< Yeremya 23 >

1 “Otlağımın koyunlarını yok edip dağıtan çobanların vay başına!” diyor RAB.
“Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
2 Halkımı güden çobanlar için İsrail'in Tanrısı RAB şöyle diyor: “Sürümü dağıtıp sürdünüz, onlarla ilgilenmediniz. Şimdi ben sizinle ilgileneceğim, yaptığınız kötülük yüzünden sizi cezalandıracağım.” RAB böyle diyor.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
3 “Sürmüş olduğum bütün ülkelerden sürümün sağ kalanlarını toplayıp otlaklarına geri getireceğim; orada verimli olup çoğalacaklar.
“Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
4 Onları güdecek çobanlar koyacağım başlarına. Bundan böyle korkmayacak, yılgınlığa düşmeyecekler. Bir tanesi bile eksilmeyecek” diyor RAB.
Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
5 “İşte Davut için doğru bir dal Çıkaracağım günler geliyor” diyor RAB. “Bu kral bilgece egemenlik sürecek, Ülkede adil ve doğru olanı yapacak.
Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
6 Onun döneminde Yahuda kurtulacak, İsrail güvenlik içinde yaşayacak. O, ‘Yahve sidkenu’ adıyla anılacak.
Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
7 “Artık insanların, ‘İsrail halkını Mısır'dan çıkaran RAB'bin varlığı hakkı için’ demeyecekleri günler geliyor” diyor RAB.
“Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
8 “Bunun yerine, ‘İsrail soyunu kuzey ülkesinden ve sürdüğü bütün öbür ülkelerden geri getiren RAB'bin varlığı hakkı için’ diyecekler. Böylece kendi topraklarında yaşayacaklar.”
bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
9 Peygamberlere gelince, Yüreğim paramparça, Bütün kemiklerim titriyor. RAB'bin yüzünden, O'nun kutsal sözleri yüzünden Sarhoş gibi, Şaraba yenik düşen bir adam gibiyim.
Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
10 Çünkü ülke zina edenlerle dolu, Lanet yüzünden yas tutuyor. Otlaklar kurumuş. İzledikleri yol kötü, Güçlerini haksızca kullanıyorlar.
Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
11 “Peygamber de kâhin de tanrısız; Tapınağımda bile kötülüklerini gördüm” diyor RAB.
“Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
12 “Bu yüzden izledikleri yol Onlar için kaygan olacak; Karanlığa sürülecek, Orada tökezleyip düşecekler. Çünkü cezalandırılacakları yıl Başlarına felaket getireceğim” diyor RAB.
“Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
13 “Samiriye peygamberleri arasında Şu iğrençliği gördüm: Baal adına peygamberlik ederek Halkım İsrail'i baştan çıkarıyorlar.
“Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
14 Yeruşalim peygamberleri arasında Şu korkunç şeyi gördüm: Zina ediyorlar, yalan peşindeler. Kötülük edenleri güçlendirdiklerinden, Kimse kötülüğünden dönmüyor. Benim için hepsi Sodom gibi, Yeruşalim halkı Gomora gibi oldu.”
Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
15 Bu nedenle Her Şeye Egemen RAB peygamberler için şöyle diyor: “Onlara pelinotu yedirecek, Zehirli su içireceğim. Çünkü Yeruşalim peygamberleri Tanrısızlığın bütün ülkeye yayılmasına neden oldular.”
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
16 Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Size peygamberlik eden peygamberlerin Dediklerine kulak asmayın, Onlar sizi aldatıyor. RAB'bin ağzından çıkanları değil, Kendi hayal ettikleri görümleri anlatıyorlar.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
17 Beni küçümseyenlere sürekli, ‘RAB diyor ki: Size esenlik olacak!’ diyorlar. Yüreklerinin inatçılığı doğrultusunda davrananlara, ‘Başınıza felaket gelmeyecek’ diyorlar.
Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
18 RAB'bin sözünü duyup anlamak için RAB'bin meclisinde kim bulundu ki? O'nun sözüne kulak verip duyan kim?
Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
19 İşte, RAB'bin fırtınası öfkeyle kopacak, Kasırgası döne döne kötülerin başına patlayacak.
Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
20 Aklının tasarladığını tümüyle yapana dek RAB'bin öfkesi dinmeyecek. Son günlerde açıkça anlayacaksınız bunu.
Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
21 Bu peygamberleri ben göndermedim, Ama çabucak ortaya çıktılar. Onlara hiç seslenmedim, Yine de peygamberlik ettiler.
Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
22 Ama meclisimde dursalardı, Sözlerimi halkıma bildirir, Onları kötü yollarından ve davranışlarından Döndürürlerdi.
Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
23 Ben yalnızca yakındaki Tanrı mıyım? Uzaktaki Tanrı da değil miyim?” diyor RAB,
“Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
24 “Kim gizli yere saklanır da Onu görmem?” diyor RAB, “Yeri göğü doldurmuyor muyum?” diyor RAB.
Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
25 “Adımla yalancı peygamberlik edenlerin ne dediklerini duydum. ‘Bir düş gördüm! Bir düş!’ diyorlar.
“Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
26 Kafalarından uydurdukları hileleri aktaran bu yalancı peygamberler ne zamana dek sürdürecekler bunu?
Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
27 Ataları nasıl Baal yüzünden adımı unuttuysa, onlar da birbirlerine düşlerini anlatarak halkıma adımı unutturmayı tasarlıyorlar.
Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
28 Düşü olan peygamber düşünü anlatsın; ama sözümü alan onu sadakatle bildirsin. Buğdayın yanında saman nedir ki?” diyor RAB.
Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
29 “Benim sözüm ateş gibi değil mi? Kayaları paramparça eden balyoz gibi değil mi?” RAB böyle diyor.
“Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
30 “İşte bunun için sözlerimi birbirlerinden çalan peygamberlere karşıyım” diyor RAB.
“Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
31 “Evet, kendi sözlerini söyleyip, ‘RAB böyle diyor’ diyen peygamberlere karşıyım” diyor RAB.
“Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
32 “Uydurma düşler gören peygamberlere karşıyım” diyor RAB. “Bu düşleri anlatıyor, yalanlarla, boş övünmelerle halkımı baştan çıkarıyorlar. Ben onları ne gönderdim, ne de atadım. Bu halka hiç mi hiç yararları yok” diyor RAB.
Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
33 “Halktan biri, bir peygamber ya da kâhin, ‘RAB'bin bildirisi nedir?’ diye sorarsa, ‘Ne bildirisi?’ diye karşılık vereceksin. Sizi başımdan atacağım” diyor RAB.
“Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
34 “Eğer bir peygamber, kâhin ya da başka biri, ‘Bu RAB'bin bildirisidir’ derse, onu da ailesini de cezalandıracağım.
Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
35 Her biriniz komşunuza ve kardeşinize, ‘RAB ne yanıt verdi?’ ya da, ‘RAB ne söyledi?’ demelisiniz.
Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
36 Bundan böyle, ‘RAB'bin bildirisi’ lafını ağzınıza almayacaksınız. Herkesin sözü kendi bildirisi olacak. Yaşayan Tanrı'nın, Her Şeye Egemen RAB'bin, Tanrımız'ın sözlerini çarpıtıyorsunuz siz.
Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
37 Bir peygambere, ‘RAB sana ne yanıt verdi?’ ya da, ‘RAB ne söyledi?’ demelisiniz.
Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
38 Ama, ‘RAB'bin bildirisidir’ derseniz, RAB diyor ki, ‘RAB'bin bildirisidir’ diyorsunuz. Oysa, ‘RAB'bin bildirisidir’ demeyeceksiniz diye sizi uyarmıştım.
Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
39 Bu yüzden sizi büsbütün unutacağım, sizi de size ve atalarınıza verdiğim kenti de önümden söküp atacağım.
Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
40 Sizi hiç unutulmayacak bir utanca düşürecek, sürekli alay konusu edeceğim.”
Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

< Yeremya 23 >