< Mezmurlar 135 >

1 RAB'be övgüler sunun! RAB'bin adına övgüler sunun, Ey RAB'bin kulları! Ey sizler, RAB'bin Tapınağı'nda, Tanrımız'ın Tapınağı'nın avlularında hizmet edenler, Övgüler sunun!
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 RAB'be övgüler sunun, Çünkü RAB iyidir. Adını ilahilerle övün, Çünkü hoştur bu.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 RAB kendine Yakup soyunu, Öz halkı olarak İsrail'i seçti.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Biliyorum, RAB büyüktür, Rabbimiz bütün ilahlardan üstündür.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 RAB ne isterse yapar, Göklerde, yeryüzünde, Denizlerde, bütün derinliklerde.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Yeryüzünün dört bucağından bulutlar yükseltir, Yağmur için şimşek çaktırır, Ambarlarından rüzgar estirir.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 İnsanlardan hayvanlara dek Mısır'da ilk doğanları öldürdü.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Ey Mısır, senin orta yerinde, Firavunla bütün görevlilerine Belirtiler, şaşılası işler gösterdi.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Birçok ulusu bozguna uğrattı, Güçlü kralları öldürdü:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Amorlu kral Sihon'u, Başan Kralı Og'u, Bütün Kenan krallarını.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 Topraklarını mülk, Evet, mülk olarak halkı İsrail'e verdi.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Ya RAB, adın sonsuza dek sürecek, Bütün kuşaklar seni anacak.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 RAB halkını haklı çıkarır, Kullarına acır.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Ulusların putları altın ve gümüşten yapılmış, İnsan elinin eseridir.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Ağızları var, konuşmazlar, Gözleri var, görmezler,
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Kulakları var, duymazlar, Soluk alıp vermezler.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Onları yapan, onlara güvenen herkes Onlar gibi olacak!
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Ey İsrail halkı, RAB'be övgüler sun! Ey Harun soyu, RAB'be övgüler sun!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Ey Levi soyu, RAB'be övgüler sun! RAB'be övgüler sunun, ey RAB'den korkanlar!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Yeruşalim'de oturan RAB'be Siyon'dan övgüler sunulsun! RAB'be övgüler sunun!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Mezmurlar 135 >