< Yeşaya 49 >

1 Ey kıyı halkları, işitin beni, Uzaktaki halklar, iyi dinleyin. RAB beni ana rahmindeyken çağırdı, Annemin karnındayken adımı koydu.
Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
2 Ağzımı keskin kılıç yaptı, Elinin gölgesinde gizledi beni. Beni keskin bir ok yaptı, Kendi ok kılıfına sakladı.
Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
3 Bana, “Kulumsun, ey İsrail, Görkemimi senin aracılığınla göstereceğim” dedi.
Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
4 Ama ben, “Boşuna emek verdim” dedim, “Gücümü boş yere, bir hiç için tükettim. RAB yine de hakkımı savunur, Tanrım yaptıklarımın karşılığını verir.”
Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
5 Kulu olmam için, Yakup soyunu kendisine geri getirmem, İsrail'i önünde toplamam için Rahimde beni biçimlendiren RAB şimdi şöyle diyor: –O'nun gözünde onurluyum, Tanrım bana güç kaynağı oldu.–
Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
6 “Yakup'un oymaklarını canlandırmak, Sağ kalan İsrailliler'i geri getirmek için Kulum olman yeterli değil. Seni uluslara ışık yapacağım. Öyle ki, kurtarışım yeryüzünün dört bucağına ulaşsın.”
yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
7 İnsanların hor gördüğüne, Ulusların iğrendiğine, Egemenlerin kulu olana İsrail'in Kurtarıcısı ve Kutsalı RAB diyor ki, “Seni seçmiş olan İsrail'in Kutsalı sadık RAB'den ötürü Krallar seni görünce ayağa kalkacak, Önderler yere kapanacak.”
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
8 RAB şöyle diyor: “Lütuf zamanında seni yanıtlayacağım, Kurtuluş günü sana yardım edecek, Seni koruyacağım. Seni halka antlaşma olarak vereceğim. Öyle ki, yıkık ülkeyi yeniden kurasın, Mülk olarak yeni sahiplerine veresin.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
9 Tutsaklara, ‘Çıkın’, Karanlıktakilere, ‘Dışarı çıkın’ diyeceksin. Yol boyunca beslenecek, Her çıplak tepede otlak bulacaklar.
kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
10 Acıkmayacak, susamayacaklar, Kavurucu sıcak ve güneş çarpmayacak onları. Çünkü onlara merhamet eden kendilerine yol gösterecek Ve onları pınarlara götürecek.
Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
11 Bütün dağlarımı yola dönüştüreceğim, Anayollarım yükseltilecek.
Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
12 İşte halkım ta uzaklardan, Kimi kuzeyden, kimi batıdan, kimi de Sinim'den gelecek.”
Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
13 Ey gökler, sevinçle haykırın, Neşeyle coş, ey yeryüzü! Ey dağlar, sevinç çığlıklarına katılın, Çünkü RAB halkını avutacak, Ezilene merhamet gösterecek.
Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
14 Oysa Siyon, “RAB beni terk etti, Rab beni unuttu” diyordu.
Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
15 Ama RAB, “Kadın emzikteki çocuğunu unutabilir mi?” diyor, “Rahminden çıkan çocuktan sevecenliği esirger mi? Kadın unutabilir, Ama ben seni asla unutmam.
“Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
16 Bak, adını avuçlarıma kazıdım, Duvarlarını gözlüyorum sürekli.
Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
17 Oğulların koşar adım geliyor, Seni yıkıp viran edenlerse çıkıp gidecek.
Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
18 Başını kaldır da çevrene bir bak: Hepsi toplanmış sana geliyor. Ben RAB, varlığım hakkı için diyorum ki, Onların hepsi senin süsün olacak, Bir gelin gibi takınacaksın onları.
Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
19 “Çünkü yıkılmış, viraneye dönmüştün, Ülken yerle bir olmuştu. Ama şimdi halkına dar geleceksin, Seni harap etmiş olanlar senden uzak duracaklar.
“Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
20 Yitirdiğini sandığın çocuklarının sesini yine duyacaksın: ‘Burası bize dar geliyor, Yaşayacak bir yer ver bize’ diyecekler.
Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
21 O zaman içinden, ‘Kim doğurdu bunları bana?’ diyeceksin, ‘Çocuklarımı yitirmiştim, doğuramıyordum. Sürgüne gönderilmiş, dışlanmıştım. Öyleyse bunları kim büyüttü? Yapayalnız kalmıştım, Nereden çıkıp geldi bunlar?’”
Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
22 Egemen RAB diyor ki, “Bakın, uluslara elimle işaret verdiğimde, Sancağımı yükselttiğimde halklara, Senin oğullarını kucaklarında getirecek, Kızlarını omuzlarında taşıyacaklar.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
23 Krallar size babalık, Prensesler sütannelik yapacak, Yüzüstü yere kapanıp Ayaklarının tozunu yalayacaklar. O zaman benim RAB olduğumu anlayacaksın. Bana umut bağlayan utandırılmayacak.”
Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
24 Güçlünün ganimeti elinden alınabilir mi? Zorbanın elindeki tutsak kurtulabilir mi?
Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
25 Ama RAB diyor ki, “Evet, güçlünün elindeki tutsaklar alınacak, Zorbanın aldığı ganimet de kurtarılacak. Seninle çekişenle ben çekişeceğim, Senin çocuklarını ben kurtaracağım.
Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
26 Sana zulmedenlere kendi etlerini yedireceğim, Tatlı şarap içmiş gibi kendi kanlarıyla sarhoş olacaklar. Böylece bütün insanlar bilecek ki Seni kurtaran RAB benim; Kurtarıcın, Yakup'un Güçlüsü benim.”
Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

< Yeşaya 49 >