< Hezekiel 5 >

1 “Ey insanoğlu, keskin bir kılıç al, berber usturası gibi kullanarak başını, sakalını tıraş et. Sonra bir terazi getir, kılları bölümlere ayır.
“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
2 Yeruşalim'in kuşatılması bitince, kılların üçte birini kentin ortasında yakacaksın. Üçte birini kılıçla kentin çevresine fırlatacak, kalan üçte birini de rüzgara savuracaksın. Ben de yalın kılıç onların peşine düşeceğim.
Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
3 Birkaç tel kıl bırak, giysinin kıvrımlarına tak.
Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
4 Yine birkaçını alıp ateşe at, yansın. O kıllardan bütün İsrail halkına ateş yayılacak.
Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
5 “Egemen RAB diyor ki: Bu Yeruşalim'i ulusların ortasına yerleştirdim, çevresini ülkelerle kuşattım.
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
6 Öyleyken Yeruşalim çevresindeki bütün uluslardan ve ülkelerden daha çok kötülük yaparak ilkelerimi, kurallarımı çiğnedi. İlkelerime karşı geldi, kurallarım uyarınca davranmadı.
Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
7 Bundan ötürü Egemen RAB diyor ki: Çevrenizde yaşayan uluslardan daha azgındınız, kurallarımı izlemediniz, ilkelerime uymadınız. Çevrenizde yaşayan ulusların ilkelerine de uymadınız.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
8 “Bundan ötürü Egemen RAB diyor ki: İşte ben size karşıyım, ulusların gözü önünde sizi cezalandıracağım.
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
9 Yaptığınız bütün iğrençlikler yüzünden önceden yapmadığımı, bir daha yapmayacağımı size yapacağım.
Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
10 Böylece aranızda babalar çocuklarını, çocuklar da babalarını yiyecekler. Sizi cezalandıracağım, sağ kalanlarınızı her yana dağıtacağım.
Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
11 Egemen RAB varlığım hakkı için diyor, madem tapınağımı iğrenç put ve uygulamalarınızla kirlettiniz, ben de sizi esirgemeyecek, size acımayacak, sizi kayırmayacağım.
Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
12 Kentte yaşayanlarınızın üçte biri salgın hastalık ya da kıtlık yüzünden yok olacak; üçte biriniz çevrede kılıçtan geçirilecek; üçte birinizi de her yana dağıtıp yalın kılıç peşinize düşeceğim.
Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
13 “Böylece kızgınlığım son bulacak, onlara karşı öfkemi yatıştıracağım. O zaman ben de rahata kavuşacağım. Öfkemi onların üzerine boşaltınca, ben RAB'bin kıskançlığımdan onlarla konuştuğumu anlayacaklar.
“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
14 “Çevrenizdeki uluslar arasında, yoldan her geçenin gözü önünde sizi yıkıma uğratacak, aşağılayacağım.
“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
15 Öfke, kızgınlık ve acı paylamalarla sizi cezalandırdığımda çevrenizdeki uluslar arasında alay konusu olacak, aşağılanacaksınız; ders alınacak, şaşılacak bir duruma düşeceksiniz. Ben, RAB bunu söyledim.
Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
16 Sizi yok etmek için üzerinize öldürücü, yıkıcı kıtlık oklarını salacağım. Üzerinize salacağım kıtlığı daha da artıracak, sizi her türlü yiyecekten yoksun bırakacağım.
Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
17 Üzerinize kıtlık ve yabanıl hayvanlar salacağım, sizi çocuklarınızdan edecekler. Salgın hastalık ve dökülen kan sizi süpürüp yok edecek; başınıza da kılıç getireceğim. Ben, RAB böyle söyledim.”
Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”

< Hezekiel 5 >