< Uruyan Yuhana 16 >

1 Nwa lanza liwue li diya in yicila nnuzu nan nya kiti kilau we anin bele nono katwa Kutelle inun kuzere, “Can nan nyan ye idi gutun imon inanzan ti nana nayi Ketelle kuzure.”
Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni mkamwage mabakuli hayo saba ya ghadhabu ya Mungu duniani.”
2 Unan katwa Kutelle unan burne talo uyi a gutuna innye ku; ukonu unanzan nin nanut daa kitene na nit a le na ina seru kulap finawan tene, nin na le na idin tumuzunu ku yeli mye.
Basi, malaika wa kwanza akaenda akamwaga bakuli lake juu ya nchi. Mara madonda mabaya na ya kuumiza sana yakawapata wote waliokuwa na alama ya yule mnyama, na wale walioiabudu sanamu yake.
3 Unan mba gutuna kun mye nan nya kurawa kudiya; ku so nafo nmii na le na ikuzu, vat nimon in lai nan nya kurawa kudiwe kuu.
Kisha malaika wa pili akamwaga bakuli lake baharini. Nayo bahari ikawa damu tupu kama damu ya mtu aliyekufa, na viumbe vyote hai baharini vikafa.
4 Unan talle gutuna kun mye nan nya nali nin nigun gaawa a figunan myeen; i lawa myeen.
Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, navyo vikageuka damu.
5 Nu lanza anan kadura nan nya myeene benle, “Fe di dert - ule na u de umi de ulau - bara na udaa nin wucu.
Nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema, “Ewe mtakatifu, Uliyeko na uliyekuwako! Wewe ni mwenye haki katika hukumu hii uliyotoa.
6 Bara na ina gutun myii na nit a lau u mine nnaa nani nmyii i sono; imon ile nan i caun nani ri.”
Maana waliimwaga damu ya watu wako na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; wamestahili hivyo!”
7 Nlanza kitin ki zalan mgutuzunu myii kawaa, “Nanere, Kutelle cikilari ulege na adin su tigo vat, mawucuwucu kedegenarrai nin cene.”
Kisha nikasikia sauti madhabahuni ikisema, “Naam, Bwana Mungu Mwenye Uwezo! Hukumu zako ni za kweli na haki!”
8 Unan nas se gutuna kun me ku kur ne ketene wui iyeninghe mun likara ajuju anit nin nlaa.
Kisha malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua. Jua likapewa nguvu ya kuwachoma watu kwa moto wake.
9 I wa juju nani nin piyu kang, inin zeigo lisa kutelle, ule na adin nin likara ketene ni mon inanz. Na iwa sun alapi mene ba sa ineghe ngongon.
Basi, watu wakaunguzwa vibaya sana; wakamtukana Mungu aliye na uwezo juu ya mabaa hayo makubwa. Lakini hawakuziacha dhambi zao na kumtukuza Mungu.
10 Unan kadura Kutelle unan taun gutun kum mye ku kurune kiti lisosin finawan tene, nsiti tursu kipin tigo mye. Iwa kifzin ayine mene nan nyan niyu udiya.
Kisha malaika wa tano akamwaga bakuli lake juu ya makao makuu ya yule mnyama. Giza likauvamia utawala wake, watu wakauma ndimi zao kwa sababu za maumivu,
11 Izoguzo Kutelle kitine kani bara uniyu udia nin na nut mene, unari usunu kulapi mene na ina su.
wakamtukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na madonda yao. Lakini hawakuyaacha matendo yao mabaya.
12 Unan kadura Kutelle unan tucine sutu kun mye kucurine nan nya kurawa affaratis, nmein ne kutu bara unan kele libau na go na iwa nuzun kusarimnu cun nwui.
Kisha malaika wa sita akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa uitwao Eufrate. Maji yake yakakauka, na hivyo njia ilitengenezwa kwa ajili ya wafalme wa mashariki.
13 Iyene uruhu uzenzen utart na iyi adi nafo a kponkpi din nucu nan nya tinuu ndragon, finawan tene, nin nanan liru nin nuu kutenlelle kinu.
Kisha nikaona pepo wabaya watatu walio kama vyura, wakitoka kinywani mwa yule joka, kinywani mwa yule mnyama, na kinywani mwa yule nabii wa uongo.
14 Uruhu na gbergenu nsu nman izikiki nin nalop. I wa nucu udu kitin nago nyii va anan pitirno nani vat udu kiti likum liri lidiya Kutelle, na adi tigo vat.
Hawa ndio roho za pepo wafanyao miujiza. Ndio wanaokwenda kwa wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita kuu Siku ile ya Mungu Mwenye Uwezo.
15 (“Yenjen! Indin cinu nafo ukiri! Unan mariari ule na adin caa, ule na ddin cinu dert bara a wa so fisere ininyene unan cin mye na aduku.”)
“Sikiliza! Mimi naja kama mwizi! Heri mtu akeshaye na kuvaa nguo zake ili asije akaenda uchi huko na huko mbele ya watu.”
16 I daa nin shenu ki kah na idin yicu nin lilem ibrinanci Harmagedon. (Kuparan nam)
Basi, roho hao wakawakusanya hao wafalme mahali paitwapo kwa Kiebrania Harmagedoni.
17 Unan zuru kala kumeh nan nyan nfunu. Liwui udiya nuzu nan nya kiti kilauwe nin nuzu kutete, a woro, “Umala!”
Kisha malaika wa saba akamwaga bakuli lake hewani. Sauti kubwa ikasikika kutoka kwenye kiti cha enzi, Hekaluni, ikisema, “Mwisho umefika!”
18 Umarzinun nkanan wadi di nin ti wui nin tutuzu, nin zunu kutiyen udiya - nin zunu KKutelle udia ule na isa su ba uwuroo ukey nit nyii, uzunu kutiyen kone wadi udiya.
Kukatokea umeme, kelele, ngurumo na tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijapata kutokea tangu Mungu alipomuumba mtu.
19 Ka gbiri ka diya wa kusu kidowo titat, inmyena, nipinpin diso. Kutelle lizino nin Babila udiya mbun Kutelle anaa kipine kakuk ntoro mi gbagbai tinana nayi mye.
Mji ule mkuu ukapasuliwa sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikateketea. Babuloni, mji mkuu, haukusahauliwa na Mungu. Aliunywesha kikombe cha divai ya ghadhabu yake kuu.
20 Nitin nsalin myeing nan nya kuli kudya cu na iwa kuru iyene nani ba.
Visiwa vyote vikatoweka, nayo milima haikuonekena tena.
21 A tantani a didiya, ngetek mene nafo utanlent urmu, nuzu kitene kani ada diso kitene na nite, i zugo Kutelle bara imon inanzan na tam ta ni, bara na imon inanzanghe wa nani kang.
Mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa kama kilo hamsini kila moja, ikawanyeshea watu. Nao wakamtukana Mungu kwa sababu ya mapigo ya mvua hiyo ya mawe. Naam, pigo la mvua hiyo ya mawe lilikuwa kubwa mno.

< Uruyan Yuhana 16 >