< Від Луки 21 >

1 Поглянувши ж добачив, як кидали дари свої в скарбону заможні.
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2 Побачив же й одну вдовицю вбогу, що кидала туди дві лепти.
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3 І рече: Правдиво глаголю вам, що вдовиця вбога ся більш усїх укинула:
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4 всі бо ті з достатку свого кидали у дари Божі, ся ж з недостатку свого увесь прожиток свій, що мала, вкинула.
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
5 І як деякі говорили про церкву, що каміннєм красним та посьвятами украшена, рече:
Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
6 Із сього, що бачите, прийдуть днї, в котрі не зоставить ся камінь на камені, щоб не зруйновано.
“Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
7 Питали ж Його, кажучи: Учителю, коли ж се буде? й що за ознака коли се мав стати ся?
Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
8 Він же рече: Гледїть, щоб не була введені; многі бо прийдуть в імя моє, кажучи: Що се я. А час приближив ся; не йдіть же за вами.
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
9 Яв же почуєте про войни та ворохобнї, не полохайтесь; мусить бо перш се статись; тільки ж не зараз конець.
Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
10 Тодї рече їм: Устане нарід на нарід і царство на царство,
Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
11 і трус великий по місцях, і голоднеча, й помір буде, й страхи, й о-внаки з неба великі будуть.
Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
12 Та перш того всього наложать на вас руки свої і гонити муть, видаючи в школи й темницї, і водячи перед царі та ігемони задля імя мого.
“Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
13 І станеть ж воно вам на сьвідкуваннє.
Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
14 Постановіть же в серцях, ваших наперед, не готовитись відказувати:
Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
15 я бо дам вам уста й премудрість, котрій не здолїють противитись, анї встояти усї противники ваші.
Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
16 Будете ж видавані й від родителїв, і братів, і родини, й приятелїв; і вбивати муть деяких з вас.
Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
17 І будете ненавиджені від усіх задля імя мого.
Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
18 Та й волосина з голови вашої не загине.
Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
19 У терпінню вашому осягнїть душі ваші.
Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
20 Як же побачите, що обгорнуто таборами Єрусалим, тоді знайте, що наближило ся спустїннє його.
“Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
21 Тодї, хто в Юдеї, нехай біжять у гори; а хто в середині в йому, нехай виходять; а ті, що по селах, нехай не ввіходять у него.
Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
22 Бо се днї мести, щоб справдилось усе написане.
Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
23 Горе ж важким і годуючим у ті днї! буде бо біда велика на землі, і гнів на народі сьому.
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
24 І поляжуть від гострого меча, й позаймані будуть у полонь до всіх поган; і топтати муть Єрусалим погане, доки сповнять ся часи поган.
Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
25 І будуть ознаки на сонцї, й місяці, й зорях, а на землї переполох народів у ваколотї; як зареве море та филї.
“Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
26 І омертвіють люде від страху та дожидання того, що прийде на все-денну: сили бо небесні захитають ся.
Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
27 І тодї побачять Сина чоловічого йдучого на хмарі з силою і славою великою.
Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
28 Як же почне се діятись, випростуйтесь і підіймайте голови ваші; бо наближилось викупленнє ваше.
Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
29 І сказав приповість їм: Бачте смоківницю і всякі дерева:
Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
30 Як розпукутоть ся вже, бачивши самі розумієте, що вже близько лїто.
Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
31 Так і ви, коли побачите, як се станеть ся, знайте, що близько царство Боже.
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Істино глаголи вам: Ще не перейде рід сей, доки все станеть ся.
“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
33 Небо й земля перейде, слова ж мої не перейдуть.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
34 Остерегайте ся ж, щоб часом не обтягчились ваші серця прожорством та пянством, та журбою життя сього, й щоб несподівано на вас не настиг день той.
“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
35 Бо, як сітка, впаде на всіх, що живуть на лицї всієї землі.
Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
36 Пильнуйте, по всяк час молячись, щоб удостоїли ся втекти від того всього, що має статись, і станути перед Сином чоловічим.
Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
37 Навчав же днями в церкві, ночами ж виходячи, пробував на горі, званій Оливною.
Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
38 Усї ж люде сходились рано до Него в церкву слухати Його.
Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.

< Від Луки 21 >