< Yeremya 13 >

1 RAB bana, “Git, kendine keten bir kuşak satın alıp beline sar, ama suya sokma” dedi.
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.”
2 RAB'bin buyruğu uyarınca bir kuşak satın alıp belime sardım.
Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.
3 RAB bana ikinci kez seslendi:
Ndipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili:
4 “Satın aldığın belindeki kuşağı al, Perat'a git. Kuşağı orada bir kaya kovuğuna gizle.”
“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.”
5 RAB'bin buyruğu uyarınca gidip kuşağı Perat'a yakın bir yere gizledim.
Ndipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
6 Uzun süre sonra RAB bana, “Kalk, Perat'a git, gizlemeni buyurduğum kuşağı al” dedi.
Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
7 Bunun üzerine Perat'a gittim, gizlediğim yeri kazıp kuşağı aldım. Ancak kuşak çürümüştü, hiçbir işe yaramazdı.
Hivyo nikaenda Frati na kuuchimbua ule mkanda kutoka pale nilipokuwa nimeuficha, lakini sasa ulikuwa umeharibika na haufai tena kabisa.
8 RAB bana şöyle seslendi:
Ndipo neno la Bwana likanijia:
9 “RAB diyor ki, ‘İşte Yahuda'nın gururunu da Yeruşalim'in büyük gururunu da böyle çürüteceğim.
“Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Vivyo hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
10 Sözümü dinlemek istemeyen, yüreklerinin inadı uyarınca davranan, başka ilahları izleyip onlara kulluk eden, tapan bu kötü halk, bu işe yaramaz kuşak gibi olacak.
Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wafuatao ukaidi wa mioyo yao na kufuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu, watakuwa kama mkanda huu ambao haufai kabisa!
11 Kuşak insanın beline nasıl yapışırsa, ben de İsrail ve Yahuda halklarını kendime öyle yapıştırdım’ diyor RAB, ‘Öyle ki, bana ün, övgü, onur getirecek bir halk olsunlar. Ama dinlemediler.’”
Kwa maana kama vile mkanda ufungwavyo kiunoni mwa mtu, ndivyo nilivyojifunga nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda,’ asema Bwana, ‘ili wawe watu wangu kwa ajili ya utukufu wangu, sifa na heshima yangu. Lakini hawajasikiliza.’
12 “Onlara de ki, ‘İsrail'in Tanrısı RAB, Her tulum şarapla dolacak, diyor.’ Eğer sana, ‘Her tulumun şarapla dolacağını bilmiyor muyuz sanki?’ derlerse,
“Waambie: ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo.’ Kama wao wakikuambia, ‘Kwani hatujui kwamba kila kiriba inapasa kijazwe mvinyo?’
13 onlara de ki, ‘Bu ülkede yaşayan herkesi –Davut'un tahtında oturan kralları, kâhinleri, peygamberleri, Yeruşalim'de yaşayanların tümünü– sarhoş olana dek şarapla dolduracağım’ diyor RAB.
Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: nitawajaza ulevi wote waishio katika nchi hii, pamoja na wafalme waketio juu ya kiti cha enzi cha Daudi, makuhani, manabii na wale wote waishio Yerusalemu.
14 ‘Onları –babalarla çocukları– birbirlerine çarpacağım. Acımadan, esirgemeden, sevecenlik göstermeden hepsini yok edeceğim’ diyor RAB.”
Nitawagonganisha kila mmoja na mwenzake, baba na wana wao, asema Bwana. Sitawarehemu wala kuwahurumia ili niache kuwaangamiza.’”
15 Dinleyin, kulak verin, Gururlanmayın, Çünkü RAB konuştu.
Sikieni na mzingatie, msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amenena.
16 Karanlık basmadan, Kararan dağlarda Ayaklarınız tökezlemeden Tanrınız RAB'bi onurlandırın. Siz ışık beklerken, RAB onu kopkoyu, zifiri karanlığa çevirecek.
