< Hezekiel 39 >

1 “İnsanoğlu, Gog'a karşı peygamberlik et ve ona de ki, ‘Egemen RAB şöyle diyor: Ey Roş'un, Meşek'in, Tuval'ın önderi Gog, sana karşıyım.
“Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
2 Seni geri çevirip sürükleyeceğim. Seni uzak kuzeyden çıkarıp İsrail'in dağlarına getireceğim.
Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
3 Sol elindeki yayını vuracak, sağ elindeki oklarını düşüreceğim.
Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
4 Sen de askerlerinle senden yana olan uluslar da İsrail dağlarına serileceksiniz. Sizi yem olarak her çeşit yırtıcı kuşa, yabanıl hayvana vereceğim.
Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
5 Açık kırlarda düşüp öleceksiniz. Çünkü bunu ben söyledim. Egemen RAB böyle diyor.
Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
6 Magog'un ve kıyıda güvenlik içinde yaşayanların üzerine ateş yağdıracağım. O zaman benim RAB olduğumu anlayacaklar.
Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
7 “‘Halkım İsrail arasında kutsal adımı tanıtacağım. Bundan böyle kutsal adımın aşağılanmasına izin vermeyeceğim. Uluslar benim İsrail'de kutsal olan RAB olduğumu anlayacaklar.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
8 O gün yaklaştı! Söylediklerim olacak. Egemen RAB böyle diyor. Budur sözünü ettiğim gün!
Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
9 “‘O zaman İsrail kentlerinde yaşayanlar dışarı çıkıp topladıkları silahları yakacaklar. Küçük büyük kalkanları, yayları, okları, sopaları, mızrakları ateşe atacaklar. Bunlarla yedi yıl ateş yakacaklar.
Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
10 Kırdan odun toplamayacak, ormandan odun kesmeyecekler. Yakmak için silahları kullanacaklar. Mallarını yağmalayanları yağmalayacak, kendilerini soyanları soyacaklar. Egemen RAB böyle diyor.
Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
11 “‘O gün Lut Gölü'nün doğusunda, Gezginler Deresi'nde Gog'a İsrail'de bilinen bir mezar yeri vereceğim. Gog'la bütün ordusu orada gömülecek. Oraya Hamon-Gog Vadisi adı verilecek. Oradan geçecek gezginlerin önü kesilecek.
Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
12 İsrail halkı ülkeyi arındırmak için onları gömecek. Bu yedi ay sürecek.
Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
13 Onları bütün ülke halkı gömecek. Görkemimi açıkladığım gün onlar için onur olacak. Egemen RAB böyle diyor.
Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
14 “‘Ülkeyi arındırmak için adamlar görevlendirilecek. Bazıları ülkeyi sürekli dolaşacak, öbürleriyse yerde kalan cesetleri gömecekler. Yedi aylık süre bitince, araştırma işine başlayacaklar.
Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
15 Bu adamlar ülkenin her yanını dolaşacak. Bir insan kemiği görünce, mezarcılar onu Hamon-Gog Vadisi'ne gömünceye dek, yanına bir işaret koyacak.
Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
16 Orada Hamona adında bir kent olacak. Böylelikle ülke arındırılacak.’
Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
17 “İnsanoğlu, Egemen RAB şöyle diyor: Her çeşit kuşa ve yabanıl hayvana seslen: ‘Sizin için hazırlayacağım kurbana, İsrail dağları üzerindeki büyük kurbana gelin, her yandan toplanın! Orada et yiyecek, kan içeceksiniz.
Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
18 Başan'ın besili hayvanlarının –koçların, kuzuların, tekelerin, boğaların– etini yiyip kanını içer gibi yiğitlerin etini yiyecek, dünya önderlerinin kanını içeceksiniz.
Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
19 Sizin için hazırlayacağım kurbandan doyana dek yağ yiyeceksiniz, sarhoş oluncaya dek kan içeceksiniz.
Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
20 Soframda atlardan, atlılardan, yiğitlerden ve her çeşit askerden bol bol yiyip doyacaksınız.’ Egemen RAB böyle diyor.
Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
21 “Görkemimi uluslar arasında açıklayacağım. Bütün uluslar kendilerine verdiğim cezayı, üzerlerine koyduğum elimi görecekler.
Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
22 İsrail halkı o günden başlayarak benim Tanrıları RAB olduğumu anlayacak.
Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
23 Uluslar İsrail halkının işlediği suç yüzünden, bana ihanet ettiği için sürgüne gittiğini anlayacaklar. Yüzümü onlardan gizledim, onları düşmanlarının eline teslim ettim, hepsi kılıçtan geçirildi.
Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
24 Onları kirliliklerine, isyanlarına göre cezalandırdım, yüzümü onlardan gizledim.
Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
25 “Bundan ötürü Egemen RAB şöyle diyor: Yakup'un sürgündeki soyunu geri getirecek, İsrail halkına acıyacağım. Kutsal adımı kıskançlıkla koruyacağım.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
26 Ülkelerinde güvenlik içinde yaşayınca, onları korkutan kimse olmayınca, utançlarını, bana ettikleri bütün ihanetleri unutacaklar.
Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
27 Onları uluslar arasından geri getirip düşman ülkelerinden topladığım zaman, onlar aracılığıyla birçok ulusa kutsallığımı göstereceğim.
Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
28 O zaman benim Tanrıları RAB olduğumu anlayacaklar. Onları uluslar arasına sürgüne göndermeme karşın, hiçbirini bırakmadan ülkelerine geri getireceğim.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
29 Onlardan bir daha yüzümü gizlemeyeceğim, çünkü İsrail halkı üzerine Ruhum'u dökeceğim.” Egemen RAB böyle diyor.
Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Hezekiel 39 >