< Daniel 8 >

1 Kral Belşassar'ın krallığının üçüncü yılında, ben Daniel daha önce gördüğüm görümden başka bir görüm gördüm.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 Görümde kendimi Elam İli'ndeki Sus Kalesi'nde, Ulay Kanalı'nın yanında gördüm.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 Gözlerimi kaldırıp bakınca kanal kıyısında duran bir koç gördüm; iki uzun boynuzu vardı. Boynuzlardan daha geç çıkanı öbüründen daha uzundu.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 Koçun batıya, kuzeye, güneye doğru boynuz attığını gördüm. Hiçbir hayvan ona karşı koyamıyor, kimse onun elinden kurtaramıyordu. Koç dilediği gibi davrandı ve gitgide güçlendi.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 Ben bu olayı düşünürken, batıdan ansızın gözleri arasında çarpıcı bir boynuzu olan bir teke geldi. Yere basmadan bütün dünyayı aştı.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 Güç ve öfkeyle, kanalın yanında durduğunu gördüğüm iki boynuzlu koça doğru koştu.
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 Öfkeyle saldırdığını, koça vurup boynuzlarını kırdığını gördüm. Koçun tekeye karşı duracak gücü yoktu; teke koçu yere vurup çiğnedi. Koçu onun elinden kurtaracak kimse yoktu.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 Teke çok güçlendi, ama en güçlü olduğu sırada büyük boynuzu kırıldı. Kırılan boynuzun yerine, göğün dört rüzgarına doğru çarpıcı dört boynuz çıktı.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 Bu boynuzların birinden başka bir küçük boynuz çıktı; güneye, doğuya ve Güzel Ülke'ye doğru yayılarak çok güçlendi.
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 Göklerin ordusuna erişinceye dek büyüdü. Gökteki ordudan ve yıldızlardan bazılarını yeryüzüne düşürdü, ayakları altına alıp çiğnedi.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 Kendisini Gök Ordusu'nun Önderi kadar yükseltti. Tanrı'ya sunulan günlük sunu kaldırıldı, O'nun tapınağı yıkıldı.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 Başkaldırı yüzünden günlük sunuya karşı çıkıldı. Gerçek ayak altında çiğnendi. Küçük boynuz yaptığı her şeyde başarılı oldu.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Sonra kutsal bir varlığın konuştuğunu duydum. Başka kutsal bir varlık ona, “Bu görümde –günlük sunuyla, yıkım getiren başkaldırıyla, kutsal yerin ve ordunun ayak altında çiğnenmesiyle ilgili görümde– olanlar ne zamana dek sürecek?” diye sordu.
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 Kutsal varlık bana, “2 300 akşam, sabah olacak, sonra kutsal yer yeniden düzene konulacak” dedi.
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 Ben Daniel, gördüğüm görümün ne anlama geldiğini çözmeye çalışırken, insana benzer biri karşımda durdu.
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 Bir insan sesinin Ulay Kanalı'ndan, “Ey Cebrail, görümün ne anlama geldiğini şuna açıkla” diye seslendiğini duydum.
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 Cebrail durduğum yere yaklaşınca korkudan yere yığıldım. Bana, “Ey insanoğlu!” dedi, “Bu görümün sonla ilgili olduğunu anla.”
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 O benimle konuşurken, yüzükoyun yere uzanmış, derin bir uykuya dalmışım. Dokunup beni ayağa kaldırdı.
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 Bana, “Daha sonra Tanrı'nın öfkesi sona erdiğinde neler olacağını sana söyleyeceğim” dedi, “Çünkü görüm sonun belirlenen zamanıyla ilgilidir.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 Gördüğün iki boynuzlu koç Med ve Pers krallarını simgeler.
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 Teke Grek Kralı'dır; gözleri arasındaki büyük boynuz birinci kraldır.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 Kırılan boynuzun yerine çıkan dört boynuz, ulusundan çıkacak dört krallığı simgeliyor. Ama ilk kral kadar güçlü olmayacaklar.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 “Bu dört krallığın sonu yaklaşıp yapılan kötülükler doruğa varınca, sert yüzlü ve aldatmada usta bir kral ortaya çıkacak.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 Kendisinden gelmeyen büyük bir güce kavuşacak. Şaşırtıcı yıkımlar yapacak, el attığı her işte başarılı olacak. Güçlüleri ve kutsal halkı yok edecek.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 Yapacağı işleri aldatarak başaracak, kendisini yükseltecek. Güvenlikte olan birçoklarını yok edecek, Önderler Önderi'ne karşı duracak. Ama kendisi insan eli değmeden yok edilecek.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 “Akşam ve sabahla ilgili sana bildirilen görüm gerçektir. Ama sen görümü gizli tut. Çünkü uzak bir gelecekle ilgilidir.”
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 Ben Daniel günlerce bitkin ve hasta kaldım. Sonra kalkıp kralın işlerini yapmayı sürdürdüm. Bu anlaşılması güç görümden ötürü şaşkındım.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >