< До євреїв 1 >

1 Почасту і всяково промовляючи здавна Бог до батьків через пророків,
Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
2 в останнї сї днї глаголав до нас через Сина, котрого настановив наслїдником усього, котрим і віки створив. (aiōn g165)
lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
3 Сей, будучи сяєвом слави і обра-аом особи Його, і двигаючи все словом сили своєї, зробивши собою очищеннє гріхів наших, осївсь по правицї величчя на вишинах,
Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
4 Стільки луччнй будучи від ангелів, скільки славнїще над їх наслїдував імя.
Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
5 Кому бо рече коли з ангелів: Син мій єси Ти, я сьогоднї родив Тебе? і знов: Я буду Йому Отцем, а Він буде менї Сином?
Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
6 Коли ж знов уводить Перворідня у вселенну, глаголе: І нехай поклонять ся Йому всї ангели Божі.
Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
7 І до ангелів же глаголе: Що творить духи ангелами своїми, а поломе огня слугами своїми.
Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
8 Про Сина ж; Престол Твій, Боже, по вік вічний, палиця правоти - палиця царювання Твого. (aiōn g165)
Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
9 Полюбив єси правду, і зненавидів беззаконнє; за се помазав тебе, Боже, Бог твій єлеєм радости більш спільників Твоїх.
Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
10 І (знов): У починї Ти, Господи, землю оснував єси, і небеса - дїло рук Твоїх.
Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 Вони зникнуть. Ти ж пробуваєш, і всї, як шати зветшають,
Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
12 і як одежину згорнеш їх, і перемінять ся; Ти ж той же самий єси, і лїта Твої не скінчать ся.
Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
13 Кому ж із ангелів сказав коли: Сиди по правиці в мене, доки положу ворогів Твоїх підніжком ніг Твоїх?
Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
14 Чи не всї ж вони служебні духи, посилаєм! на служеннє про тих, що хочуть наслідувати спасеннє?
Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.

< До євреїв 1 >