< Yaratiliş 4 >

1 Adem karısı Havva ile yattı. Havva hamile kaldı ve Kayin'i doğurdu. “RAB'bin yardımıyla bir oğul dünyaya getirdim” dedi.
Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
2 Daha sonra Kayin'in kardeşi Habil'i doğurdu. Habil çoban oldu, Kayin ise çiftçi.
Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
3 Günler geçti. Bir gün Kayin toprağın ürünlerinden RAB'be sunu getirdi.
Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
4 Habil de sürüsünde ilk doğan hayvanlardan bazılarını, özellikle de yağlarını getirdi. RAB Habil'i ve sunusunu kabul etti.
Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
5 Kayin'le sunusunu ise reddetti. Kayin çok öfkelendi, suratını astı.
lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
6 RAB Kayin'e, “Niçin öfkelendin?” diye sordu, “Niçin surat astın?
Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
7 Doğru olanı yapsan, seni kabul etmez miyim? Ancak doğru olanı yapmazsan, günah kapıda pusuya yatmış, seni bekliyor. Ona egemen olmalısın.”
Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
8 Kayin kardeşi Habil'e, “Haydi, tarlaya gidelim” dedi. Tarlada birlikteyken kardeşine saldırıp onu öldürdü.
Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
9 RAB Kayin'e, “Kardeşin Habil nerede?” diye sordu. Kayin, “Bilmiyorum, kardeşimin bekçisi miyim ben?” diye karşılık verdi.
Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
10 RAB, “Ne yaptın?” dedi, “Kardeşinin kanı topraktan bana sesleniyor.
Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
11 Artık döktüğün kardeş kanını içmek için ağzını açan toprağın laneti altındasın.
Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
12 İşlediğin toprak bundan böyle sana ürün vermeyecek. Yeryüzünde aylak aylak dolaşacaksın.”
Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
13 Kayin, “Cezam kaldıramayacağım kadar ağır” diye karşılık verdi,
Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
14 “Bugün beni bu topraklardan kovdun. Artık huzurundan uzak kalacak, yeryüzünde aylak aylak dolaşacağım. Kim bulsa öldürecek beni.”
Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
15 Bunun üzerine RAB, “Seni kim öldürürse, ondan yedi kez öç alınacak” dedi. Kimse bulup öldürmesin diye Kayin'in üzerine bir nişan koydu.
Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
16 Kayin RAB'bin huzurundan ayrıldı. Aden bahçesinin doğusunda, Nod topraklarına yerleşti.
Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
17 Kayin karısıyla yattı. Karısı hamile kaldı ve Hanok'u doğurdu. Kayin o sırada bir kent kurmaktaydı. Kente oğlu Hanok'un adını verdi.
Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
18 Hanok'tan İrat oldu. İrat'tan Mehuyael, Mehuyael'den Metuşael, Metuşael'den Lemek oldu.
Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
19 Lemek iki kadınla evlendi. Birinin adı Âda, öbürünün ise Silla'ydı.
Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
20 Âda Yaval'ı doğurdu. Yaval sürü sahibi göçebelerin atasıydı.
Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
21 Kardeşinin adı Yuval'dı. Yuval lir ve ney çalanların atasıydı.
Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
22 Silla Tuval-Kayin'i doğurdu. Tuval-Kayin tunç ve demirden çeşitli kesici aletler yapardı. Tuval-Kayin'in kızkardeşi Naama'ydı.
Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
23 Lemek karılarına şöyle dedi: “Ey Âda ve Silla, beni dinleyin, Ey Lemek'in karıları, sözlerime kulak verin. Beni yaraladığı için Bir adam öldürdüm, Beni hırpaladığı için Bir genci öldürdüm.
Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
24 Kayin'in yedi kez öcü alınacaksa, Lemek'in yetmiş yedi kez öcü alınmalı.”
Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
25 Adem karısıyla yine yattı. Havva bir erkek çocuk doğurdu. “Tanrı Kayin'in öldürdüğü Habil'in yerine bana başka bir oğul bağışladı” diyerek çocuğa Şit adını verdi.
Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
26 Şit'in de bir oğlu oldu, adını Enoş koydu. O zaman insanlar RAB'bi adıyla çağırmaya başladı.
Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.

< Yaratiliş 4 >