< Matta 9 >

1 İsa tekneye binip karşı kıyıya geçti ve kendi kentine gitti.
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2 Kendisine, yatak üzerinde felçli bir adam getirdiler. İsa onların imanını görünce felçliye, “Cesur ol, oğlum, günahların bağışlandı” dedi.
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3 Bunun üzerine bazı din bilginleri içlerinden, “Bu adam Tanrı'ya küfrediyor!” dediler.
Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
4 Onların ne düşündüklerini bilen İsa dedi ki, “Yüreğinizde neden kötü düşüncelere yer veriyorsunuz?
Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, “Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5 Hangisi daha kolay? ‘Günahların bağışlandı’ demek mi, yoksa ‘Kalk, yürü’ demek mi?
Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6 Ne var ki, İnsanoğlu'nun yeryüzünde günahları bağışlama yetkisine sahip olduğunu bilesiniz diye...” Sonra felçliye, “Kalk, yatağını topla, evine git!” dedi.
Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako.”
7 Adam da kalkıp evine gitti.
Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8 Halk bunu görünce korkuya kapıldı. İnsana böyle bir yetki veren Tanrı'yı yücelttiler.
Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9 İsa oradan geçerken, vergi toplama yerinde oturan birini gördü. Matta adındaki bu adama, “Ardımdan gel” dedi. Adam da kalkıp İsa'nın ardından gitti.
Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, “Nifuate.” Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10 Sonra İsa, Matta'nın evinde sofrada otururken, birçok vergi görevlisiyle günahkâr gelip O'nunla ve öğrencileriyle birlikte sofraya oturdu.
Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11 Bunu gören Ferisiler, İsa'nın öğrencilerine, “Sizin öğretmeniniz neden vergi görevlileri ve günahkârlarla birlikte yemek yiyor?” diye sordular.
Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, “Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
12 İsa bunu duyunca şöyle dedi: “Sağlamların değil, hastaların hekime ihtiyacı var.
Yesu aliwasikia, akasema, “Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13 Gidin de, ‘Ben kurban değil, merhamet isterim’ sözünün anlamını öğrenin. Çünkü ben doğru kişileri değil, günahkârları çağırmaya geldim.”
Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi.”
14 Bu arada Yahya'nın öğrencileri gelip İsa'ya, “Neden biz ve Ferisiler oruç tutuyoruz da senin öğrencilerin tutmuyor?” diye sordular.
Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, “Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?”
15 İsa şöyle karşılık verdi: “Güvey aralarındayken, davetliler yas tutar mı? Ama güveyin aralarından alınacağı günler gelecek, o zaman oruç tutacaklar.
Yesu akawajibu, “Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16 Hiç kimse eski giysiyi yeni kumaş parçasıyla yamamaz. Çünkü yeni kumaş çeker, giysiden kopar, yırtık daha beter olur.
“Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17 Hiç kimse yeni şarabı eski tulumlara doldurmaz. Yoksa tulumlar patlar; hem şarap dökülür, hem de tulumlar mahvolur. Yeni şarap yeni tulumlara konur, böylece her ikisi de korunmuş olur.”
Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama.”
18 İsa onlara bu sözleri söylerken bir havra yöneticisi gelip O'nun önünde yere kapanarak, “Kızım az önce öldü. Ama sen gelip elini onun üzerine koyarsan, dirilecek” dedi.
Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, “Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi.”
19 İsa kalkıp öğrencileriyle birlikte adamın ardından gitti.
Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20 Tam o sırada, on iki yıldır kanaması olan bir kadın İsa'nın arkasından yetişip giysisinin eteğine dokundu.
Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21 İçinden, “Giysisine bir dokunsam kurtulurum” diyordu.
Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
22 İsa arkasına dönüp onu görünce, “Cesur ol, kızım! İmanın seni kurtardı” dedi. Ve kadın o anda iyileşti.
Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, “Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya.” Mama huyo akapona saa ileile.
23 İsa, yöneticinin evine varıp kaval çalanlarla gürültülü kalabalığı görünce, “Çekilin!” dedi. “Kız ölmedi, uyuyor.” Onlar ise kendisiyle alay ettiler.
Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
akasema, “Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu.” Nao wakamcheka.
25 Kalabalık dışarı çıkarılınca İsa içeri girip kızın elini tuttu, kız ayağa kalktı.
Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26 Bu haber bütün bölgeye yayıldı.
Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27 İsa oradan ayrılırken iki kör, “Ey Davut Oğlu, halimize acı!” diye feryat ederek O'nun ardından gittiler.
Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, “Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
28 İsa eve girince körler yanına geldi. Onlara, “İstediğinizi yapabileceğime inanıyor musunuz?” diye sordu. Körler, “İnanıyoruz, ya Rab!” dediler.
Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, “Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?” Nao wakamjibu, “Naam, Mheshimiwa.”
29 Bunun üzerine İsa körlerin gözlerine dokunarak, “İmanınıza göre olsun” dedi.
Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, “Na iwe kwenu kama mnavyoamini.”
30 Ve adamların gözleri açıldı. İsa, “Sakın kimse bunu bilmesin” diyerek onları sıkı sıkı uyardı.
Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: “Msimwambie mtu yeyote jambo hili.”
31 Onlar ise çıkıp İsa'yla ilgili haberi bütün bölgeye yaydılar.
Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32 Adamlar çıkarken İsa'ya dilsiz bir cinli getirdiler.
Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33 Cin kovulunca adamın dili çözüldü. Halk hayret içinde, “İsrail'de böylesi hiç görülmemiştir” diyordu.
Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, “Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!”
34 Ferisiler ise, “Cinleri, cinlerin önderinin gücüyle kovuyor” diyorlardı.
Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, “Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya.”
35 İsa bütün kent ve köyleri dolaşarak havralarda öğretiyor, göksel egemenliğin Müjdesi'ni duyuruyor, her hastalığı, her illeti iyileştiriyordu.
Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36 Kalabalıkları görünce onlara acıdı. Çünkü çobansız koyunlar gibi şaşkın ve perişandılar.
Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37 O zaman İsa öğrencilerine, “Ürün bol, ama işçi az” dedi,
Hapo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38 “Bu nedenle ürünün sahibi Rab'be yalvarın, ürününü kaldıracak işçiler göndersin.”
Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.”

< Matta 9 >