< Yasa'Nin Tekrari 3 >

1 “Bundan sonra dönüp Başan'a doğru ilerledik. Başan Kralı Og'la ordusu bizimle savaşmak için Edrei'de karşımıza çıktı.
Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
2 RAB bana, ‘Ondan korkma!’ dedi, ‘Çünkü onu da ordusuyla ülkesini de senin eline teslim ettim. Amorlular'ın Heşbon'da yaşayan Kralı Sihon'a yaptığının aynısını ona da yapacaksın.’
Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
3 “Böylece Tanrımız RAB, Başan Kralı Og'u ve halkını da elimize teslim etti. Hiçbirini sağ bırakmadan hepsini yok ettik.
Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
4 Bütün kentlerini ele geçirdik. Ele geçirmediğimiz tek kent kalmadı. Hepsi altmış kentti: Başan'da Og'un ülkesi olan bütün Argov bölgesi.
Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
5 Bütün bu kentler yüksek surlarla, kapılarla, sürgülerle sağlamlaştırılmıştı. Bunlardan başka surla çevrilmemiş birçok köy de vardı.
Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
6 Heşbon Kralı Sihon'a yaptığımız gibi hepsini yok ettik. Her kenti, kadın, erkek ve çocuklarla birlikte, tümüyle yok ettik.
Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
7 Hayvanlara ve kentlerdeki mallara ise el koyduk.
Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
8 “Arnon Vadisi'nden Hermon Dağı'na kadar Şeria Irmağı'nın doğu yakasındaki toprakları iki Amorlu kralın elinden aldık.
Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
9 –Saydalılar Hermon'a Siryon, Amorlular'sa Senir derler.–
(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
10 Ovadaki bütün kentleri, bütün Gilat'ı, Og'un ülkesine ait kentler olan Salka ve Edrei'ye uzanan bütün Başan'ı ele geçirdik.”
Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
11 –Refalılar'dan yalnız Başan Kralı Og sağ kalmıştı. Og'un Ammonlular'ın Rabba Kenti'ndeki yatağı demirdendi. O gün kullanılan arşın ölçüsüne göre uzunluğu dokuz, eni dört arşındı.–
(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
12 “O sırada ele geçirdiğimiz topraklardan Arnon Vadisi yakınındaki Aroer Kenti'nin kuzeyini, Gilat dağlık bölgesinin yarısıyla oradaki kentleri Ruben ve Gad oymaklarına verdim.
Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
13 Gilat'ın geri kalan bölümünü ve Og'un ülkesi Başan'ı Manaşşe oymağının yarısına verdim. Başan'daki Argov bölgesi Refalılar ülkesi diye bilinirdi.
Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
14 Manaşşe soyundan Yair, Geşur ile Maaka sınırına dek uzanan bütün Argov bölgesini aldı. Başan denilen bölgeye kendi adını verdi. Orası bugün de Havvot-Yair diye anılıyor.
Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
15 Makir'e Gilat'ı verdim.
Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
16 Gilat'la Arnon Vadisi arasında kalan toprakları Ruben ve Gad oymaklarına verdim. Vadinin ortası onların sınırıydı; Ammonlular'la sınırları ise Yabbuk Irmağı'ydı.
Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
17 Arava'da da sınır Şeria Irmağı'ydı; Kinneret'ten Arava –Lut– Gölü'ne, doğuda Pisga yamaçlarının aşağısına kadar uzanıyordu.
Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
18 “O zaman size şöyle buyruk verdim: ‘Tanrınız RAB mülk edinmek için bu ülkeyi size verdi. Bütün savaşçılarınız silahlı olarak İsrailli kardeşlerinizin önüsıra gitsin.
Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
19 Ancak RAB sizi rahata erdirdiği gibi onları da rahata erdirene ve onlar Tanrınız RAB'bin Şeria Irmağı'nın karşı yakasında kendilerine vereceği toprakları ele geçirene kadar, kadınlarınız, çocuklarınız ve hayvanlarınız –biliyorum, birçok hayvanınız var– size verdiğim kentlerde kalsın. Ondan sonra, her biriniz size verdiğim toprağa dönebilir.’”
Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
21 “O zaman Yeşu'ya, ‘Tanrın RAB'bin bu iki krala neler yaptığını gözlerinle gördün’ dedim, ‘RAB gideceğin bütün ülkelere aynısını yapacak.
Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
22 Onlardan korkmayın! Tanrınız RAB sizin için savaşacak.’
Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
23 “Sonra RAB'be yalvardım:
Wakati huo nilimsihi Bwana:
24 ‘Ey Egemen RAB, büyüklüğünü ve güçlü elini bana göstermeye başladın. Gökte ve yerde senin yaptığın yüce işleri yapabilecek başka bir tanrı yok!
“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
25 İzin ver de Şeria Irmağı'ndan geçip karşı yakadaki o verimli ülkeyi, o güzel dağlık bölgeyi ve Lübnan'ı göreyim.’
Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
26 “Ama RAB sizin yüzünüzden bana öfkelendi, yalvarışıma kulak asmadı. Bana, ‘Yeter artık!’ dedi, ‘Bir daha bu konudan söz etme bana.
Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
27 Pisga Dağı'na çık. Batıya, kuzeye, güneye, doğuya bak. Gözlerinle gör. Çünkü Şeria Irmağı'ndan geçmeyeceksin.
Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
28 Yeşu'ya görev ver. Onu güçlendir ve yüreklendir. Çünkü bu halk Şeria Irmağı'ndan onun önderliğinde geçecek. Göreceğin toprakları halka o miras olarak verecek.’
Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
29 Böylece Beytpeor'un karşısındaki vadide kaldık.”
Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

< Yasa'Nin Tekrari 3 >