< До колоссян 1 >

1 Павло, із волі Божої апо́стол Христа Ісуса, і брат Тимофі́й
Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu,
2 до святих і вірних братів у Христі, що в Коло́сах: благода́ть вам і мир від Бога, Отця нашого!
kwa waumini na ndugu waaminifu katika Kristo walioko Kolosai. Neema iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3 Ми дякуємо Богові, Отцеві Господа нашого Ісуса Христа, за́вжди за вас мо́лячись,
Tunatoa shukrani kwa Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na tunawaombea mara kwa mara.
4 прочувши про вашу віру в Христа Ісуса та про любов, яку маєте до всіх святих
Tumesikia imani yenu katika Yesu Kristo na upendo mlionao kwa wale wote waliotengwa kwa ajili ya Mungu.
5 через надію, пригото́вану в небі для вас, що про неї давніше ви чули в слові правди Єва́нгелії,
Mna upendo huu kwa sababu ya taraja la uhakika lililohifadhiwa mbinguni kwa ajili yenu. Mlisikia kuhusu taraja hiyo ya uhakika kabla katika neno la kweli, injili,
6 що до вас прибула́, і на ці́лому світі плодоно́сна й росте, як і в вас, з того дня, коли ви почули й пізнали благодать Божу в правді.
ambayo imekuja kwenu. Injili hii inazaa tunda na inaenea ulimwenguni kote. Imekuwa ikifanya hivi ndani yenu pia tangu siku mlipoisikia na kujifunza kuhusu neema ya Mungu katika kweli.
7 Отак ви і навчилися від Епа́фра, улю́бленого співробі́тника нашого, що за вас він вірний служитель Христа,
Hii ndiyo injili mliyojifunza kutoka kwa Epafra, mpendwa wetu mtumishi mwenzetu, ambaye ni mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8 що й виявив нам про вашу духовну любов.
Epafra ameufanya ujulikane kwetu upendo wenu katika Roho.
9 Через це то й ми з того дня, як почули, не перестаємо молитись за вас та просити, щоб для пізна́ння волі Його були́ ви напо́внені всякою мудрістю й розумом духовним,
Kwa sababu ya upendo huu, tangu siku tuliposikia hivi, hatujaacha kuwaombea. Tumekuwa tukiomba kwamba mtajazwa na maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa kiroho.
10 щоб ви пово́дилися нале́жно щодо Господа в усякому дого́дженні, в усякому доброму ді́лі прино́сячи плід і зростаючи в пізна́нні Бога,
Tumekuwa tukiomba kwamba mtatembea kwa ustahimilivu wa Bwana katika njia zipendezazo. Tumekuwa tukiomba kwamba mtazaa tunda katika kila tendo jema na kwamba mtakua katika maarifa ya Mungu.
11 зміцняючись усякою силою за могутністю слави Його для всякої витрива́лости й довготерпі́ння з радістю,
Tunaomba mweze kutiwa nguvu katika kila uwezo kulingana na nguvu za utukufu wake katika uvumilivu na ustahimilivu wote.
12 дя́куючи Отцеві, що вчинив нас достойними участи в спа́дщині святих у світлі,
Tunaomba kwamba, kwa furaha, mtatoa shukrani kwa Baba, aliyewafanya ninyi mweze kuwa na sehemu katika urithi wa waumini katika nuru.
13 що визволив нас із вла́ди те́мряви й переставив нас до Царства Свого улю́бленого Сина,
Ametuokoa kutoka katika utawala wa giza na kutuhamishia katika ufalme wa Mwana wake mpendwa.
14 в Якім маємо відку́плення і про́щення гріхів.
Katika Mwanae tuna ukombozi, msamaha wa dhambi.
15 Він є образ невиди́мого Бога, ро́джений перш усякого тво́рива.
Mwana ni mfano wa Mungu asiyeonekana. Ni mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote.
16 Бо то Ним ство́рено все на небі й на землі, види́ме й невиди́ме, чи то престоли, чи то госпо́дства, чи то влади, чи то начальства, — усе через Нього й для Нього створено!
