< Vahiy 14 >

1 Sonra Kuzu'nun Siyon Dağı'nda durduğunu gördüm. O'nunla birlikte 144 000 kişi vardı. Alınlarında kendisinin ve Babası'nın adları yazılıydı.
Kisha nikaona mlima Sioni, na Mwanakondoo amesimama juu yake; pamoja naye walikuwa watu mia moja arobaini na nne elfu ambao juu ya paji za nyuso zao walikuwa wameandikwa jina la Mwanakondoo na jina la Baba yake.
2 Gökten, gürül gürül akan suların sesini, güçlü gök gürlemesini andıran bir ses işittim. İşittiğim ses, lir çalanların çıkardığı sese benziyordu.
Basi, nikasikia sauti kutoka mbinguni, sauti iliyokuwa kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa. Sauti niliyosikia ilikuwa kama sauti ya wachezaji muziki wakipiga vinubi vyao.
3 Bu 144 000 kişi, tahtın önünde, dört yaratığın ve ihtiyarların önünde yeni bir ezgi söylüyordu. Yeryüzünden satın alınmış olan bu kişilerden başka kimse o ezgiyi öğrenemedi.
Walikuwa wanaimba wimbo mpya mbele ya kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe hai wanne na wale wazee. Hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao watu mia moja arobaini na nne elfu waliokombolewa duniani.
4 Kendilerini kadınlarla lekelememiş olanlar bunlardır. Pak kişilerdir. Kuzu nereye giderse ardısıra giderler. Tanrı'ya ve Kuzu'ya ait olacakların ilk bölümü olmak üzere insanlar arasından satın alınmışlardır.
Watu hao ndio wale waliojiweka safi kwa kutoonana kimwili na wanawake, nao ni mabikira. Wao humfuata Mwanakondoo kokote aendako. Wamekombolewa kutoka miongoni mwa binadamu wengine, wakawa wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwanakondoo.
5 Ağızlarından hiç yalan çıkmamıştır. Kusursuzdurlar.
Hawakupata kamwe kuwa waongo; hawana hatia yoyote.
6 Bundan sonra göğün ortasında uçan başka bir melek gördüm. Yeryüzünde yaşayanlara –her ulusa, her oymağa, her dile, her halka– iletmek üzere sonsuza dek kalıcı olan Müjde'yi getiriyordu. (aiōnios g166)
Kisha nikamwona malaika mwingine anaruka juu angani akiwa na Habari Njema ya milele ya Mungu, aitangaze kwa watu wote waishio duniani, kwa mataifa yote, makabila yote, watu wa lugha zote na rangi zote. (aiōnios g166)
7 Yüksek sesle şöyle diyordu: “Tanrı'dan korkun! O'nu yüceltin! Çünkü O'nun yargılama saati geldi. Göğü, yeri, denizi, su pınarlarını yaratana tapının!”
Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumtukuza! Maana saa imefika ya kutoa hukumu yake. Mwabuduni yeye aliyeumba mbingu na nchi, bahari na chemchemi za maji.”
8 Ardından gelen ikinci bir melek, “Yıkıldı! Kendi azgın fuhuş şarabını bütün uluslara içiren büyük Babil yıkıldı!” diyordu.
Malaika wa pili alimfuata huyo wa kwanza akisema, “Ameanguka! Naam, Babuloni mkuu ameanguka! Babuloni ambaye aliwapa mataifa yote wainywe divai yake—divai kali ya uzinzi wake!”
9 Onları üçüncü bir melek izledi. Yüksek sesle şöyle diyordu: “Bir kimse canavara ve heykeline taparsa, alnına ya da eline canavarın işaretini koydurursa, Tanrı gazabının kâsesinde saf olarak hazırlanmış Tanrı öfkesinin şarabından içecektir. Böylelerine kutsal meleklerin ve Kuzu'nun önünde ateş ve kükürtle işkence edilecek.
Na malaika wa tatu aliwafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Yeyote anayemwabudu yule mnyama na sanamu yake na kukubali kutiwa alama yake juu ya paji la uso wake au juu ya mkono wake,
yeye mwenyewe atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu, ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake bila kuchanganywa na maji. Mtu huyo atateseka ndani ya moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele ya Mwanakondoo.
