< Ephesians 3 >

1 For this reason I Paul, the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles,
Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2 since indeed ye heard of the administration of the grace of God, which was given to me for you,
Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3 that according to revelation he made known to me the mystery, as I wrote before in brief.
Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4 With which reading ye can recognize my understanding in the mystery of the Christ,
nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5 which in other generations was not made known to the sons of men, as it has now been revealed by Spirit to his holy apostles and prophets.
Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6 For Gentiles to be fellow-heirs, and of the same body, and fellow partakers of his promise in the Christ through the good news.
Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7 Of which I became a helper according to the gift of that grace of God, which was given to me according to the working of his power.
Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8 To me, a man less than the least of all the sanctified, this grace was given to preach good news among the Gentiles, the unsearchable wealth of Christ,
Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9 and to make all men see what is the administration of the mystery hidden from the ages in God who created all things through Jesus Christ. (aiōn g165)
tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
10 So that now the manifold wisdom of God might be made known to the principal offices and the positions of authority in the heavenly things, through the church,
kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11 according to the purpose of the ages, which he made in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
12 in whom we have boldness and access in confidence through his faith.
Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13 Therefore I ask that ye not become discouraged at my tribulations on your behalf, which is your glory.
Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14 For this reason I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15 from whom every patriarchy in heavens and on earth is named.
aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16 So that he would grant you, according to the wealth of his glory, to be strengthened with power through his Spirit for the inner man,
Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17 for the Christ to dwell in your hearts through faith,
naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18 having been rooted and grounded in love, so that ye may be able to grasp with all the sanctified what is the breadth and length and depth and height,
kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19 and to become aware of the love of the Christ, which transcends knowledge, so that ye may be filled in all the fullness of God.
Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20 Now to him who is able to do above extraordinary-above all things that we ask or think-according to the power that works in us,
Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21 to him is the glory in the church in Christ Jesus for all generations of the age of the ages. Truly. (aiōn g165)
kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)

< Ephesians 3 >