< Yeşaya 7 >

1 Uzziya oğlu Yotam oğlu Ahaz Yahuda Kralı'yken, Aram Kralı Resin'le Remalya oğlu İsrail Kralı Pekah Yeruşalim'e saldırdılar, ama ele geçiremediler.
Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
2 Davut'un torunları Aram'ın Efrayimliler'le güçbirliği ettiğini duydular. Ahaz'la halkının yürekleri rüzgarda sallanan orman ağaçları gibi titremeye başladı.
Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
3 Bu arada RAB Yeşaya'ya şöyle seslendi: “Ahaz'ı karşılamak için oğlun Şear-Yaşuv'la birlikte Yukarı Havuz'un su yolunun sonuna, Çırpıcı Tarlası'na giden yola çık.
Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
4 Ona de ki, ‘Dikkatli ve sakin ol, korkma! Şu tüten iki yanık odun parçasının –Aram Kralı Resin'le Remalya'nın oğlunun– öfkesinden korkma.
Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
5 Aram, Efrayim ve Remalya'nın oğlu sizin için kötü şeyler tasarlıyor. Diyorlar ki,
Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
6 Haydi, Yahuda'ya saldıralım, halkı korkutup ülkeyi ele geçirelim, Taveal'ın oğlunu kral ilan edelim.
“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
7 “‘Buna karşılık Egemen RAB diyor ki, bu tasarı asla gerçekleşmeyecek.
Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
8 Çünkü Şam sadece Aram'ın başkenti, Resin de sadece Şam'ın başıdır. Efrayim'e gelince, altmış beş yıl içinde paramparça edilip halk olmaktan çıkacak.
kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
9 Samiriye sadece Efrayim'in başkenti, Remalya'nın oğlu da sadece Samiriye'nin başıdır. Bana güvenmezseniz, güvenlikte olamazsınız.’”
Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
10 RAB Ahaz'a yine seslendi:
Bwana akasema na Ahazi tena,
11 “Tanrın RAB'den bir işaret iste; ölüler diyarı kadar derin, gökler kadar yüksek olsun.” (Sheol h7585)
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol h7585)
12 Ama Ahaz, “Hayır, istemem, RAB'bi sınamam” dedi.
Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
13 Bunun üzerine Yeşaya, “Dinleyin, ey Davut'un torunları!” dedi, “İnsanların sabrını taşırmanız yetmezmiş gibi şimdi de Tanrım'ın sabrını mı taşırıyorsunuz?
Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
14 Bundan ötürü Rab'bin kendisi size bir belirti verecek: İşte, kız gebe kalıp bir oğul doğuracak; adını İmmanuel koyacak.
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
15 Çocuk kötüyü reddedip iyiyi seçecek yaşa gelince tereyağı ve bal yiyecek.
Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
16 Ama çocuk kötüyü reddedip iyiyi seçecek yaşa gelmeden, seni dehşete düşüren o iki kralın toprakları ıssız kalacak.
Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
17 “RAB seni, halkını ve babanın soyunu Efrayim'in Yahuda'dan ayrıldığı günden bu yana görülmemiş bir felakete uğratacak; üzerinize Asur Kralı'nı saldırtacak.
Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
18 “O gün RAB Mısır ırmaklarının ta uçlarından sinekleri, Asur topraklarından arıları ıslıkla çağıracak.
Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
19 Akın akın gelip derin vadilerde, kaya kovuklarında, dikenli çalılıklarda, otlaklarda konaklayacaklar.
Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
20 “O gün Rab Fırat'ın ötesinden kiraladığı usturayla –Asur Kralı'yla– sakalınızı, saçlarınızı, beden kıllarınızı tıraş edecek.
Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
21 O günlerde bir inekle bir çift koyun besleyen
Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
22 aldığı bol süt sayesinde tereyağı yiyecek. Ülkede kalan herkes bal ve tereyağıyla beslenecek.
Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
23 “O gün bin gümüş değerinde bin asmaya sahip olan her bağ dikenli çalılarla dolacak.
Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
24 İnsanlar oralara okla, yayla gidecek. Çünkü ülkenin her yanı dikenli çalılarla kaplanacak.
Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
25 Bir zamanlar çapalanıp ekin ekilen tepeler korkudan kimsenin giremeyeceği dikenliklere dönecek, sığırın gezindiği, davarın çiğnediği yerler olacak.”
Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.

< Yeşaya 7 >