< Mezmurlar 140 >

1 Müzik şefi için - Davut'un mezmuru Ya RAB, kurtar beni kötü insandan, Koru beni zorbadan.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 Onlar yüreklerinde kötülük tasarlar, Savaşı sürekli körükler,
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 Yılan gibi dillerini bilerler, Engerek zehiri var dudaklarının altında. (Sela)
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Ya RAB, sakın beni kötünün elinden, Koru beni zorbadan; Bana çelme takmayı tasarlıyorlar.
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 Küstahlar benim için tuzak kurdu, Haydutlar ağ gerdi; Yol kenarına kapan koydular benim için. (Sela)
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 Sana diyorum, ya RAB: “Tanrım sensin.” Yalvarışıma kulak ver, ya RAB.
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 Ey Egemen RAB, güçlü kurtarıcım, Savaş gününde başımı korudun.
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 Kötülerin dileklerini yerine getirme, ya RAB, Tasarılarını ileri götürme! Yoksa gurura kapılırlar. (Sela)
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 Beni kuşatanların başını, Dudaklarından dökülen fesat kaplasın.
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Kızgın korlar yağsın üzerlerine! Ateşe, dipsiz çukurlara atılsınlar, Bir daha kalkamasınlar.
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 İftiracılara ülkede hayat kalmasın, Felaket zorbaları amansızca avlasın.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 Biliyorum, RAB mazlumun davasını savunur, Yoksulları haklı çıkarır.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Kuşkusuz doğrular senin adına şükredecek, Dürüstler senin huzurunda oturacak.
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.

< Mezmurlar 140 >