< Matta 20 >

1 “Göklerin Egemenliği, sabah erkenden bağında çalışacak işçi aramaya çıkan toprak sahibine benzer.
“Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2 Adam, işçilerle günlüğü bir dinara anlaşıp onları bağına gönderdi.
Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3 “Saat dokuza doğru tekrar dışarı çıktı, çarşı meydanında boş duran başka adamlar gördü.
Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4 Onlara, ‘Siz de bağa gidip çalışın. Hakkınız neyse, veririm’ dedi, onlar da bağa gittiler. “Öğleyin ve saat üçe doğru yine çıkıp aynı şeyi yaptı.
Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5
Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6 Saat beşe doğru çıkınca, orada duran başka işçiler gördü. Onlara, ‘Neden bütün gün burada boş duruyorsunuz?’ diye sordu.
Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7 “‘Kimse bize iş vermedi ki’ dediler. “Onlara, ‘Siz de bağa gidin, çalışın’ dedi.
Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8 “Akşam olunca, bağın sahibi kâhyasına, ‘İşçileri çağır’ dedi. ‘Sonuncudan başlayarak ilkine kadar, hepsine ücretlerini ver.’
“Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9 “Saat beşe doğru işe başlayanlar gelip kâhyadan birer dinar aldılar.
Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10 İlk başlayanlar gelince daha çok alacaklarını sandılar, ama onlara da birer dinar verildi.
Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11 Paralarını alınca bağ sahibine söylenmeye başladılar:
Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12 ‘En son çalışanlar yalnız bir saat çalıştı’ dediler. ‘Ama onları günün yükünü ve sıcağını çeken bizlerle bir tuttun!’
Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13 “Bağ sahibi onlardan birine şöyle karşılık verdi: ‘Arkadaş, sana haksızlık etmiyorum ki! Seninle bir dinara anlaşmadık mı?
“Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14 Hakkını al, git! Sana verdiğimi sonuncuya da vermek istiyorum.
Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15 Kendi paramla istediğimi yapmaya hakkım yok mu? Yoksa cömertliğimi kıskanıyor musun?’
Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?”
16 “İşte böylece sonuncular birinci, birinciler de sonuncu olacak.”
Yesu akamaliza kwa kusema, “Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
17 İsa Yeruşalim'e giderken, yolda on iki öğrencisini bir yana çekip onlara özel olarak şunu söyledi: “Şimdi Yeruşalim'e gidiyoruz. İnsanoğlu, başkâhinlerin ve din bilginlerinin eline teslim edilecek, onlar da O'nu ölüm cezasına çarptıracaklar.
Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
“Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19 O'nunla alay etmeleri, kamçılayıp çarmıha germeleri için O'nu öteki uluslara teslim edecekler. Ne var ki O, üçüncü gün dirilecek.”
Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa.”
20 O sırada Zebedi oğullarının annesi oğullarıyla birlikte İsa'ya yaklaştı. Önünde yere kapanarak kendisinden bir dileği olduğunu söyledi.
Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21 İsa kadına, “Ne istiyorsun?” diye sordu. Kadın, “Buyruk ver, senin egemenliğinde bu iki oğlumdan biri sağında, biri solunda otursun” dedi.
Yesu akamwuliza, “Unataka nini?” Huyo mama akamwambia, “Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto.”
22 “Siz ne dilediğinizi bilmiyorsunuz” diye karşılık verdi İsa. “Benim içeceğim kâseden siz içebilir misiniz?” “Evet, içebiliriz” dediler.
Yesu akajibu, “Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?” Wakamjibu, “Tunaweza.”
23 İsa onlara, “Elbette benim kâsemden içeceksiniz” dedi, “Ama sağımda ya da solumda oturmanıza izin vermek benim elimde değil. Babam bu yerleri belirli kişiler için hazırlamıştır.”
Yesu akawaambia, “Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu.”
24 Bunu işiten on öğrenci iki kardeşe kızdılar.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25 Ama İsa onları yanına çağırıp şöyle dedi: “Bilirsiniz ki, ulusların önderleri onlara egemen kesilir, ileri gelenleri de ağırlıklarını hissettirirler.
Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26 Sizin aranızda böyle olmayacak. Aranızda büyük olmak isteyen, ötekilerin hizmetkârı olsun.
Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27 Aranızda birinci olmak isteyen, ötekilerin kulu olsun.
na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28 Nitekim İnsanoğlu, hizmet edilmeye değil, hizmet etmeye ve canını birçokları için fidye olarak vermeye geldi.”
Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
29 Eriha'dan ayrılırlarken büyük bir kalabalık İsa'nın ardından gitti.
Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30 Yol kenarında oturan iki kör, İsa'nın oradan geçmekte olduğunu duyunca, “Ya Rab, ey Davut Oğlu, halimize acı!” diye bağırdılar.
Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
31 Kalabalık onları azarlayarak susturmak istediyse de onlar, “Ya Rab, ey Davut Oğlu, halimize acı!” diyerek daha çok bağırdılar.
Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: “Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!”
32 İsa durup onları çağırdı. “Sizin için ne yapmamı istiyorsunuz?” diye sordu.
Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
33 Onlar da, “Ya Rab, gözlerimiz açılsın” dediler.
Wakamjibu, “Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe.”
34 İsa onlara acıdı, gözlerine dokundu. O anda yeniden görmeye başladılar ve O'nun ardından gittiler.
Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.

< Matta 20 >