< Süleyman'In Özdeyişleri 27 >

1 Yarınla övünme, Çünkü ne getireceğini bilemezsin.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Seni kendi ağzın değil, başkaları övsün, Kendi dudakların değil, yabancı övsün.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 Taş ağırdır, kum bir yüktür, Ama ahmağın kışkırtması ikisinden de ağırdır.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Öfke zalim, hiddet azgındır, Ama kıskançlığa kim dayanabilir?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Açık bir azar, Gizli tutulan sevgiden iyidir.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Düşmanın öpücükleri aldatıcıdır, Ama dostun seni iyiliğin için yaralar.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 Tok insanın canı balı bile çekmez, Aç kişiye en acı şey tatlı gelir.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Yuvasından uzak kalan kuş nasılsa, Yurdundan uzak kalan insan da öyledir.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 Güzel koku ve buhur canı ferahlatır, Dostun verdiği öğüt insana tatlı gelir.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Kendi dostunu da babanın dostunu da bırakma Ve felakete uğradığın gün kardeşinin evine gitme; Yakın komşun uzaktaki kardeşten yeğdir.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Oğlum, bilgece davran ki yüreğim sevinsin, Beni ayıplayana yanıt vereyim.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 İhtiyatlı kişi tehlikeyi görünce saklanır, Bönse öne atılır ve zarar görür.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Tanımadığı birine kefil olanın giysisini al; Bir yabancı için yapıyorsa bunu, Giysisini rehin tut.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 Sabah sabah komşuya verilen gürültülü bir selam Küfür sayılır.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Kavgacı kadının dırdırı Yağmurlu günde damlaların dinmeyen sesi gibidir.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 Böyle bir kadını dizginlemeye kalkmak, Rüzgarı ya da yağı avuçta tutmaya çalışmak gibidir.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Demir demiri biler, İnsan da insanı...
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 İncir ağacını budayan meyvesini yer, Efendisine hizmet eden onurlandırılır.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Su görüntümüzü nasıl yansıtıyorsa, Yürek de insanın içini yansıtır.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Ölüm ve yıkım diyarı insana doymaz, İnsanın gözü de hiç doymaz. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 Altın ocakta, gümüş potada sınanır, İnsansa aldığı övgüyle sınanır.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Ahmağı buğdayla birlikte dibekte tokmakla dövsen bile, Ahmaklığından kurtulmaz.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Davarına iyi bak, Sığırlarına dikkat et.
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Çünkü zenginlik kalıcı değildir Ve taç kuşaktan kuşağa geçmez.
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Çayır biçilince, yeni çimen çıkınca, Dağlardaki otlar toplanınca,
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 Kuzular seni giydirir, Tekeler tarlanın bedeli olur.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 Keçilerin sütü yalnız seni değil, Ev halkını, hizmetçilerini de doyurmaya yeter.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Süleyman'In Özdeyişleri 27 >