< Luuka 5 >

1 pe jilyahumile unsiki ghuno avaanhu vakan'kong'anikila na kun'syuta na kupulikisia ilisio lya Nguluve, pano alyale imile ulubale lwa kikogha kya Genesaleti.
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 akavona ifyombo fivili fifikile mulubale na malenga. vano visuvula vala valyahumile valyale visuka indovele save.
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 uYesu akingila mu kyobo kimonga kino kilyale kya Simoni akansuuma atwale mu malenga kutali padebe ni iisi indaghafu. pe ikala na kum'bulanisia kuhumila mu kyombo kila.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 kujova akam'bula uSimoni akati, twala ikyombo kyako kuhanga mukilindi kya malenga na kukwisia indovelo sako neke kusuvua iswi”
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 uSimoni akamwamula akati,” Mutwa tuvombile imbombo ikilo jooni, natukolile kyokyoni, neke kulisio lyako, nikisisia indovelo.
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 vati vavombile nahele vakakong'anisie iswi nyinga na sindovelo save sikatengula kudemuka.
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 pe vakavakemhela avajanave neke viise kukuvatanga. vakisa vakamemia ifyombo fyave fyoni fyope fikatengula kusovelela.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 neke uSimoni Peteli ati avwene ndikio, akaghua pamafundo gha Yesu akati, “Mutwa vuuka palyune, ulwakuva une nilinisambi”
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 ulwakuva alyadeghisivue na voni vanovalyale palikimo nu mwene kuvusuvi vwa swi vuno vakavuvombile.
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 ili likavakong'anisie uYakovo nu Yohani avaanha va Sebedayo, vano valyale vakong'aniki va Simoni. uYesu akam'bula u Simoni akati, “nungoghopaghe, ulwakuva kutengulila lino nakughendelela ghutengula kusuvula avaanhu”
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 vati vahumisie ifyombo fyave ku iisi indaghafu vakafileka na kumbingilila umwene.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 jilyahumile kuuti ye alyafikile mu mpulo ghumonga, umuunhu juno alyale amemile uvukoma alyale ukuo. ati amwaghile uYesu, akasula misia umutu ghake paasi na kukufunya akati,” Mutwa nave ghunoghua, ghuwesia kunivalasia”.
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 pe pano uYesu akagholosia uluvoko lwake na kun'kola, akati,” nilonda kuvalasivua” nu n'siki ghula ghula uvukoma vukamuleka.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 akamulaghisia nangam'bulaghe umuunhu ghweni, neke akam'bula kuuti, “lutagha juve ghwe mwene ukajivonesie kuvatekesi na kuhumia ilitekelo lwa kuvalasuvua, palikimo na kila kino uMoose akuvuli ku vujovi vwako.
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 neke imhola inofu sikaghenda kutali kyongo, ni lipugha likome ilya vaanhu likisa palikimo kumpulikisia ye ivulanisia na kusosia inhamu savo.
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 neke ke kinga ikukala kuvusyefu kukufunya.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 kikahumile ikighono kimonga mu fighono fino alyale ivulanisia, pwevalyale avaFalisayi na vavulanisi vwa ndaghilo vano vakikalile apuo vano vakisile kuhumila mu fikaaja ifingi mu vughavo vwa Galilaya na ku Yudea kange kuhumila mu mpulo ghwa Yelusalemu. ingufu sa Nguluve silyale palikimo nave kunsosia.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 avaanhu vamonga vakisile vampindile mu kitefu umuunhu juno v, pe vakalonda isila ja kumwingisia mun'kate neke kumughonia pavulogolo pa Yesu.
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 navaka jaghile isila ja kumwingisia mun'kate ulwakuva ilipugha lya vaanhu lilyale likome. pe vakatogha pakyanya pa lipaala lya nyumba na kumwisia umuunhu jula paasi kukilia mu figai pe vakavika pakate pa vaanhu pavulongolo pa Yesu.
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 lolagha ulwitiko lwako, uYesu akati, “nyalukolo usaghilue isambi sako”
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 avavulanisi na vaFarisayi vakatengula kuposia ilio. akaati uju ghwe veni juno ijova imbivi? ghwe veni juno isaghila isambi neke ghwe Nguluve mwene?
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 neke uYesu, akakagwile kiki vakale visagha, akavamula na kukuvavula,”
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 kiki mukuposesania mu mooja ghinu? kiliku kye kihugu kujova, 'isambi sako sisaghilue' au kuuti 'ghenda ulute?'
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 neke mukagule kuuti umwana ghwa muunhu ali nu vutavulua vwa kusaghila isambi mu iisi. nukukuvula uve, 'sisimuka utole ilitefu lyako ulutaghe ku nyumba jako
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 unsiki ghughuo akasisimuka pa vulongolo pa veeve, akatola ilitefu lwake ghuno akaghonile. pe akagomoka kwa mwene na kukumughinia uNguluve.
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 avaanhu voni vakadeghisivue na kumwimika uNguluve. vakamemilue nu vwoghofi vakatisagha,”tusaghile sino nasajaatu umusyughu”
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 pe lino ye ghahumile aghuo, uYesu alyahumile ukuo kuhuma ukuo na kukumwagha unsongesia songo juno akemeluagha Lawi ikalile ulubale lwa kusongekesia isongo, akavavula akati, “mbingilile”
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 pe uLawi akima na kumbingilila, akafileka ifinu fyoni kunsana.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 pe uLawi akavika ku nyumba ja mwene ikikulukulu ikikome vwimila Yesu. pe valyale avasonesia songo vinga na vaanhu avange vinga vakikalile pamesa na pilia palikimo na veene.
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 neke avaFarisayi na valembi vaave valyale vikuvasukunalila avavulanisivua, vakati, “kiki mulia na pinyua na vasongesia songo palikimo na vaanhu avange avanya sambi?”
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 uYesu akavamula akati, “avaanhu vano va nu vwumi uvunono navanoghile kukumulonda umughanga, neke vala veene vano vatamu vevene vikumulonda umughanga.
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 nanikisile kuvakemhela avanya kyang'ani neke valate, looli kuvakemela avanya sambi vapate kulaata”
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 vakam'bula vakati, “avavulanisivua va Yohani ke kinga vitogha kukidunda na kusuma, avavulanisivua na vafarisayi vope vivomba vule vule. neke avavulanisivua vako vilia na kunyua”
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 uYesu akavavula akati, “jiwesekana umuunhu ghweni kudinda uvutolani kuvano vaghongolilue unsiki ghuno unyavutolani ajighe navo?
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 neke ifighono filikwisa unsiki ghuno unyavutolani vikum'busia ku veene, pepano mu fighono ifio ilidinda.
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 pe uYesu akajova navo kange ku kihwani akati,”nakwale umuunhu juno idemula ulubale lwa mwenda kuhuma mu mwenda umpya na kuhonela mu mwenda un'kulu. nave ivomba nahele, idemula umwenda umpya nu lubale lwa mwenda umpya nakwale kinoghela kuhonela mu mwenda un'kulu.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 kange nakwale umuunhu juno ivika uluhuje ulupia mu supa ing'ulu, ndeve ivomba ndikio, uluhuje ulupia lwale lubajula isupa jila, nu luhuje lwale lukung'ika ni supa sale sibajuka.
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 neke uluhuje uupia lunoghile kuvika mu supa imia.
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 kange nakwale umuunhu juno alekile pinyua uluhuje ulupia neke anyue ulukulu, ulwakuva viiti ulwapakali lwe lunono kukila”
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luuka 5 >