< Yeşaya 27 >

1 O gün RAB Livyatan'ı, o kaçan yılanı, Evet Livyatan'ı, o kıvrıla kıvrıla giden yılanı Acımasız, kocaman, güçlü kılıcıyla cezalandıracak, Denizdeki canavarı öldürecek.
Katika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu, ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
2 O gün RAB, “Sevdiğim bağ için ezgiler söyleyin” diyecek,
Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
3 “Ben RAB, bağın koruyucusuyum, Onu sürekli sularım. Kimse zarar vermesin diye Gece gündüz beklerim.
Mimi, Bwana, ninalitunza, nalinyweshea maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
4 Kızgın değilim. Keşke karşıma dikenli çalılar çıksa! Onların üzerine yürür, Tümünü ateşe verirdim.
Mimi sijakasirika. Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeliichoma moto yote.
5 Ya da koruyuculuğuma sarılsınlar, Barışsınlar benimle, Evet, benimle barışsınlar.”
Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
6 Yakup soyu gelecekte kök salacak, İsrail filizlenip çiçeklenecek, Yeryüzünü meyvesiyle dolduracak.
Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
7 RAB İsrailliler'i, kendilerini cezalandıranları cezalandırdığı gibi cezalandırdı mı? Ya da İsrailliler'i başkalarını öldürdüğü gibi öldürdü mü?
Je, Bwana amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
8 RAB onları yargıladı, Kovup sürgüne gönderdi. Doğu rüzgarının estiği gün Onları şiddetli soluğuyla savurdu.
Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
9 Böylece Yakup soyunun suçu bağışlanacak. Günahlarının kaldırılmasının sonucu şöyle olacak: Sunağın taşlarını tebeşir taşı gibi un ufak ettiklerinde Ne Aşera putu ne de buhur sunağı kalacak.
Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atakapoyafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
10 Surlu kent terk edildi, Çöl kadar ıssız, sahipsiz bir yurt oldu. Dana orada otlayıp uzanacak, Filizlerini yiyip bitirecek.
Mji ulio na boma umebaki ukiwa, makao yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
11 Kuruyan dalları koparılacak, Kadınlar gelip bunları yakacaklar. Çünkü bu halk akıllı bir halk değil. Bu yüzden onları yaratan kendilerine acımayacak, Onlara biçim veren onları kayırmayacak.
Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaonyeshi fadhili.
12 Ey İsrailoğulları, o gün RAB gürül gürül akan Fırat ile Mısır Vadisi arasında harman döver gibi, sizi birer birer toplayacak.
Katika siku ile Bwana atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
13 Evet, o gün büyük bir boru çalınacak; Asur'da yitenlerle Mısır'a sürgün edilenler gelip kutsal dağda, Yeruşalim'de RAB'be tapınacaklar.
Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Bwana katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.

< Yeşaya 27 >