< 2 до коринтян 7 >

1 Отож, мої любі, мавши ці обі́тниці, очистьмо себе від усякої не́чисти тіла та духа, — і творімо святиню у Божім страху́!
Wapendwa wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizi, na tujitakase wenyewe kwa kila jambo ambalo linatufanya kuwa wachafu katika miili yetu na katika roho. Na tuutafute utakatifu katika hofu ya Mungu.
2 Дайте місце для нас! Ми ніко́го не скривдили, ніко́го не зіпсували, нікого не ошука́ли!
Fanyeni nafasi kwa ajili yetu! Hatujamkosea mtu yeyote. Hatukumdhuru mtu yeyote. Hatujajinufaisha kwa faida ya mtu yeyote.
3 Говорю́ не на о́суд, бо я перед тим був сказав, що ви в серцях наших, щоб нам із вами чи померти чи жити.
Nasema hili siyo kwa kuwalaumu. Kwa kuwa nimeshasema kwamba mmo mioyoni mwetu, kwetu sisi kufa pamoja na kuishi pamoja.
4 У мене велика сміли́вість до вас, велика мені похвала́ з вас, я повний потіхи, збагачаюся радістю при всякому нашому горі.
Nina ujasiri mwingi ndani yenu, na ninajivuna kwa ajili yenu. Nimejawa na faraja. Ninajawa na furaha hata katikati ya mateso yetu yote.
5 Бо коли ми прийшли в Македо́нію, тіло наше не мало спочинку нія́кого, у всьому бідуючи: назовні — бої, страхіття — всере́дині.
Tulikuja Makedonia, miili yetu haikuwa na pumziko. Badala yake, tulipata taabu kwa namna zote kwa kupigwa vita upande wa nje na hofu upande wa ndani.
6 Але Бог, що тішить прини́жених, потішив нас при́ходом Тита,
Lakini Mungu, anayefariji waliokata tamaa, alitufariji kwa ujio wa Tito.
7 і не тільки його прибуття́м, а й поті́шенням, що ним він потішився з вас, коли розповідав нам про вашу журбу́, про ваш смуток, про вашу горли́вість до мене, так що я більше тішився.
Haikuwa kwa ujio wake tu kwamba Mungu alitufariji. ilikuwa pia faraja zile Tito alizopokea kutoka kwenu. Yeye alituambia upendo mkuu mlionao, huzuni yenu, na mlivyokuwa na wasiwasi kwa ajili yangu. Hivyo nimezidi kuwa na furaha zaidi.
8 Коли я й засмутив вас листом, то не каюся, хоч і каявся був, бо бачу, що той лист засмутив вас, хоч і часово.
Hata ingawa waraka wangu uliwafanya kusikitika, mimi siujutii. lakini ninaujutia wakati nilipoona waraka huo uliwafanya ninyi kuwa na huzuni. lakini mlikuwa na huzuni kwa muda mfupi.
9 Я радію тепер не тому́, що ви засмутились, а що ви засмутилися на покая́ння, бо ви засмутились для Бога, щоб ні в чо́му не мати втрати від нас.
Sasa nina furaha, si kwa sababu mlikuwa na shida, lakini kwa sababu huzuni zenu iliwaleta kwenye toba. Mlipatwa na huzuni ya kiungu, hivyo mliteswa si kwa hasara kwa sababu yetu.
10 Бо смуток для Бога чинить каяття́ на спасі́ння, а про нього не жалуємо, а смуток світськи́й — чинить смерть.
Kwa kuwa huzuni ya kiungu huleta toba ambayo hukamilisha wokovu bila ya kuwa na majuto. Huzuni ya kidunia, hata hivyo, huleta mauti.
11 Бо ось саме це, що ви засмутились для Бога, яку пильність велику воно вам зробило, яку оборону, яке обурення, який страх, яке бажа́ння, яку горливість, яку по́мсту! Ви в усім показали, що чисті ви в справі.
Angalieni huzuni hii ya kiungu ilizalisha azma gani kubwa ndani yenu. Jinsi gani azma ilikuwa kubwa ndani yenu kuthibitisha kuwa hamkuwa na hatia. Kwa jinsi gani uchungu wenu ulivyokuwa mkubwa, hofu yenu, matamanio yenu, bidii yenu, na shauku yenu kuona kwamba haki inapaswa kutendeka! Katika kila jambo mmethibitisha wenyewe kutokuwa na hatia.
12 А коли я й писав вам, то не через того, хто кри́вдить, і не через покри́вдженого, а щоб виявилася для вас наша пильність про вас перед Богом.
Ingawa niliwaandikia ninyi, sikuandika kwa ajili ya mkosaji, wala si kwa mtu aliyeteswa na maovu. Nimeandika ili kwamba udhati wa mioyo yenu kwa ajili yetu ifanywe kujulikana kwenu mbele ya macho ya Mungu.
13 Тому́ то потіхою вашою вті́шились ми, а ще більше зраділи ми радістю Тита, що ви всі заспоко́їли духа його.
Ni kwa ajili ya hii kwamba tunafarijika. Katika nyongeza ya faraja yetu wenyewe, tunafurahi pia, hata zaidi kwa sababu ya furaha ya Tito, kwa kuwa roho yake iliburudishwa na ninyi nyote.
14 Бо коли я про вас йому чим похвалився, то не осоро́мився; але як ми вам говорили все правду, так і наша хвала́ перед Титом правдива була́!
Kwa kuwa kama nilijivuna kwake kuhusiana na ninyi, sikuwa na aibu. Kinyume chake, kama tu kila neno tulilolisema kwenu lilikuwa kweli, Majivuno yetu kuhusu ninyi kwa Tito yalithibitisha kuwa kweli.
15 І серце його прихильніше до вас, коли згадує він про покору всіх вас, як його прийняли́ ви були зо стра́хом і тремті́нням.
Upendo wake kwa ajili yenu hata ni mkubwa zaidi, kama akumbukapo utii wenu nyote, jinsi mlivyomkaribisha yeye kwa hofu na kutetemeka.
16 Отож, тішуся я, що мо́жу покластись у всьому на вас!
Ninafurahi kwa sababu nina ujasiri kamili ndani yenu.

< 2 до коринтян 7 >