< Yeşaya 9 >

1 Bununla birlikte sıkıntı çekmiş olan ülke karanlıkta kalmayacak. Geçmişte Zevulun ve Naftali bölgelerini alçaltan Tanrı, gelecekte Şeria Irmağı'nın ötesinde, Deniz Yolu'nda, ulusların yaşadığı Celile'yi onurlandıracak.
Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:
2 Karanlıkta yürüyen halk Büyük bir ışık görecek; Ölümün gölgelediği diyarda Yaşayanların üzerine ışık parlayacak.
Watu wanaotembea katika giza wameona nuru kuu, wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.
3 Ya RAB, ulusu çoğaltacak, sevincini artıracaksın. Ekin biçenlerin neşelendiği, Ganimet paylaşanların coştuğu gibi, Onlar da sevinecek senin önünde.
Umelikuza taifa, na kuzidisha furaha yao, wanafurahia mbele zako, kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno, kama watu wafurahivyo wagawanyapo nyara.
4 Çünkü onlara yük olan boyunduruğu, Omuzlarını döven değneği, Onlara eziyet edenlerin sopasını paramparça edeceksin; Tıpkı Midyanlılar'ı yenilgiye uğrattığın günkü gibi.
Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani, umevunja nira iliyowalemea, ile gongo mabegani mwao na fimbo yake yeye aliyewaonea.
5 Savaşta giyilen çizmeleri Ve kana bulanmış giysileri Yakılacak, ateşe yem olacak.
Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani, na kila vazi lililovingirishwa katika damu vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa, vitakuwa kuni za kuwasha moto.
6 Çünkü bize bir çocuk doğacak, Bize bir oğul verilecek. Yönetim onun omuzlarında olacak. Onun adı Harika Öğütçü, Güçlü Tanrı, Ebedi Baba, Esenlik Önderi olacak.
Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume, nao utawala utakuwa mabegani mwake. Naye ataitwa Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
7 Davut'un tahtı ve ülkesi üzerinde egemenlik sürecek. Egemenliğinin ve esenliğinin büyümesi son bulmayacak. Egemenliğini adaletle, doğrulukla kuracak Ve sonsuza dek sürdürecek. Her Şeye Egemen RAB'bin gayreti bunu sağlayacak.
Kuongezeka kwa utawala wake na amani hakutakuwa na mwisho. Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi na juu ya ufalme wake, akiuthibitisha na kuutegemeza kwa haki na kwa adili, tangu wakati huo na hata milele. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote utatimiza haya.
8 Rab İsrail için, Yakup soyu için yargısını bildirdi. Bu yargı yerine gelecek.
Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo, utamwangukia Israeli.
9 Bütün halk, Efrayim ve Samiriye'de yaşayanlar, Rab'bin bu yargısını duyacak. Gururlu ve küstah olan bu halk diyor ki,
Watu wote watajua hili: Efraimu na wakazi wa Samaria, wanaosema kwa kiburi na majivuno ya mioyo,
10 “Kerpiç evler yıkıldı, Ama yerlerine yontma taştan evler yapacağız. Yabanıl incir ağaçları kesildi, Ama yerlerine sedir ağaçları dikeceğiz.”
“Matofali yameanguka chini, lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa, mitini imeangushwa, lakini tutapanda mierezi badala yake.”
11 Bundan dolayı RAB, Resin'in hasımlarını Halka karşı güçlendirecek; Düşmanlarını, doğudan Aramlılar'ı, Batıdan Filistliler'i ayaklandıracak. Bunlar ağızlarını ardına kadar açıp İsrail'i yutacaklar. Bütün bunlara karşın RAB'bin öfkesi dinmedi, Eli hâlâ kalkmış durumda.
Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao na kuchochea watesi wao.
Waashuru kutoka upande wa mashariki na Wafilisti kutoka upande wa magharibi wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
13 Halk kendisini cezalandıran RAB'be dönmeyecek, Her Şeye Egemen RAB'bi aramayacak.
Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga, wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 Bunun için RAB İsrail'den başı da kuyruğu da Hurma dalını da sazı da Bir günde kesip atacak.
Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia, tawi la mtende na tete katika siku moja.
15 Baş ileri gelen saygın kişi, Kuyruksa öğretisi sahte olan peygamberdir.
Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa, nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.
16 Çünkü bu halkı saptıranlar ona yol gösterenlerdir. Onları izleyenler de yem oluyor.
Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha, nao wale wanaoongozwa wamepotoka.
17 Bu yüzden Rab onların gençleri için sevinç duymayacak, Öksüzlerine, dul kadınlarına acımayacak. Çünkü hepsi tanrısızdır, kötülük yaparlar. Her ağız saçmalıyor. Bütün bunlara karşın RAB'bin öfkesi dinmedi, Eli hâlâ kalkmış durumda.
Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana, wala hatawahurumia yatima na wajane, kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu, na kila kinywa kinanena upotovu. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
18 Kötülük dikenli çalıları yiyip bitiren ateş gibidir. Ormandaki çalılığı tutuşturur, Duman sütunları yükseltir.
Hakika uovu huwaka kama moto; huteketeza michongoma na miiba, huwasha moto vichaka vya msituni, hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.
19 Her Şeye Egemen RAB'bin öfkesi Ülkeyi ateş gibi sardı. Halk ateşe yem olacak, Kardeş kardeşini esirgemeyecek.
Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote nchi itachomwa kwa moto, nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto. Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.
20 İnsanlar şurada burada bulduklarını yiyecekler, Ama aç kalacak, doymayacaklar. Herkes çocuğunun etini yiyecek:
Upande wa kuume watakuwa wakitafuna, lakini bado wataona njaa; upande wa kushoto watakuwa wakila, lakini hawatashiba. Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:
21 Manaşşe Efrayim'i, Efrayim Manaşşe'yi yiyecek, Sonra birlikte Yahuda'nın üzerine yürüyecekler. Bütün bunlara karşın RAB'bin öfkesi dinmedi, Eli hâlâ kalkmış durumda.
Manase atamla Efraimu, naye Efraimu atamla Manase; nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.

< Yeşaya 9 >