Mpeni utukufu Bwana Mungu wenu, kabla hajaleta giza, kabla miguu yenu haijajikwaa juu ya vilima vitakavyotiwa giza. Mlitarajia nuru, lakini ataifanya kuwa giza nene na kuibadili kuwa huzuni kubwa.
17 Ama bu uyarıyı dinlemezseniz, Gururunuz yüzünden ağlayacağım gizlice, Gözlerim acı acı gözyaşı dökecek, Gözyaşlarım sel gibi akacak. Çünkü RAB'bin sürüsü sürgüne gönderilecek.
Lakini kama hamtasikiliza, nitalia sirini kwa ajili ya kiburi chenu; macho yangu yatalia kwa uchungu, yakitiririka machozi, kwa sababu kundi la kondoo la Bwana litachukuliwa mateka.
18 Krala ve ana kraliçeye söyle: “Tahtlarınızdan inin, Çünkü görkemli taçlarınız başınızdan düştü.”
Mwambie mfalme na mamaye, “Shukeni kutoka kwenye viti vyenu vya enzi, kwa kuwa taji zenu za utukufu zitaanguka kutoka vichwani mwenu.”
19 Negev'deki kentler kapanacak, Onları açan olmayacak. Sürgüne gönderilecek Yahuda, Tamamı sürgüne gönderilecek.
Miji iliyoko Negebu itafungwa, wala hapatakuwa na mtu wa kuifungua. Watu wa Yuda wote watapelekwa uhamishoni, wakichukuliwa kabisa waende mbali.
20 Gözlerinizi kaldırıp bakın, Kuzeyden gelenleri görün. Nerede sana emanet edilen sürü? Övündüğün kuzular nerede?
Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini. Liko wapi lile kundi ulilokabidhiwa, kondoo wale uliojivunia?
21 Sana dost olması için yetiştirdiğin kişileri RAB başına yönetici atayınca ne diyeceksin? Doğuran kadının çektiği sancı gibi Seni de ağrı tutmayacak mı?
Utasema nini Bwana atakapowaweka juu yako wale ulioungana nao kama marafiki wako maalum? Je, hutapatwa na utungu kama mwanamke aliye katika utungu wa kuzaa?
22 “Neden bütün bunlar başıma geldi?” dersen, Günahlarının çokluğu yüzünden eteklerin açıldı, Tecavüze uğradın.
Nawe kama ukijiuliza, “Kwa nini haya yamenitokea?” Ni kwa sababu ya dhambi zako nyingi ndipo marinda yako yameraruliwa na mwili wako umetendewa vibaya.
23 Kûşlu derisinin rengini, Pars beneklerini değiştirebilir mi? Kötülük etmeye alışmış olan sizler de iyilik edemezsiniz.
Je, Mkushi aweza kubadili ngozi yake au chui kubadili madoadoa yake? Vivyo hivyo nawe huwezi kufanya mema wewe uliyezoea kutenda mabaya.
24 “Çöl rüzgarının savurduğu saman çöpü gibi Dağıtacağım sizleri.
“Nitawatawanya kama makapi yapeperushwayo na upepo wa jangwani.
25 Payın, sana ayırdığım pay bu olacak” diyor RAB. “Çünkü beni unuttun, Sahte ilahlara güvendin.
Hii ndiyo kura yako, fungu nililokuamuria,” asema Bwana, “kwa sababu umenisahau mimi na kuamini miungu ya uongo.
26 Ayıbın ortaya çıksın diye Eteklerini yüzüne dek kaldıracağım.
Nitayafunua marinda yako mpaka juu ya uso wako ili aibu yako ionekane:
27 Kırdaki tepeler üzerinde Yaptığın iğrençlikleri –zinalarını, Çapkın çapkın kişneyişini, yüzsüz fahişeliklerini– gördüm. Vay başına geleceklere, ey Yeruşalim! Ne zamana dek böyle kirli kalacaksın?”
uzinzi wako na kulia kwako kama farasi kulikojaa tamaa, ukahaba wako usio na aibu! Nimeyaona matendo yako ya machukizo juu ya vilima na mashambani. Ole wako, ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa najisi mpaka lini?”

< Yeremya 13 >