< Eyüp 31 >

1 “Gözlerimle antlaşma yaptım Şehvetle bir kıza bakmamak için.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Çünkü insanın yukarıdan, Tanrı'dan payı nedir, Yücelerden, Her Şeye Gücü Yeten'den mirası ne?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Kötüler için felaket, Haksızlık yapanlar için bela değil mi?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Yürüdüğüm yolları görmüyor mu, Attığım her adımı saymıyor mu?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 “Eğer yalan yolunda yürüdümse, Ayağım hileye seğirttiyse,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 –Tanrı beni doğru teraziyle tartsın, Kusursuz olduğumu görsün–
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Adımım yoldan saptıysa, Yüreğim gözümü izlediyse, Ellerim pisliğe bulaştıysa,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Ektiğimi başkaları yesin, Ekinlerim kökünden sökülsün.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 “Eğer gönlümü bir kadına kaptırdıysam, Komşumun kapısında pusuya yattıysam,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Karım başkasının buğdayını öğütsün, Onunla başka erkekler yatsın.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 Çünkü bu utanç verici, Yargılanması gereken bir suç olurdu.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Yıkım diyarına dek yakan bir ateştir o, Bütün ürünümü kökünden kavururdu.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 “Benimle ters düştüklerinde Kölemin ve hizmetçimin hakkını yemişsem,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 Tanrı yargıladığında ne yaparım? Hesap sorduğunda ne yanıt veririm?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Beni ana karnında yaratan onu da yaratmadı mı? Rahimde bize biçim veren O değil mi?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 “Eğer yoksulların dileğini geri çevirdimse, Dul kadının umudunu kırdımsa,
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Ekmeğimi yalnız yedim, Öksüzle paylaşmadımsa,
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 Gençliğimden beri öksüzü baba gibi büyütmedimse, Doğduğumdan beri dul kadına yol göstermedimse,
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Giysisi olmadığı için can çekişen birini Ya da örtüsü olmayan bir yoksulu gördüm de,
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 Koyunlarımın yünüyle ısıtmadıysam, O da içinden beni kutsamadıysa,
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 Mahkemede sözümün geçtiğini bilerek Öksüze el kaldırdımsa,
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Kolum omuzumdan düşsün, Kol kemiğim kırılsın.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 Çünkü Tanrı'dan gelecek beladan korkarım, O'nun görkeminden ötürü böyle bir şey yapamam.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 “Eğer umudumu altına bağladımsa, Saf altına, ‘Güvencim sensin’ dedimse,
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Servetim çok, Varlığımı bileğimle kazandım diye sevindimse,
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 Işıldayan güneşe, Parıldayarak hareket eden aya bakıp da,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 İçimden ayartıldımsa, Elim onlara taptığımı gösteren bir öpücük yolladıysa,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Bu da yargılanacak bir suç olurdu, Çünkü yücelerdeki Tanrı'yı yadsımış olurdum.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 “Eğer düşmanımın yıkımına sevindim, Başına kötülük geldi diye keyiflendimse,
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 –Kimsenin canına lanet ederek Ağzımın günah işlemesine izin vermedim–
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Evimdeki insanlar, ‘Eyüp'ün verdiği etle Karnını doyurmayan var mı?’ diye sormadıysa,
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 –Hiçbir yabancı geceyi sokakta geçirmezdi, Çünkü kapım her zaman yolculara açıktı–
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Kalabalıktan çok korktuğum, Boyların aşağılamasından yıldığım, Susup dışarı çıkmadığım için Suçumu bağrımda gizleyip Adem gibi isyanımı örttümse,
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 –“Keşke beni dinleyen biri olsa! İşte savunmamı imzalıyorum, Her Şeye Gücü Yeten bana yanıt versin! Hasmımın yazdığı tomar elimde olsa,
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Kuşkusuz onu omuzumda taşır, Taç gibi başıma koyardım.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 Attığım her adımı ona bildirir, Kendisine bir önder gibi yaklaşırdım.–
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 “Toprağım bana feryat ediyorsa, Sabanın açtığı yarıklar bir ağızdan ağlıyorsa,
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 Ürününü para ödemeden yedimse Ya da üzerinde oturanların kalbini kırdımsa,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Orada buğday yerine diken, Arpa yerine delice bitsin.” Eyüp'ün konuşması sona erdi.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Eyüp 31 >