< Mezmurlar 33 >

1 Ey doğru insanlar, RAB'be sevinçle haykırın! Dürüstlere O'nu övmek yaraşır.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 Lir çalarak RAB'be şükredin, On telli çenk eşliğinde O'nu ilahilerle övün.
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 O'na yeni bir ezgi söyleyin, Sevinç çığlıklarıyla sazınızı konuşturun.
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Çünkü RAB'bin sözü doğrudur, Her işi sadakatle yapar.
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 Doğruluğu, adaleti sever, RAB'bin sevgisi yeryüzünü doldurur.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Gökler RAB'bin sözüyle, Gök cisimleri ağzından çıkan solukla yaratıldı.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Deniz sularını bir araya toplar, Engin suları ambarlara depolar.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 Bütün yeryüzü RAB'den korksun, Dünyada yaşayan herkes O'na saygı duysun.
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 Çünkü O söyleyince, her şey var oldu; O buyurunca, her şey belirdi.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 RAB ulusların planlarını bozar, Halkların tasarılarını boşa çıkarır.
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 Ama RAB'bin planları sonsuza dek sürer, Yüreğindeki tasarılar kuşaklar boyunca değişmez.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Ne mutlu Tanrısı RAB olan ulusa, Kendisi için seçtiği halka!
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 RAB göklerden bakar, Bütün insanları görür.
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 Oturduğu yerden, Yeryüzünde yaşayan herkesi gözler.
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 Herkesin yüreğini yaratan, Yaptıkları her şeyi tartan O'dur.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 Ne büyük ordularıyla zafer kazanan kral var, Ne de büyük gücüyle kurtulan yiğit.
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 Zafer için at boş bir umuttur, Büyük gücüne karşın kimseyi kurtaramaz.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Ama RAB'bin gözü kendisinden korkanların, Sevgisine umut bağlayanların üzerindedir;
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 Böylece onları ölümden kurtarır, Kıtlıkta yaşamalarını sağlar.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 Umudumuz RAB'dedir, Yardımcımız, kalkanımız O'dur.
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 O'nda sevinç bulur yüreğimiz, Çünkü O'nun kutsal adına güveniriz.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Madem umudumuz sende, Sevgin üzerimizde olsun, ya RAB!
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.

< Mezmurlar 33 >