< Yeşaya 22 >

1 Görüm Vadisi'yle ilgili bildiri: Gürültü patırtı içinde eğlenen kent halkı, Ne oldu size, neden hepiniz damlara çıktınız? Ölenleriniz ne kılıçtan geçirildi, Ne de savaşta öldü.
Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
2
Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
3 Önderleriniz hep birlikte kaçtılar, Yaylarını kullanmadan tutsak alındılar. Uzağa kaçtığınız halde ele geçenlerin hepsi tutsak edildi.
Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
4 Bunun için dedim ki, “Beni yalnız bırakın, acı acı ağlayayım. Halkımın uğradığı yıkımdan ötürü Beni avutmaya kalkmayın.”
Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
5 Çünkü Rab'bin, Her Şeye Egemen RAB'bin Görüm Vadisi'nde kargaşa, bozgun Ve dehşet saçacağı gün, Duvarların yıkılacağı, Dağlara feryat edileceği gün geliyor.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
6 Elamlılar ok kılıflarını sırtlanıp savaş arabalarıyla, Atlılarıyla geldiler. Kîr halkı kalkanlarını açtı.
Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
7 Verimli vadileriniz savaş arabalarıyla doldu, Atlılar kent kapılarının karşısına dizildi.
Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
8 RAB'bin Yahuda'yı savunmasız bıraktığı gün Orman Sarayı'ndaki silahlara güvendiniz.
ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
9 Davut Kenti'nin duvarlarında Çok sayıda gedik olduğunu gördünüz, Aşağı Havuz'da su depoladınız,
mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
10 Yeruşalim'deki evleri saydınız, Surları onarmak için evleri yıktınız.
Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
11 Eski Havuz'un suları için İki surun arasında bir depo yaptınız. Ama bunu çok önceden tasarlayıp Gerçekleştirmiş olan Tanrı'ya güvenmediniz, O'nu umursamadınız.
Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
12 Rab, Her Şeye Egemen RAB O gün sizi ağlayıp yas tutmaya, Saçlarınızı kesip çul kuşanmaya çağırdı.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
13 Oysa siz keyif çatıp eğlendiniz, “Yiyelim içelim, nasıl olsa yarın öleceğiz” diyerek Sığır, koyun kestiniz, Et yiyip şarap içtiniz.
Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
14 Her Şeye Egemen RAB bana, “Siz ölene dek bu suçunuz bağışlanmayacak” diye seslendi. Rab, Her Şeye Egemen RAB böyle diyor.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
15 Rab, Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “Haydi, o kâhyaya, Sarayın sorumlusu Şevna'ya git ve de ki,
Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
16 ‘Burada ne işin var? Kimin var ki, kendine burada mezar kazdın, Yüksekte kendine mezar, kayada konut oydun?
Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
17 Ey güçlü kişi, RAB seni tuttuğu gibi şiddetle savuracak.
“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
18 Top gibi evirip çevirip Geniş bir ülkeye fırlatacak. Orada öleceksin, Gurur duyduğun arabaların orada kalacak. Efendinin evi için utanç nedenisin!
Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
19 Seni görevden alacak, Makamından alaşağı edeceğim.
Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
20 “‘O gün Hilkiya oğlu kulum Elyakim'i çağırıp
“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
21 Senin cüppeni ona giydireceğim. Senin kuşağınla onu güçlendirip Yetkini ona vereceğim. Yeruşalim'de yaşayanlara Ve Yahuda halkına o babalık yapacak.
Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 Davut'un evinin anahtarını ona teslim edeceğim. Açtığını kimse kapayamayacak, Kapadığını kimse açamayacak.
Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
23 Onu sağlam yere çakılmış çadır kazığı yapacağım, Ailesi için onur kürsüsü olacak.
Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
24 Ailenin ağırlığı –soyundan türeyen herkes– Taslardan kâselere kadar her küçük kap ona asılacak.’”
Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
25 Her Şeye Egemen RAB diyor ki, “O gün sağlam yere çakılmış kazık yerinden çıkacak, kırılıp düşecek, ona asılan yük de yok olacak.” Çünkü RAB böyle diyor.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.

< Yeşaya 22 >