< Eyüp 37 >

1 “Yüreğim titrer buna, Yerinden oynar.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Dinleyin, gürleyen sesini dinleyin, Ağzından çıkan sesi!
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Şimşeğini göğün altındaki her yere, Yeryüzünün dört bucağına salar.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Ardından bir ses gümbürder, Görkemli sesiyle gürler. Sesi duyulunca şimşekleri alıkoymaz.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Tanrı'nın sesi şaşılacak biçimde gürler, O, anlayışımızın ötesinde büyük işler yapar.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Çünkü kara, ‘Yere düş’ der, Sağanağa, ‘Bütün şiddetinle boşal.’
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Yarattığı bütün insanlar ne yaptığını bilsin diye, Herkese işini bıraktırır.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Hayvanlar kovuklarına girer, İnlerinde otururlar.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Kasırga yuvasından kopar, Soğuk saçılan rüzgarlardan.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Tanrı'nın soluğu suları dondurur, Geniş sular buz tutar.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Bulutlara nem yükler, Şimşeğini her yana yayar.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Yeryüzünde ne buyurursa yapmak üzere Bulutlar O'nun istediği yönde döner durur.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Ya insanları cezalandırmak Ya da yeryüzünü sulayıp sevgisini göstermek için Yağmur gönderir.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 “Dinle, Eyüp, Dur da düşün Tanrı'nın şaşılası işlerini.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Tanrı'nın bulutları nasıl düzenlediğini, Şimşeğini nasıl çaktırdığını biliyor musun?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Bulutların dengesini, Bilgisi kusursuz olanın şaşılası işlerini biliyor musun?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Dünyanın soluğu kesildiğinde Güneyin kavurucu rüzgarı altında Giysilerin seni terletmez mi?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Dökme tunç bir ayna kadar sert olan gökkubbeyi O'nunla birlikte yayabilir misin?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 “O'na ne söyleyeceğimizi öğret bize, Çünkü karanlık yüzünden sözümüze düzen veremiyoruz.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Konuşmak istediğim O'na söylenebilir mi? Kimse yutulmak ister mi?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Rüzgar geçip göğü temizlediğinde Gökte parıldayan ışığa kimse bakamaz.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Altın parıltısı geliyor kuzeyden, Tanrı korkunç görkeme bürünmüş.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Her Şeye Gücü Yeten'e biz ulaşamayız. Gücü yücedir, Adaleti ve eşsiz doğruluğuyla kimseyi ezmez.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Bu yüzden insanlar O'na saygı duyar, Çünkü O, bilgeleri dikkate almaz.”
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Eyüp 37 >