< Yeremya 38 >

1 Mattan oğlu Şefatya, Paşhur oğlu Gedalya, Şelemya oğlu Yehukal ve Malkiya oğlu Paşhur Yeremya'nın halka söylediği şu sözleri duydular:
Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
2 “RAB diyor ki, ‘Bu kentte kalan kılıçtan, kıtlıktan, salgından ölecek. Kildaniler'e gidense sağ kalacak, canını kurtarıp yaşayacak.’
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
3 RAB diyor ki, ‘Bu kent kesinlikle Babil Kralı'nın ordusuna teslim edilecek, Babil Kralı onu ele geçirecek.’”
Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
4 Önderler krala, “Bu adam öldürülmeli” dediler, “Çünkü söylediği bu sözlerle kentte kalan askerlerin ve halkın cesaretini kırıyor. Bu adam halkın yararını değil, zararını istiyor.”
Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
5 Kral Sidkiya, “İşte o sizin elinizde” diye yanıtladı, “Kral size engel olamaz ki.”
Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
6 Böylece Yeremya'yı alıp kralın oğlu Malkiya'nın muhafız avlusundaki sarnıcına halatlarla sarkıtarak indirdiler. Sarnıçta su yoktu, yalnız çamur vardı. Yeremya çamura battı.
Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
7 Sarayda görevli hadım Kûşlu Ebet-Melek Yeremya'nın sarnıca atıldığını duydu. Kral Benyamin Kapısı'nda otururken,
Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
8 Ebet-Melek saraydan çıkıp kralın yanına gitti ve ona şöyle dedi:
Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
9 “Efendim kral, bu adamların Peygamber Yeremya'ya yaptıkları kötüdür. Onu sarnıca attılar, orada açlıktan ölecek. Çünkü kentte ekmek kalmadı.”
“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
10 Bunun üzerine kral, “Buradan yanına üç adam al, Peygamber Yeremya'yı ölmeden sarnıçtan çıkarın” diye ona buyruk verdi.
Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
11 Ebet-Melek yanına adamları alarak saray hazinesinin alt odasına gitti. Oradan eski bezler, yırtık pırtık giysiler alıp halatlarla sarnıca, Yeremya'ya sarkıttı.
Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
12 Sonra Yeremya'ya, “Bu eski bezleri, yırtık giysileri halatlarla bağlayıp koltuklarının altına geçir” diye seslendi. Yeremya söyleneni yaptı.
Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
13 Onu halatlarla çekip sarnıçtan çıkardılar. Yeremya muhafız avlusunda kaldı.
nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
14 Kral Sidkiya Peygamber Yeremya'yı RAB'bin Tapınağı'nın üçüncü girişine getirterek, “Sana bir şey soracağım” dedi, “Benden bir şey gizleme.”
Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
15 Yeremya, “Sana bir şey bildirirsem, beni öldürmeyecek misin?” diye karşılık verdi, “Üstelik öğüt versem bile beni dinlemeyeceksin.”
Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
16 Kral Sidkiya, “Bize yaşam veren RAB'bin varlığı hakkı için seni öldürmeyeceğim, canının peşinde olan bu adamların eline seni teslim etmeyeceğim” diyerek gizlice ant içti.
Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
17 Bunun üzerine Yeremya Sidkiya'ya şu karşılığı verdi: “İsrail'in Tanrısı, Her Şeye Egemen RAB Tanrı diyor ki, ‘Babil Kralı'nın komutanlarına teslim olursan, canın bağışlanacak, bu kent de ateşe verilmeyecek. Sen de ailen de sağ kalacaksınız.
Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
18 Ama Babil Kralı'nın komutanlarına teslim olmazsan, kent Kildaniler'e teslim edilecek, onu ateşe verecekler. Sen de onlardan kaçıp kurtulamayacaksın.’”
Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
19 Kral Sidkiya, “Kildaniler'in tarafına geçen Yahudiler'den korkuyorum” dedi, “Kildaniler beni onların eline verebilir, onlar da bana kötü davranırlar.”
Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
20 “Vermezler” diye yanıtladı Yeremya, “Lütfen sana aktardığım RAB'bin sözünü işit. O zaman sağ kalır, iyilik görürsün.
Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
21 Ama teslim olmak istemezsen, RAB bana şunu açıkladı:
Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
22 Yahuda Kralı'nın sarayında kalan bütün kadınlar Babil Kralı'nın komutanlarına çıkarılacak. O kadınlar sana, “‘Güvendiğin insanlar Seni aldatıp yenilgiye uğrattı; Çamura battı ayakların, Güvendiğin insanlar seni bırakıp gitti’ diyecekler.
Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
23 “Bütün karıların, çocukların Kildaniler'e teslim edilecek. Sen de onlardan kaçıp kurtulamayacak, Babil Kralı'nın eliyle yakalanacaksın. Bu kent ateşe verilecek.”
“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
24 Sidkiya, “Ölmek istemiyorsan, konuştuklarımızı kimse duymasın” dedi,
Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
25 “Görevliler seninle konuştuğumu duyup da gelir, ‘Krala ne söyledin, kral sana ne dedi, açıkla bize, bizden gizleme! Yoksa seni öldürürüz’ derlerse,
Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
26 ‘Beni Yonatan'ın evine geri gönderme, yoksa orada ölürüm diye krala yalvardım’ dersin.”
basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
27 Bütün görevliler gelip Yeremya'yı sorguya çektiler. Yeremya kralın kendisine söylemesini buyurduğu her şeyi onlara anlattı. Sorguyu bıraktılar. Çünkü kralla yaptığı konuşma duyulmamıştı.
Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
28 Yeremya Yeruşalim'in ele geçirildiği güne dek muhafız avlusunda kaldı.
Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.

< Yeremya 38 >