< Romalilar 11 >

1 Öyleyse soruyorum: Tanrı kendi halkından yüz mü çevirdi? Kesinlikle hayır! Ben de İbrahim soyundan, Benyamin oymağından bir İsrailli'yim.
Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2 Tanrı önceden bildiği kendi halkından yüz çevirmedi. Yoksa İlyas'la ilgili bölümde Kutsal Yazı'nın ne dediğini, İlyas'ın Tanrı'ya nasıl İsrail'den yakındığını bilmez misiniz?
Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3 “Ya Rab, senin peygamberlerini öldürdüler, senin sunaklarını yıktılar. Yalnız ben kaldım. Beni de öldürmeye çalışıyorlar.”
“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?”
4 Tanrı'nın ona verdiği yanıt nedir? “Baal'ın önünde diz çökmemiş yedi bin kişiyi kendime ayırdım.”
Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: “Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali.”
5 Aynı şekilde, şimdiki dönemde de Tanrı'nın lütfuyla seçilmiş küçük bir topluluk vardır.
Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6 Eğer bu, lütufla olmuşsa, iyi işlerle olmamış demektir. Yoksa lütuf artık lütuf olmaktan çıkar!
Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7 Sonuç ne? İsrail aradığına kavuşamadı, seçilmiş olanlar ise kavuştular. Geriye kalanlarınsa yürekleri nasırlaştırıldı.
Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8 Yazılmış olduğu gibi: “Tanrı onlara uyuşukluk ruhu verdi; Bugüne dek görmeyen gözler, duymayan kulaklar verdi.”
kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao.”
9 Davut da şöyle diyor: “Sofraları onlara tuzak, Kapan, tökez ve ceza olsun.
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10 Gözleri kararsın, göremesinler. Bellerini hep iki büklüm et!”
Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!”
11 Öyleyse soruyorum: İsrailliler, bir daha kalkmamak üzere mi sendeleyip düştüler? Kesinlikle hayır! Ama onların suçu yüzünden öteki uluslara kurtuluş verildi; öyle ki, İsrailliler onlara imrensin.
Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12 Eğer İsrailliler'in suçu dünyaya zenginlik, bozgunu uluslara zenginlik getirdiyse, bütünlüğü çok daha büyük bir zenginlik getirecektir!
Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13 Öteki uluslardan olan sizlere söylüyorum: Uluslara elçi olarak gönderildiğim için görevimi yüce sayarım.
Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14 Böylelikle belki soydaşlarımı imrendirip bazılarını kurtarırım.
nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15 Çünkü onların reddedilmesi dünyanın Tanrı'yla barışmasını sağladıysa, kabul edilmeleri ölümden yaşama geçiş değil de nedir?
Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16 Hamurun ilk parçası kutsalsa, tümü kutsaldır; kök kutsalsa, dallar da kutsaldır.
Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17 Ama zeytin ağacının bazı dalları kesildiyse ve sen yabanıl bir zeytin filiziyken onların yerine aşılanıp ağacın semiz köküne ortak oldunsa, o dallara karşı övünme. Eğer övünüyorsan, unutma ki, sen kökü taşımıyorsun, kök seni taşıyor.
Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19 O zaman, “Ben aşılanayım diye dallar kesildi” diyeceksin.
Lakini utasema: “Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake.”
20 Doğru, onlar imansızlık yüzünden kesildiler. Sense imanla yerinde duruyorsun. Böbürlenme, kork!
Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21 Çünkü Tanrı asıl dalları esirgemediyse, seni de esirgemeyecektir.
Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22 Onun için Tanrı'nın iyiliğini de sertliğini de gör. O, düşenlere karşı serttir; ama O'nun iyiliğine bağlı kalırsan, sana iyi davranır. Yoksa sen de kesilip atılırsın!
Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23 İmansızlıkta direnmezlerse, İsrailliler de öz ağaca aşılanacaklar. Çünkü Tanrı'nın onları eski yerlerine aşılamaya gücü vardır.
Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24 Eğer sen doğal yapısı yabanıl zeytin ağacından kesilip doğaya aykırı olarak cins zeytin ağacına aşılandınsa, asıl dalların öz zeytin ağacına aşılanacakları çok daha kesindir!
Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25 Kardeşler, bilgiçliğe kapılmamanız için şu sırdan habersiz kalmanızı istemem: İsrailliler'den bir bölümünün yüreği, öteki uluslardan kurtulacakların sayısı tamamlanıncaya dek duyarsız kalacaktır.
Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26 Sonunda bütün İsrail kurtulacaktır. Yazılmış olduğu gibi: “Kurtarıcı Siyon'dan gelecek, Yakup'un soyundan tanrısızlığı uzaklaştıracak.
Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27 Onların günahlarını kaldıracağım zaman Kendileriyle yapacağım antlaşma budur.”
Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 İsrailliler Müjde'yi reddederek sizin uğrunuza Tanrı'ya düşman oldular; ama Tanrı'nın seçimine göre, ataları sayesinde sevilmektedirler.
Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29 Çünkü Tanrı'nın armağanları ve çağrısı geri alınamaz.
Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30 Bir zamanlar Tanrı'nın sözünü dinlemeyen sizler şimdi İsrailliler'in sözdinlemezliğinin sonucu merhamete kavuştunuz.
Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31 Bunun gibi, İsrailliler de, sizin kavuştuğunuz merhametle merhamete erişmek için şimdi söz dinlemez oldular.
Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32 Çünkü Tanrı, merhametini herkese göstermek için herkesi sözdinlemezliğin tutsağı kıldı. (eleēsē g1653)
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
33 Tanrı'nın zenginliği ne büyük, bilgeliği ve bilgisi ne derindir! O'nun yargıları ne denli akıl ermez, yolları ne denli anlaşılmazdır!
Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34 “Rab'bin düşüncesini kim bilebildi? Ya da kim O'nun öğütçüsü olabildi?”
“Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35 “Kim Tanrı'ya bir şey verdi ki, Karşılığını O'ndan isteyebilsin?”
Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?”
36 Her şeyin kaynağı O'dur; her şey O'nun aracılığıyla ve O'nun için var oldu. O'na sonsuza dek yücelik olsun! Amin. (aiōn g165)
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Romalilar 11 >