< Zekeriya 1 >

1 Darius'un krallığının ikinci yılının sekizinci ayında RAB İddo oğlu Berekya oğlu Peygamber Zekeriya aracılığıyla şöyle seslendi:
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 “RAB atalarınıza çok öfkelendi.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Bu nedenle halka de ki, Her Şeye Egemen RAB böyle diyor: ‘Her Şeye Egemen RAB, bana dönün’ diyor; ‘Ben de size dönerim diyor Her Şeye Egemen RAB.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Atalarınız gibi davranmayın! Önceki peygamberler, Her Şeye Egemen RAB kötü yollarınızdan ve kötü uygulamalarınızdan dönün diyor, diyerek onları uyardılar. Ne var ki, onlar dinlemediler, bana aldırış etmediler. Böyle diyor RAB.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Hani atalarınız nerede? Peygamberler de sonsuza kadar mı yaşar?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 Peygamber kullarıma buyurduğum sözler ve kurallar atalarınıza ulaşmadı mı?’ “Onlar da dönüp, ‘Her Şeye Egemen RAB yollarımıza ve uygulamalarımıza bakarak bizim için ne düşündüyse aynen yaptı’ dediler.”
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 Darius'un krallığının ikinci yılında, on birinci ay olan Şevat ayının yirmi dördüncü günü RAB İddo oğlu Berekya oğlu Peygamber Zekeriya'ya görümlerle seslendi.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 Gece vadideki mersin ağaçlarının arasında kızıl ata binmiş bir adam gördüm. Arkasında kızıl, kula ve beyaz atlar vardı.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 “Efendim, bunlar ne?” diye sordum. Benimle konuşan melek, “Bunların ne olduğunu sana göstereceğim” diye yanıtladı.
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 Mersin ağaçları arasında duran adam da, “Bunlar dünyayı dolaşmak için RAB'bin gönderdikleridir” diye açıkladı.
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 Mersin ağaçları arasında duran RAB'bin meleğine, “Dünyayı dolaştık” dediler, “İşte bütün dünya esenlik ve güvenlik içinde!”
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Bunun üzerine RAB'bin meleği, “Ey Her Şeye Egemen RAB, yetmiş yıldır öfkelendiğin Yeruşalim'den ve Yahuda kentlerinden sevecenliğini ne zamana dek esirgeyeceksin?” dedi.
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 RAB benimle konuşan meleği tatlı, avutucu sözlerle yanıtladı.
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 Bunun üzerine benimle konuşan melek, “Şunu duyur!” dedi, “Her Şeye Egemen RAB, ‘Yeruşalim ve Siyon için büyük kıskançlık duyuyorum’ diyor,
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 ‘Tasasız uluslara ise çok öfkeliyim; çünkü ben biraz öfkelenmiştim, onlarsa kötülüğe kötülük kattılar.’
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 “Onun için RAB, ‘Yeruşalim'e sevecenlikle döneceğim’ diyor, ‘Tapınağım orada yeniden kurulacak ve Yeruşalim üzerine ölçü ipi çekilecek!’ Böyle diyor Her Şeye Egemen RAB.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 “Şunu da duyur: Her Şeye Egemen RAB, ‘Kentlerim yine bollukla dolup taşacak’ diyor, ‘Ben RAB, Siyon'u yine avutacağım, Yeruşalim'i yine seçeceğim.’”
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 Sonra gözlerimi kaldırıp baktım, dört boynuz vardı.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 Benimle konuşan meleğe, “Bunlar ne?” diye sordum. Melek, “Bunlar Yahuda, İsrail ve Yeruşalim halkını dağıtmış olan boynuzlardır” diye karşılık verdi.
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 Sonra RAB bana dört usta gösterdi.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 “Bunlar ne yapmaya geliyor?” diye sordum. Melek, “Şu boynuzlar Yahuda halkını öyle dağıttı ki, kimse başını kaldıramadı” dedi, “Bu ustalar da Yahuda halkını dağıtmak için boynuz kaldıran ulusları yıldırıp boynuzlarını yere çalmaya geldiler.”
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zekeriya 1 >