صدای ندا کننده‌ای در بیابان که راه خداوند را مهیا سازید و طرق او راراست نمایید.» ۳ 3
“sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
یحیی تعمید‌دهنده در بیابان ظاهر شد وبجهت آمرزش گناهان به تعمید توبه موعظه می‌نمود. ۴ 4
Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
و تمامی مرز و بوم یهودیه و جمیع سکنه اورشلیم نزد وی بیرون شدند و به گناهان خود معترف گردیده، در رود اردون از او تعمیدمی یافتند. ۵ 5
Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
و یحیی را لباس از پشم شتر وکمربند چرمی بر کمر می‌بود و خوراک وی ازملخ و عسل بری. ۶ 6
Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
و موعظه می‌کرد و می‌گفت که «بعد از من کسی تواناتر از من می‌آید که لایق آن نیستم که خم شده، دوال نعلین او را باز کنم. ۷ 7
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
من شما را به آب تعمید دادم. لیکن او شما را به روح‌القدس تعمید خواهد داد.» ۸ 8
Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
و واقع شد در آن ایام که عیسی از ناصره جلیل آمده در اردن از یحیی تعمید یافت. ۹ 9
Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
وچون از آب برآمد، در ساعت آسمان را شکافته دید و روح را که مانند کبوتری بروی نازل می‌شود. ۱۰ 10
Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
و آوازی از آسمان در‌رسید که «توپسر حبیب من هستی که از تو خشنودم.» ۱۱ 11
Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
پس بی‌درنگ روح وی را به بیابان می‌برد. ۱۲ 12
Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
و مدت چهل روز در صحرا بود و شیطان او راتجربه می‌کرد و با وحوش بسر می‌برد و فرشتگان او را پرستاری می‌نمودند. ۱۳ 13
naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
و بعد از گرفتاری یحیی، عیسی به جلیل آمده، به بشارت ملکوت خدا موعظه کرده، ۱۴ 14
Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
می گفت: «وقت تمام شد و ملکوت خدانزدیک است. پس توبه کنید و به انجیل ایمان بیاورید.» ۱۵ 15
akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
و چون به کناره دریای جلیل می‌گشت، شمعون و برادرش اندریاس را دید که دامی دردریا می‌اندازند زیرا که صیاد بودند. ۱۶ 16
Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
عیسی ایشان را گفت: «از عقب من آیید که شما را صیادمردم گردانم.» ۱۷ 17
Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
بی‌تامل دامهای خود را گذارده، از پی او روانه شدند. ۱۸ 18
Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
و از آنجا قدری پیشتررفته، یعقوب بن زبدی و برادرش یوحنا را دید که در کشتی دامهای خود را اصلاح می‌کنند. ۱۹ 19
Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
درحال ایشان را دعوت نمود. پس پدر خود زبدی را با مزدوران در کشتی گذارده، از عقب وی روانه شدند. ۲۰ 20
Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
و چون وارد کفرناحوم شدند، بی‌تامل درروز سبت به کنیسه درآمده، به تعلیم دادن شروع کرد، ۲۱ 21
Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
به قسمی که از تعلیم وی حیران شدند، زیرا که ایشان را مقتدرانه تعلیم می‌داد نه مانندکاتبان. ۲۲ 22
Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
و در کنیسه ایشان شخصی بود که روح پلیدداشت. ناگاه صیحه زده، ۲۳ 23
Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
گفت: «ای عیسی ناصری ما را با تو چه‌کار است؟ آیا برای هلاک کردن ما آمدی؟ تو را می‌شناسم کیستی، ای قدوس خدا!» ۲۴ 24
naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
عیسی به وی نهیب داده، گفت: «خاموش شو و از او درآی!» ۲۵ 25
Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
در ساعت آن روح خبیث او را مصروع نمود و به آواز بلند صدازده، از او بیرون آمد. ۲۶ 26
Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
و همه متعجب شدند، بحدی که از همدیگر سوال کرده، گفتند: «این چیست و این چه تعلیم تازه است که ارواح پلید رانیز با قدرت امر می‌کند و اطاعتش می‌نمایند؟» ۲۷ 27
Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
و اسم او فور در تمامی مرز و بوم جلیل شهرت یافت. ۲۸ 28
Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
و از کنیسه بیرون آمده، فور با یعقوب ویوحنا به خانه شمعون و اندریاس درآمدند. ۲۹ 29
Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
ومادر‌زن شمعون تب کرده، خوابیده بود. درساعت وی را از حالت او خبر دادند. ۳۰ 30
Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
پس نزدیک شده، دست او را گرفته، برخیزانیدش که همان وقت تب از او زایل شد و به خدمت گذاری ایشان مشغول گشت. ۳۱ 31
Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
شامگاه چون آفتاب به مغرب شد، جمیع مریضان و مجانین را پیش او آوردند. ۳۲ 32
Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
و تمام شهر بر در خانه ازدحام نمودند. ۳۳ 33
Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
و بسا کسانی را که به انواع امراض مبتلا بودند، شفا داد ودیوهای بسیاری بیرون کرده، نگذارد که دیوهاحرف زنند زیرا که او را شناختند. ۳۴ 34
Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
بامدادان قبل از صبح برخاسته، بیرون رفت و به ویرانه‌ای رسیده، در آنجا به دعا مشغول شد. ۳۵ 35
Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
و شمعون و رفقایش در‌پی او شتافتند. ۳۶ 36
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
چون او را دریافتند، گفتند: «همه تو رامی طلبند.» ۳۷ 37
nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
بدیشان گفت: «به دهات مجاورهم برویم تا در آنها نیز موعظه کنم، زیرا که بجهت این کار بیرون آمدم.» ۳۸ 38
Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
پس در تمام جلیل درکنایس ایشان وعظ می‌نمود و دیوها را اخراج می‌کرد. ۳۹ 39
Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
و ابرصی پیش وی آمده، استدعا کرد وزانو زده، بدو گفت: «اگر بخواهی، می‌توانی مراطاهر سازی!» ۴۰ 40
Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
عیسی ترحم نموده، دست خودرا دراز کرد و او را لمس نموده، گفت: «می‌خواهم. طاهر شو!» ۴۱ 41
Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
و چون سخن گفت، فی الفور برص از او زایل شده، پاک گشت. ۴۲ 42
Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
و اورا قدغن کرد و فور مرخص فرموده، ۴۳ 43
Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
گفت: «زنهار کسی را خبر مده، بلکه رفته خود را به کاهن بنما و آنچه موسی فرموده، بجهت تطهیر خودبگذران تا برای ایشان شهادتی بشود.» ۴۴ 44
akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
لیکن اوبیرون رفته، به موعظه نمودن و شهرت دادن این امر شروع کرد، بقسمی که بعد از آن او نتوانست آشکارا به شهر درآید بلکه در ویرانه های بیرون بسر می‌برد و مردم از همه اطراف نزد وی می‌آمدند. ۴۵ 45
Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.

< مرقس 1 >