< Mezmurlar 138 >

1 Davut'un mezmuru Bütün yüreğimle sana şükrederim, ya RAB, İlahlar önünde seni ilahilerle överim.
Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 Kutsal tapınağına doğru eğilir, Adına şükrederim, Sevgin, sadakatin için. Çünkü adını ve sözünü her şeyden üstün tuttun.
Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
3 Seslendiğim gün bana yanıt verdin, İçime güç koydun, beni yüreklendirdin.
Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4 Şükretsin sana, ya RAB, yeryüzü krallarının tümü, Çünkü ağzından çıkan sözleri işittiler.
Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 Yaptığın işleri ezgilerle övsünler, ya RAB, Çünkü çok yücesin.
Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6 RAB yüksekse de, Alçakgönüllüleri gözetir, Küstahları uzaktan tanır.
Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
7 Sıkıntıya düşersem, canımı korur, Düşmanlarımın öfkesine karşı el kaldırırsın, Sağ elin beni kurtarır.
Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 Ya RAB, her şeyi yaparsın benim için. Sevgin sonsuzdur, ya RAB, Elinin eserini bırakma!
Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.

< Mezmurlar 138 >