< Hezekiel 45 >

1 “‘Ülkeyi mülk olarak paylaştırdığınız zaman, RAB'be ülkeden pay olarak 25 000 arşın uzunlukta, 20 000 arşın genişlikte kutsal bir bölge ayıracaksınız. Bütün bu bölge kutsal olacak.
“‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000, upana wake dhiraa 20,000 eneo hili lote litakuwa takatifu.
2 Uzunluğu ve genişliği 500 arşınlık bir bölüm kutsal yer için, 50 arşınlık bir yer de çevresindeki alan için ayrılacak.
Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini.
3 Bu bölgeden uzunluğu 25 000 arşınlık, genişliği 10 000 arşınlık bir bölüm ölçeceksiniz. Tapınak, En Kutsal Yer orada olacak.
Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu.
4 Burası tapınakta hizmet etmek üzere RAB'be yaklaşan kâhinlere ayrılacak ve ülkenin kutsal payı olacak. Kâhinlerin evleri de tapınak da o kutsal bölgede olacak.
Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu.
5 Tapınakta hizmet eden Levililer'e miras olarak 25 000 arşın uzunlukta, 10 000 arşın genişlikte bir bölge verilecek. Orada, yaşamaları için kendilerine ait kentler olacak.
Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.
6 “‘Kutsal bölgeye düşen payla birlikte kent için uzunluğu 25 000, genişliği 5 000 arşınlık bir pay ayıracaksınız; bu bütün İsrail halkı için olacak.
“‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 “‘Kutsal bölgeye düşen pay ile kente düşen payın iki yanındaki topraklar öndere verilecek. Batıdan batıya, doğudan doğuya doğru uzanacak. Batı sınırından doğu sınırına dek uzunluğu bir İsrail oymağına düşen pay kadardır.
“‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila.
8 Bu toprak İsrail'de önderin payı olacak. Bundan böyle önderlerim halkıma bir daha baskı yapmayacak, ama oymaklarına göre İsrail halkına ülkeyi miras olarak verecekler.
Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.
9 “‘Egemen RAB şöyle diyor: Yeter artık, ey İsrail önderleri! Zorbalığı, baskıyı bırakın. Adil ve doğru olanı yapın. Halkımı kendi topraklarından kovmayın. Egemen RAB böyle diyor.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi.
10 Doğru ölçüler kullanın, kullandığınız efa ve bat doğru olsun.
Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa na bathi.
11 Efa ile bat aynı ölçüde olsun. Bat homerin onda birine, efa da homerin onda birine eşit olmalı. İkisinin de ölçüsü homere göre olacak.
Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili.
12 Bir şekel yirmi geraya eşit olmalı. Altmış şekel de bir minaya eşit olmalı.’”
Shekeli moja itakuwa gera ishirini. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.
13 “‘Sunacağınız sunular şunlardır: Her homer buğdaydan efanın altıda biri, her homer arpadan efanın altıda biri kadarını vereceksiniz.
“‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri.
14 Bat ölçüsüne göre istenen zeytinyağı miktarı, her kordan batın onda biri kadardır. Bir kor on bat ya da bir homere eşittir.
Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.)
15 İsrail'in sulak otlaklarındaki sürüden iki yüz koyundan bir koyun alınacak. Halkın günahlarını bağışlatmak için bu koyunlar yakmalık sunular, tahıl ve esenlik sunuları için kullanılacak. Egemen RAB böyle diyor.
Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi.
16 Ülke halkı bu armağanları İsrail'deki öndere verecek.
Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum.
17 İsrail'de kutlanan bütün bayramlarda –şenliklerde, Yeni Ay törenlerinde, Şabat günlerinde– tahıl sunularını, yakmalık ve dökmelik sunuları önder sağlayacak. İsrail halkının günahlarını bağışlatmak için yakmalık sunuları, günah, tahıl, esenlik sunularını sağlayacak.
Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.
18 “‘Egemen RAB şöyle diyor: Birinci ayın birinci günü kusursuz bir boğa alacak, tapınağı arındıracaksın.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu.
19 Kâhin günah sunusunun kanından alıp tapınağın kapı sövelerine, sunağın üst çıkıntısının dört köşesine, iç avlunun kapı sövelerine sürecek.
Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani.
20 Yanlışlıkla ya da bilgisizlikten günah işleyen biri için ayın yedinci günü aynısını yapacaksın. Böylece tapınağı arındıracaksın.
Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.
21 “‘Birinci ayın on dördüncü günü Fısıh Bayramı'nı yedi gün kutlayacak, mayasız ekmek yiyeceksiniz.
“‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
22 O gün önder kendisi ve ülke halkı için günah sunusu olarak bir boğa sağlayacak.
Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi.
23 Yedi gün bayram boyunca her gün RAB'be yakmalık sunu olarak kusursuz yedi boğayla yedi koç, günah sunusu olarak da bir teke sağlayacak.
Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
24 Tahıl sunusu olarak her boğa ve koç için birer efa tahıl, her efa için bir hin zeytinyağı sağlayacak.
Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.
25 “‘Yedinci ayın on beşinci günü başlayan ve yedi gün süren bayramda önder yakmalık sunuları, günah ve tahıl sunularını, zeytinyağını her gün aynı miktarda sağlayacak.
“‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.

< Hezekiel 45 >