Kwakuwa kwa yeye vitu vyote viliumbwa, vile vilivyoko mbinguni na vilivyoko duniani, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. ikiwa ni vya enzi au mamlaka au utawala au wenye nguvu, vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
17 А Він є перший від усього, і все в Нім стоїть.
Yeye amekuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
18 І Він — Голова тіла, Церкви. Він початок, перворо́джений з мертвих, щоб у всьому Він мав пе́ршенство.
Na yeye ndiye kichwa cha mwili yaani kanisa, yeye ni mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka miongoni mwa wafu, hivyo, ana nafasi ya kwanza miongoni mwa vitu vyote.
19 Бо вгодно було́, щоб у Нім перебува́ла вся повнота́,
Kwa kuwa Mungu alipendezwa kwamba utimilifu wake wote uishi ndani yake,
20 і щоб Ним поєднати з Собою все, примиривши кров'ю хреста Його, через Нього, чи то зе́мне, чи то небесне.
na kupatanisha vitu vyote kwake kwa njia ya Mwanawe. Mungu alifanya amani kupitia damu ya msalaba wake. Mungu alipatanisha vitu vyote kwake mwenyewe, ikiwa ni vitu vya duniani au vitu vya mbinguni.
21 І вас, що були́ колись відчужені й вороги думкою в злих учинках,
Nanyi pia, kwa wakati mmoja mlikuwa wageni kwa Mungu na mlikuwa maadui wake katika akili na matendo maovu.
22 тепер же примирив смертю в лю́дськім тілі Його, щоб учинити вас святими, і непорочними, і неповинними перед Собою,
Lakini sasa amewapatanisha ninyi kwa mwili wake kupitia kifo. Alifanya hivi ili kuwaleta ninyi watakatifu, wasio na lawama na bila dosari mbele yake,
23 якщо тільки пробува́єте в вірі тверді́ та ста́лі, і не відпадаєте від надії Єва́нгелії, що ви чули її, яка проповідана всьому створі́нню під небом, якій я, Павло, став служи́телем.
kama mkiendelea katika imani, mliyoimarishwa na kuwa thabiti, pasipo kuondoshwa mbali kutoka kwenye taraja la ujasiri la injili mliyoisikia. Hi ndiyo injili iliyotangazwa kwa kila mtu aliyeumbwa chini ya mbingu. Hii ndiyo injili ambayo kwayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi.
24 Тепер я радію в стражда́ннях своїх за вас, і доповнюю недостачу скорбо́ти Христової і тілі своїм за тіло Його, що воно — Церква;
Sasa nafurahia mateso yangu kwa ajili yenu. Nami natimiliza katika mwili wangu kinachopungua kwa mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
25 якій я став служи́телем за Божим заря́дженням, що для вас мені дане, щоб виконати Слово Боже, —
Mimi ni mtumishi wa kanisa hili, sawasawa na wajibu niliopewa kutoka kwa Mungu kwa ajili yenu, kulijaza neno la Mungu.
26 Таємницю, захо́вану від віків і поколінь, а тепер виявлену Його святим, (aiōn g165)
Huu ni ukweli wa siri iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi na kwa vizazi. Lakini sasa imefunuliwa kwa wote waaminio katika Yeye. (aiōn g165)
27 що їм Бог захотів показати, яке багатство слави цієї таємниці між поганами, а вона — Христос у вас, надія слави!
Ni kwa wale ambao Mungu alitaka kufunua kulivyo utajiri wa utukufu wa siri ya ukweli huu miongoni mwa Mataifa. Ni kwamba Kristo yumo ndani yenu, ujasiri wa utukufu ujao.
28 Його ми проповідуємо, нагадуючи кожній люди́ні й навчаючи кожну люди́ну всякої мудрости, щоб учинити кожну люди́ну досконалою в Христі.
Huyu ndiye tunayemtangaza. Tunamwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote, ili kwamba tumlete kila mtu mkamilifu katika Kristo.
29 У то́му й працюю я, борючи́ся силою Його, яка сильно діє в мені.
Kwa jili hii, mimi najibidisha na kujitahidi kulingana na nguvu yake ifanyayo kazi ndani yangu katika uweza.

< До колоссян 1 >