< Ephesians 2 >

1 Even you, who were dead in trespasses and sins
Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.
2 in which ye once walked according to the era of this world, according to the ruler of the power of the air, the spirit that now works in the sons of disobedience. (aiōn g165)
Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu. (aiōn g165)
3 Among whom we also all once behaved in the lusts of our flesh, doing the intentions of the flesh and of the thoughts, and were by nature children of wrath as also the others.
Na hata sisi sote tulikuwa kama wao; tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya tu mambo yale yaliyoipendeza miili na akili zetu. Kidunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.
4 But God, being rich in mercy, through his great love that he loved us,
Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa mapendo yasiyopimika,
5 even us being dead in the transgressions, he made alive together with the Christ (ye are saved by grace),
hata, ingawa tulikuwa tumekufa kwa sababu ya dhambi, alitufanya hai pamoja na Kristo. Kwa neema ya Mungu ninyi mmeokolewa.
6 and raised us up together, and seated us together in the heavenly things in Christ Jesus.
Kwa kuungana na Kristo Yesu, Mungu alitufufua pamoja naye, tukatawale pamoja naye mbinguni.
7 So that in the coming ages he might show the transcending wealth of his grace in kindness toward us in Christ Jesus. (aiōn g165)
Ndivyo alivyopenda kuonyesha kwa watu wa nyakati za baadaye, ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu. (aiōn g165)
8 For ye are saved by grace through faith, and this a gift of God, not from you,
Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu.
9 not from works, so that not any man may boast.
Wala halitokani na matendo yenu wenyewe, asije mtu akajivunia kitu.
10 For we are his workmanship, created in Christ Jesus for good works, which God preordained that we should walk in them.
Sisi ni viumbe vyake Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
11 Remember therefore that once ye, the Gentiles in flesh, who are called uncircumcision by that which is called circumcision (in flesh, made by hands),
Ninyi mlio kwa asili watu wa mataifa mengine—mnaoitwa, “wasiotahiriwa” na Wayahudi ambao hujiita, “Waliotahiriwa,” (kwa sababu ya kile wanachoifanyia miili yao) —kumbukeni mlivyokuwa zamani.
12 that ye were at that time independent of Christ, alienated from the citizenship of Israel, and alien of the covenants of the promise, having no hope and godless in the world.
Wakati ule ninyi mlikuwa bila Kristo; mlikuwa nje ya jamii ya Israeli; mlikuwa wageni na hamkuwa na sehemu yoyote katika lile agano la zile ahadi. Mlikuwa bila matumaini Mungu hapa duniani.
13 But now in Christ Jesus ye, being formerly far off, became near in the blood of the Christ.
Lakini sasa, kwa kuungana na Kristo Yesu, ninyi ambao hapo awali mlikuwa mbali, mmekaribishwa kwa njia ya damu yake Kristo.
14 For he is our peace, who made both one, and broke down the dividing wall of partition,
Maana Kristo mwenyewe ametuletea amani kwa kuwafanya Wayahudi na watu wa mataifa mengine kuwa jamii moja. Kwa mwili wake yeye mwenyewe aliubomoa ule ukuta uliowatenganisha na kuwafanya maadui.
15 having abolished in his flesh the enmity-the law of the commandments in ordinances-so that he might create in himself the two into one new man, making peace,
Aliiondoa ile Sheria ya Wayahudi pamoja na amri zake na kanuni zake, ili kutokana na jamii hizo mbili aumbe jamii moja mpya katika umoja naye na hivyo kuleta amani.
16 and might reconcile them both in one body to God through the cross, having slain the enmity by it.
Kwa mwili wake, Kristo aliuangamiza uadui wao; kwa msalaba wake aliziunganisha jamii hizo kuwa moja na kuzipatanisha na Mungu.
17 And after coming he preached good news, peace to you, to those far off and to those near,
Basi, Kristo alikuja akahubiri Habari Njema ya amani kwenu ninyi watu wa mataifa mengine mliokuwa mbali na Mungu, na pia kwa Wayahudi ambao walikuwa karibu na Mungu.
18 because through him we both have the access in one Spirit to the Father.
Hivyo, kwa njia yake, sisi sote, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, tunaweza kumwendea Baba katika Roho mmoja.
19 So then ye are no more alien and foreign, but fellow citizens of the sanctified, and belonging to the household of God.
Basi, ninyi si wageni tena, wala si watu wa nje; ninyi ni raia pamoja na watu wa Mungu, na ni watu wa jamaa ya Mungu.
20 Which was built upon the foundation of the apostles and prophets, Christ Jesus himself being the chief corner,
Mmejengwa juu ya msingi uliowekwa na mitume na manabii, naye Kristo mwenyewe ndiye jiwe kuu la msingi.
21 in whom the whole building joined together grows into a holy temple in the Lord,
Yeye ndiye mwenye kulitengeneza jengo lote na kulikuza hata liwe hekalu takatifu kwa ajili ya B wana.
22 in whom ye also are built together in Spirit into a habitation of God.
Katika kuungana naye, ninyi pia mnajengwa pamoja na wote wengine, muwe makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.

< Ephesians 2 >