< Malaki 3 >

1 “İşte habercimi gönderiyorum. Önümde yolu hazırlayacak. Aradığınız Rab ansızın tapınağına gelecek; görmeyi özlediğiniz antlaşma habercisi gelecek” diyor Her Şeye Egemen RAB.
“Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
2 Ama onun geleceği güne kim dayanabilir? O belirince kim durabilir? Çünkü o maden arıtıcının ateşi, çamaşırcının kül suyu gibi olacak;
Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo.
3 gümüş eritip arıtan gibi davranacak: Levililer'i arındırıp altın, gümüş temizler gibi temizleyecek. Böylece RAB'be doğrulukla sunular sunacaklar.
Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki,
4 Geçmiş günlerde, geçmiş yıllarda olduğu gibi, RAB Yahuda ve Yeruşalim'in sunacağı sunulardan hoşnut kalacak.
nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.
5 Her Şeye Egemen RAB, “Yargılamak için size yaklaşacağım” diyor, “Büyücülere, zina edenlere, yalan yere ant içenlere, işçinin, dulun, öksüzün, yabancının hakkını çiğneyenlere –benden korkmayanlara– karşı hemen tanık olacağım.”
“Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
6 “Ben RAB'bim, değişmem. Siz bunun için yok olmadınız, ey Yakup soyu!
“Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa.
7 Atalarınızın günlerinden bu yana kurallarımı çiğnediniz, onlara uymadınız. Bana dönün, ben de size dönerim” diyor Her Şeye Egemen RAB. “Oysa siz, ‘Nasıl döneriz?’ diye soruyorsunuz.
Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
8 “İnsan Tanrı'dan çalar mı? Oysa siz benden çalıyorsunuz. “‘Senden nasıl çalıyoruz?’ diye soruyorsunuz. “Ondalıkları, sunuları çalıyorsunuz.
“Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi. “Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’ “Mnaniibia zaka na dhabihu.
9 Siz lanete uğradınız. Çünkü bütün ulus benden çalıyorsunuz.
Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi.
10 Tapınağımda yiyecek bulunması için bütün ondalıklarınızı ambara getirin. Beni bununla sınayın” diyor Her Şeye Egemen RAB. “Göreceksiniz ki, göklerin kapaklarını size açacağım, üzerinize dolup taşan bereket yağdıracağım.
Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha.
11 Çekirgelerin ekinlerinizi yemesini engelleyeceğim. Tarlada asmanız ürünsüz kalmayacak” diyor Her Şeye Egemen RAB.
Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
12 “Bütün uluslar ne mutlu size diyecekler. Çünkü ülkeniz özlenen bir yer olacak.” Böyle diyor Her Şeye Egemen RAB.
“Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
13 “Bana karşı sert sözler söylediniz” diyor RAB. “Oysa siz, ‘Sana karşı ne söyledik?’ diye soruyorsunuz.
“Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana. “Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’
14 “Şunu dediniz: ‘Tanrı'ya kulluk etmek yararsızdır. Her Şeye Egemen RAB'bin isteklerini yerine getirmek, O'nun önünde yas tutar gibi davranmak bize ne kazanç sağlıyor?
“Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote?
15 Şimdi kendini beğenmişlere mutlu diyoruz. Kötülük edenler başarılı oluyor, Tanrı'yı deneyenler cezadan kurtuluyor.’”
Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’”
16 Bunun üzerine RAB'den korkanlar birbirleriyle konuştular. RAB dediklerine kulak verip duydu. RAB'den korkup adını sayanlar için O'nun önünde bir anma kitabı yazıldı.
Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.
17 Her Şeye Egemen RAB, “Öz halkımı ortaya çıkardığım gün, benim olacaklar” diyor, “Bir baba kendisine hizmet eden oğlunu nasıl esirgerse ben de onları öyle esirgeyeceğim.
“Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia.
18 O zaman siz doğru kişiyle kötü kişi, Tanrı'ya kulluk edenle etmeyen arasındaki ayrımı yine göreceksiniz.”
Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.

< Malaki 3 >