< Ezra 4 >

1 Yahudalılar'la Benyaminliler'in düşmanları, sürgünden dönenlerin İsrail'in Tanrısı RAB için bir tapınak yaptığını duyunca,
Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
2 Zerubbabil'in ve boy başlarının yanına vardılar. “Tapınağı sizinle birlikte kuralım” dediler, “Çünkü biz de, sizin gibi Tanrınız'a tapıyoruz; bizi buraya getiren Asur Kralı Esarhaddon'un döneminden bu yana sizin Tanrınız'a kurban sunuyoruz.”
wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
3 Ne var ki Zerubbabil, Yeşu ve İsrail'in öteki boy başları, “Tanrımız'a bir tapınak kurmak size düşmez” diye karşılık verdiler, “Pers Kralı Koreş'in buyruğu uyarınca, İsrail'in Tanrısı RAB için tapınağı yalnız biz kuracağız.”
Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
4 Bunun üzerine çevre halkı Yahudalılar'ı tapınağın yapımından caydırmak için korkutmaya, cesaretlerini kırmaya girişti.
Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
5 Tasarılarına engel olmak için Pers Kralı Koreş'in döneminden Pers Kralı Darius'un krallığına dek rüşvetle danışmanlar tuttular.
Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
6 Ahaşveroş'un krallığının başlangıcında, Yahudalılar'ın düşmanları Yahuda ve Yeruşalim'de yaşayanları suçlayan bir belge düzenlediler.
Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
7 Pers Kralı Artahşasta'nın krallığı döneminde, Bişlam, Mitredat, Taveel ve öbür çalışma arkadaşları Artahşasta'ya bir mektup yazdılar. Mektup Aramice yazılıp çevrildi.
Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
8 Vali Rehum ile Yazman Şimşay Kral Artahşasta'ya Yeruşalim'i suçlayan bir mektup yazdılar. Mektup şöyleydi:
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
9 “Vali Rehum, Yazman Şimşay ve öbür çalışma arkadaşları, yargıçlar, yöneticiler, görevliler, Persler, Erekliler, Babilliler, Elam topraklarından gelen Sus halkı,
Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
10 büyük ve onurlu Asurbanipal'ın sürüp Samiriye Kenti'yle Fırat'ın batı yakasındaki bölgeye yerleştirdiği öbür halklarından.”
na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
11 İşte Kral Artahşasta'ya gönderilen mektubun örneği: “Kral Artahşasta'ya, “Fırat'ın batı yakasındaki bölgede yaşayan kullarından:
(Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
12 “Yönetimindeki öbür bölgelerden çıkıp bize gelen Yahudiler Yeruşalim'e yerleşerek o asi ve kötü kenti yeniden kurmaya başladılar. Bunu bilgine sunuyoruz. Temelini pekiştiriyor, surlarını tamamlıyorlar.
Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
13 Ey kral, bilmelisin ki, bu kent yeniden kurulur, surları tamamlanırsa, Yahudiler yine vergi ödemeyecek; krallığının geliri de azalacak.
Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
14 Biz sarayının ekmeğini yedik. Sana zarar gelmesine izin veremeyiz. Bunun için, haberin olsun diye bu mektubu gönderiyoruz.
Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
15 Atalarının belgeleri araştırılsın. Kayıtlarda bu kentin asi, krallara, valilere zarar veren bir kent olduğunu göreceksin. Bu kent öteden beri başkaldıran bir kenttir. Yerle bir edilmesinin nedeni de budur.
ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
16 Bu yüzden, ey kral, sana bildiriyoruz: Bu kent yeniden kurulur, surları tamamlanırsa, Fırat'ın batı yakasındaki bölgede hiçbir payın kalmayacak.”
Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
17 Kral şu yanıtı gönderdi: “Samiriye'de ve Fırat'ın batı yakasındaki öbür yerlerde yaşayan Vali Rehum'a, Yazman Şimşay'a ve öbür çalışma arkadaşlarına selamlar.
Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
18 “Bize gönderdiğiniz mektup çevrilip bana okundu.
Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
19 Buyruğum üzerine araştırma yapıldı. Bu kentin öteden beri krallara başkaldırdığı, isyan ettiği, ayaklandığı saptandı.
Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
20 Yeruşalim'i güçlü krallar yönetti. Fırat'ın batı yakasındaki bütün bölgede egemenlik sürdüler. Oradaki halktan vergi topladılar.
Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
21 Şimdi işi durdurmaları için bu adamlara bir buyruk çıkarın. Öyle ki, ben buyruk vermedikçe kent yeniden kurulmasın.
Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
22 Bu konuya özen gösterin; krallığıma daha fazla zarar gelmesin.”
Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
23 Kral Artahşasta'nın mektubunun örneği kendilerine okunur okunmaz, Rehum, Yazman Şimşay ve öbür çalışma arkadaşları hemen Yeruşalim'e Yahudiler'in yanına gittiler ve zorla onları durdurdular.
Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
24 Böylece Tanrı'nın Yeruşalim'deki Tapınağı'nın yapımı, Pers Kralı Darius'un krallığının ikinci yılına dek askıda kaldı.
Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.

< Ezra 4 >