< Левит 7 >

1 А оце зако́н жертви за провину, — Найсвятіше вона.
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
2 На місці, де ріжуть цілопаления, заріжуть жертву за провину, а кров її священик покропить на жертівника навколо.
Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 А ввесь її лій із неї він принесе́, — курдюка́, і лій, що покриває ну́трощі,
Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
4 і оби́дві нирки, і лій, що на них, що на стегнах, а сальника на печінці здійме з нирками,
zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
5 та й спалить те священик на жертівнику, — це огняна́ жертва для Господа, жертва за провину вона.
Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
6 Кожен чоловічої статі серед священиків буде їсти її, — на місці святому буде вона їджена, Найсвятіше вона.
Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
7 Як про жертву за гріх, так само про жертву за провини — зако́н їм один: священикові, що очистить нею, йому вона буде.
Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
8 А священик, що приносить чиєсь цілопалення, — шкура цілопалення, яке приніс він, священикові, йому вона бу́де.
Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
9 І кожна жертва хлібна, що в печі буде печена, і кожна пригото́влена в горшку та на лопатці, — священикові, що приносить її, йому вона бу́де.
Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
10 А кожна хлібна жертва, мішана в оливі й суха, — буде вона всім синам Аароновим, як одному, так і другому.
Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
11 А оце зако́н про мирну жертву, що хтось принесе її Господе́ві.
Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
12 Якщо принесе її на подяку, то він принесе на жертву подяки прісні калачі́, мішані в оливі, і прісні коржі, помазані оливою, і вимішана пшенична мука, калачі, мішані в оливі.
Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
13 Разом із калачами ква́шеного хліба принесе він жертву свою, при мирній жертві подяки його.
Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
14 І принесе він щось одне з кожної жертви, — прино́шення для Господа; це буде священикові, що кро́пить кров мирної жертви, — буде йому.
Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
15 А м'ясо мирної жертви подяки його буде їджене в дні його жертви, — не позоставить із нього нічо́го до ра́нку.
Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
16 А якщо жертва його прино́шення — обі́тниця, або добровільний дар, то вона буде їджена в день прине́сення ним його жертви, а позостале з неї й назавтра буде їджене.
Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
17 А позостале з м'яса кривавої жертви в третім дні буде спалене.
Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
18 А якщо справді буде їджене з м'яса мирної жертви його в третім дні, то не буде вподо́баний той, хто прино́сить її, — це не буде залічене йому, буде не́чисть; а хто їстиме з неї, понесе свій гріх.
Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
19 А те м'ясо, що доторкнеться до чогось нечистого, не бу́де їджене, — на огні буде спа́лене. А м'ясо чисте — кожен чистий буде їсти м'ясо.
Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
20 А душа, що буде їсти м'ясо з мирної жертви, що вона Господня, а не́чисть його на ньому, то буде вона винищена з наро́ду свого́.
Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
21 А коли хто доторкнеться до чогось нечистого, до нечистоти лю́дської, або до нечистої худоби, або до всього нечистого плазу́ючого, та проте буде їсти з м'яса мирної жертви, що Господня вона, то буде той ви́нищений із наро́ду свого“.
Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
22 І Господь промовляв до Мойсея, говорячи:
Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
23 „Кажи до Ізраїлевих синів, говорячи: жодного лою волового, ані овечого, ані козиного не бу́дете їсти.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
24 А лій із па́дла й лій пошмато́ваного буде вживаний для всякої потреби, але їсти — не будете їсти його́.
Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
25 Бо кожен, хто їсть лій із худоби, що з неї приносить огняну́ жертву для Господа, то душа та, що їсть, буде ви́нищена з наро́ду свого́.
Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
26 І жодної крови пта́ства та худоби не будете їсти по всіх ваших осе́лях.
Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
27 Кожна душа, що їстиме яку-будь кров, — то буде винищена душа та з-посеред наро́ду свого́“.
Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
28 І Господь промовляв до Мойсея, говорячи:
Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
29 „Промовляй до Ізраїлевих синів, говорячи: Хто приносить свою мирну жертву до Господа, той принесе своє прино́шення Господе́ві з своєї мирної жертви.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
30 Руки його принесу́ть огняні жертви Господні, — лій із грудиною, принесе груди́ну, щоб колиха́ти її, як колиха́ння перед Господнім лицем.
Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
31 І священик спалить той лій на же́ртівнику. А та грудина буде Ааронові та синам його.
Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
32 А праве стегно з мирних же́ртов ваших дасте священикові, як прино́шення.
Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
33 Хто з Ааро́нових синів приносить кров мирних жертов та лій, — йому буде на па́йку праве стегно́.
Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
34 Бо Я взяв від Ізраїлевих синів грудину колиха́ння й стегно прино́шення з мирних жертов їхніх, та й дав їх священикові Ааро́нові й синам його на вічну постанову від Ізраїлевих синів.
Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
35 Оце ча́стка з пома́зання Ааро́на та частка з пома́зання синів його з огняни́х же́ртов Господніх у день прино́шення їх на священнослу́ження Господе́ві,
Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
36 що наказав Госпо́дь давати їм у день їхнього пома́зання від Ізра́їлевих синів, — вічна постанова на їхні покоління!
Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
37 Оце зако́н про цілопа́лення, про хлібну жертву, і про жертву за гріх, і про жертву за прови́ну, і про посвя́чення, та про жертву мирну,
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
38 що Госпо́дь наказав був Мойсеєві на Сіна́йській горі в день нака́зу Його Ізра́їлевим синам прино́сити жертви свої Господе́ві в Сіна́йській пусти́ні“.
ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”

< Левит 7 >