< Yaratiliş 29 >

1 Yakup yoluna devam ederek doğu halklarının ülkesine vardı.
Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
2 Kırda bir kuyu gördü. Kuyunun yanıbaşında üç davar sürüsü yatıyordu. Sürülere o kuyudan su verilirdi. Kuyunun ağzında büyük bir taş vardı.
Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
3 Bütün sürüler oraya toplanınca, çobanlar kuyunun ağzındaki taşı yuvarlar, davarlarını suvardıktan sonra taşı yine yerine, kuyunun ağzına koyarlardı.
Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
4 Yakup çobanlara, “Kardeşler, nerelisiniz?” diye sordu. Çobanlar, “Harranlı'yız” diye yanıtladılar.
Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
5 Yakup, “Nahor'un torunu Lavan'ı tanıyor musunuz?” diye sordu. “Tanıyoruz” dediler.
Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
6 Yakup, “İyi midir?” diye sordu. “İyidir. İşte kızı Rahel davarlarla birlikte geliyor.”
Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
7 Yakup, “Akşama daha çok var” dedi, “Sürülerin toplanma vakti değil. Davarlarınızı suvarın, götürüp otlatın.”
Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
8 Çobanlar, “Bütün sürüler toplanmadan, kuyunun ağzındaki taşı yuvarlamadan olmaz” dediler, “Ancak o zaman davarları suvarabiliriz.”
Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
9 Yakup onlarla konuşurken Rahel babasının davarlarını getirdi. Rahel çobanlık yapıyordu.
Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
10 Yakup dayısı Lavan'ın kızı Rahel'i ve davarları görünce, gidip kuyunun ağzındaki taşı yuvarladı, dayısının davarlarını suvardı.
Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
11 Rahel'i öperek hıçkıra hıçkıra ağladı.
Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
12 Rahel'e baba tarafından akraba olduklarını, Rebeka'nın oğlu olduğunu anlattı. Rahel koşup babasına haber verdi.
Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
13 Lavan, yeğeni Yakup'un geldiğini duyunca, onu karşılamaya koştu. Ona sarılıp öptü, evine getirdi. Yakup bütün olanları Lavan'a anlattı.
Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
14 Lavan, “Sen benim etim, kemiğimsin” dedi. Yakup Lavan'ın yanında bir ay kaldıktan sonra,
Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
15 Lavan, “Akrabamsın diye benim için bedava mı çalışacaksın?” dedi, “Söyle, ne kadar ücret istiyorsun?”
Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
16 Lavan'ın iki kızı vardı. Büyüğünün adı Lea, küçüğünün adı Rahel'di.
Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
17 Lea'nın gözleri alımlıydı, Rahel ise boyu bosu yerinde, güzel bir kızdı.
Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
18 Yakup Rahel'e aşıktı. Lavan'a, “Küçük kızın Rahel için sana yedi yıl hizmet ederim” dedi.
Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
19 Lavan, “Onu sana vermek başkasına vermekten daha iyidir” dedi, “Yanımda kal.”
Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
20 Yakup Rahel için yedi yıl çalıştı. Rahel'i sevdiği için, yedi yıl ona birkaç gün gibi geldi.
Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
21 Lavan'a, “Zaman doldu, kızını ver, evleneyim” dedi.
Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
22 Lavan bütün yöre halkını toplayıp bir şölen verdi.
Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
23 Gece kızı Lea'yı Yakup'a götürdü. Yakup onunla yattı.
Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
24 Lavan cariyesi Zilpa'yı kızı Lea'nın hizmetine verdi.
Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
25 Sabah olunca Yakup bir de baktı ki, yanındaki Lea! Lavan'a, “Nedir bana bu yaptığın?” dedi, “Ben Rahel için yanında çalışmadım mı? Niçin beni aldattın?”
Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
26 Lavan, “Bizim buralarda adettir. Büyük kız dururken küçük kız evlendirilmez” dedi,
Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
27 “Bu bir haftayı tamamla, Rahel'i de sana veririz. Yalnız ona karşılık yedi yıl daha yanımda çalışacaksın.”
Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
28 Yakup kabul etti. Lea'yla bir hafta geçirdi. Sonra Lavan kızı Rahel'i de ona verdi.
Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
29 Cariyesi Bilha'yı Rahel'in hizmetine verdi.
Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
30 Yakup Rahel'le de yattı. Onu Lea'dan çok sevdi. Lavan'a yedi yıl daha hizmet etti.
Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
31 RAB Lea'nın sevilmediğini görünce, çocuk sahibi olmasını sağladı. Oysa Rahel kısırdı.
Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
32 Lea hamile kalıp bir erkek çocuk doğurdu. Adını Ruben koydu. “Çünkü RAB mutsuzluğumu gördü” dedi, “Kuşkusuz artık kocam beni sever.”
Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
33 Yine hamile kaldı ve bir erkek çocuk daha doğurdu. “RAB sevilmediğimi duyduğu için bana bu çocuğu verdi” diyerek adını Şimon koydu.
Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
34 Üçüncü kez hamile kalıp bir daha erkek çocuk doğurdu. “Artık kocam bana bağlanacak” dedi, “Çünkü ona üç erkek çocuk doğurdum.” Onun için çocuğa Levi adı verildi.
Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
35 Dördüncü kez hamile kaldı ve bir erkek çocuk daha doğurdu. “Bu kez RAB'be övgüler sunacağım” dedi. Onun için çocuğa Yahuda adını verdi. Bir süre doğum yapmadı.
Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.

< Yaratiliş 29 >