11 Çektikleri işkencenin dumanı sonsuzlara dek tütecek. Canavara ve heykeline tapıp onun adının işaretini alanlar gece gündüz rahat yüzü görmeyecekler. (aiōn g165)
Moshi wa moto unaowatesa kupanda juu milele na milele. Watu hao waliomwabudu huyo mnyama na sanamu yake, na kutiwa alama ya jina lake, hawatakuwa na nafuu yoyote usiku na mchana.” (aiōn g165)
12 Bu da, Tanrı'nın buyruklarını yerine getiren, İsa'ya imanlarını sürdüren kutsalların sabrını gerektirir.”
Kutokana na hayo, ni lazima watu wa Mungu, yaani watu wanaotii amri ya Mungu na kumwamini Yesu, wawe na uvumilivu.
13 Gökten bir ses işittim. “Yaz! Bundan böyle Rab'be ait olarak ölenlere ne mutlu!” diyordu. Ruh, “Evet” diyor, “Uğraşlarından dinlenecekler. Çünkü yaptıkları onları izleyecek.”
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika! Heri watu ambao tangu sasa wanakufa wakiwa wameungana na Bwana.” Naye Roho asema, “Naam! Watapumzika kutoka taabu zao; maana matunda ya jasho lao yatawafuata.”
14 Sonra beyaz bir bulut gördüm. Bulutun üzerinde “insanoğluna benzer biri” oturuyordu. Başında altın bir taç, elinde keskin bir orak vardı.
Kisha nikatazama, na kumbe palikuwapo wingu jeupe hapo. Na juu ya wingu hilo kulikuwa na kiumbe kama mtu. Alikuwa amevaa taji ya dhahabu kichwani, na kushika mundu mkononi mwake.
15 Tapınaktan çıkan başka bir melek bulutun üzerinde oturana yüksek sesle bağırdı: “Orağını uzat ve biç! Biçme saati geldi. Çünkü yerin ekini olgunlaşmış bulunuyor.”
Kisha malaika mwingine akatoka Hekaluni, na kwa sauti kubwa akamwambia yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu, “Tafadhali, tumia mundu wako ukavune mavuno, maana wakati wa mavuno umefika; mavuno ya dunia yameiva.”
16 Bulutun üzerinde oturan, orağını yerin üzerine salladı, yerin ekini biçildi.
Basi, yule aliyekuwa amekaa juu ya wingu akautupa mundu wake duniani, na mavuno ya dunia yakavunwa.
17 Gökteki tapınaktan başka bir melek çıktı. Onun da keskin bir orağı vardı.
Kisha malaika mwingine akatoka katika Hekalu mbinguni akiwa na mundu wenye makali.
18 Ateş üzerinde yetkili olan başka bir melek de sunaktan çıkıp geldi. Keskin orağı olana yüksek sesle, “Keskin orağını uzat!” dedi. “Yerin asmasının salkımlarını topla. Çünkü üzümleri olgunlaştı.”
Kisha malaika mwingine msimamizi wa moto, akatoka madhabahuni akamwambia kwa sauti kubwa yule malaika mwenye mundu wenye makali, “Nawe tia huo mundu wako mkali, ukakate vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva!”
19 Bunun üzerine melek orağını yerin üzerine salladı. Yerin asmasının ürününü toplayıp Tanrı öfkesinin büyük masarasına attı.
Basi, malaika huyo akautupa mundu wake duniani, akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya chombo kikubwa cha kukamulia zabibu, chombo cha ghadhabu ya Mungu.
20 Kentin dışında çiğnenen masaradan kan aktı. Kan, 1 600 ok atımı kadar yayılıp atların gemlerine dek yükseldi.
Zabibu zikakamuliwa ndani ya hilo shinikizo lililoko nje ya mji, na damu ikatoka katika shinikizo hilo mtiririko mrefu kiasi cha mita mia tatu na kina chake kiasi cha mita mia mbili.

< Vahiy 14 >