< Uruyan Yuhana 17 >

1 Warum nanya nono kadura Kutelle ule na a wadi nin kukurum kun zur ada adworiyi, “Da, ima dursufe ucan mmolu nkaruwa udiya ule na a sosin kitene myein gbardan,
Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na bakuli akaja, akaniambia, “Njoo, mimi nitakuonyesha adhabu aliyopewa yule mzinzi mkuu, mji ule uliojengwa juu ya maji mengi.
2 Ame ule na Ago nyii na su uzina nan ghe, kitane ntoro in zina mye anang lisosin nanyan nyie na so bolm.”
Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye; na wakazi wa dunia wamelewa divai ya uzinzi wake.”
3 Gono kadura Kutelle yerai nanyan Ruhu udu kusho, inin yene uwani sosin kitene nfon funanan tene a wa kulung nin tizogo tisa. Finawe wadi ni nati kuzur nin na wulu.
Kisha, Roho akanikumba, akaniongoza mpaka jangwani. Huko nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama mwekundu. Mnyama huyo alikuwa ameandikwa kila mahali majina ya makufuru; alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
4 Uwane wa shon imoon nmyein nafa, nin myein mi shine nwoltu anin su kuyok nin nizinariya, atala a ciine, nin natan luu luu. A wa myein ncara mye ka kuk nizinariya ka kuluno nin nimoon izenzen, nin dinong nzwa mye.
Mwanamke huyo alikuwa amevaa vazi la rangi ya zambarau na nyekundu; alikuwa amejipamba kwa dhahabu, mawe ya thamani na lulu. Mkononi mwake alishika kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa machukizo na mambo machafu yanayoonyesha uzinzi wake.
5 Kitenemye i wa yertin imemong na iwa nyeshin: “UBABILA UDIYA, UNAH NA KARUWA NIN NIMON IZEMZEM NYII ULELE.”
Alikuwa ameandikwa juu ya paji la uso wake jina la fumbo “Babuloni mkuu, mama wa wazinzi na wa mambo yote ya kuchukiza sana duniani.”
6 Nwa yene uwanii une nta bomn nin myii nanit alau nin myii nanan nizi iban Yesu. Kubi ko nanyene ghe nwa su umamaki kan.
Nikamwona huyo mwanamke amelewa damu ya watu wa Mungu, na damu ya watu waliouawa kwa sababu ya kumtangaza Yesu. Nilipomwona nilishangaa mno.
7 Unan kadura Kutelle woroi, “Bara iyanghai usu umamaki? Mma belen fi umaana inwane nin funawan tine nan ayonghe (finawan tene fo na fidi nin nati kuzur nin nawulu kuzur).
Lakini malaika akaniambia, “Kwa nini unashangaa? Mimi nitakuambia maana iliyofichika ya mwanamke huyu na mnyama huyo amchukuaye ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.
8 Fina nawan tene na uyene fiwan duku, fiduku nene ba, bara nani fidin cinu unuzu nanyan kuwu ku cancam sa ligang. Ama li ubun mmolsu. Alenge na isosin nyei, alenge na ina yertin tisamene nanya kubaga nlai ba uwaaru ukyen nye-iwa yene finawa fone bara na awa diku na aduku nene ba adin cinu. (Abyssos g12)
Huyo mnyama uliyemwona alikuwa hai hapo awali, lakini sasa amekufa. Hata hivyo, karibu sana atapanda kutoka shimoni kuzimu, lakini ataangamizwa. Wanaoishi duniani watashangaa; naam, watu wote ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangu mwanzo wa ulimwengu, watashangaa kumwona huyo mnyama ambaye hapo awali, aliishi, kisha akafa na sasa anatokea tena! (Abyssos g12)
9 Nene kitin nan kpilizu ujinjin. Kuzure titudu kuzurari alenge na uwane sosin ku.
“Hapa panahitaji akili na hekima! Hivyo vichwa saba ni vilima saba, na huyo mwanamke anaketi juu yake. Vichwa hivyo pia ni wafalme saba.
10 Inan ago kuzurari tutung. Ago afaun namalu diyu, warun duku, na umong nsa da ba; a wadak, ama yiti na nin damdaunu ba.
Kati ya hao wafalme saba, watano wamekwisha angamia, mmoja anatawala bado, na yule mwingine bado hajafika; na atakapofika atabaki kwa muda mfupi.
11 Finawan tene fo na fiduku, na fiduku nene ba, amere litime ugo unlir; bara nani adi nanya nago kuzure, amanin du nmulsu nanit.
Huyo mnyama ambaye alikuwa anaishi hapo awali lakini sasa haishi tena ni mfalme wa nane, naye pia ni miongoni mwa hao saba, na anakwenda zake kuharibiwa.
12 Awulu likure na uwa yene ago likure na uwa yene ago likurari alenge na isa sere kipin tigo mene ba, bara na ima seru likara nafo ago nanya kube kurun ligowe nin finawantene.
“Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme ambao bado hawajaanza kutawala. Lakini watapewa mamlaka ya kutawala kwa muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.
13 Alele dinin kibinai kirum inin naa likara tigo mene kiti finawan tene.
Shabaha ya hawa kumi ni moja, na watampa yule mnyama nguvu na mamlaka yao yote.
14 Ima su likum nin kukame. Bara nani ku kame ma li nani nin likum bara na ame Cikilari nilariari nin go nago-ligowe ninghe alenge na ina fere nani, anang yenu sa uyenu.”
Watapigana na Mwanakondoo, lakini Mwanakondoo pamoja na wale aliowaita na kuwachagua, ambao ni waaminifu, atawashinda kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme.”
15 Unan kadura Kutelle wa woroi, “Nmyene na uyene, kikaa na ukaruwe sosinku, anitari, ligozin nanit, nipinpin, nin tilem tilem.
Malaika akaniambia pia, “Yale maji uliyoyaona pale alipokaa yule mzinzi, ni mataifa, watu wa kila rangi na lugha.
16 Awulu likure na uyene-unung nan finawan tene ma nari ukaruwe, utighe aso usane nin fisere, ima li inawamye ima jujughe nin nla.
Pembe zile kumi ulizoziona na yule mnyama watamchukia huyo mzinzi. Watachukua kila kitu alicho nacho na kumwacha uchi; watakula nyama yake na kumteketeza kwa moto.
17 Kutelle nati nanya nayii mene iyeru unufe mye nyenu ine likara udu funawan tene asu tigo udu kubi ko na uliru Kutelle nkulu.
Maana Mungu ametia mioyoni mwao nia ya kutekeleza shabaha yake, yaani kwa kukubaliana wao kwa wao na kumpa huyo mnyama mamlaka yao ya kutawala, mpaka hapo neno la Mungu litakapotimia.
18 Uwane na uyene, kipin kidyawari na kidi tigo kitene nago nyii vat.”
“Na yule mwanamke uliyemwona ndio ule mji mkuu unaowatawala wafalme wa dunia.”

< Uruyan Yuhana 17 >