< 2 Timoteos 2 >

1 Oğlum, Mesih İsa'da olan lütufla güçlen.
Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Birçok tanık önünde benden işittiğin sözleri, başkalarına da öğretmeye yeterli olacak güvenilir kişilere emanet et.
Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
3 Mesih İsa'nın iyi bir askeri olarak benimle birlikte sıkıntıya göğüs ger.
Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
4 Askerlik yapan kişi günlük yaşamla ilgili işlere karışmaz; kendisini askerliğe çağıranı hoşnut etmeye çalışır.
Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
5 Bunun gibi, spor yarışmasına katılan kişi de kurallar uyarınca yarışmazsa zafer tacını giyemez.
Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
6 Emek veren çiftçi üründen ilk payı alan kişi olmalıdır.
Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
7 Dediklerimi iyi düşün. Rab sana her konuda anlayış verecektir.
Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
8 Yaydığım Müjde'de açıklandığı gibi, Davut'un soyundan olup ölümden dirilmiş olan İsa Mesih'i anımsa.
Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
9 Bu Müjde uğruna bir suçlu gibi zincire vurulmaya kadar varan sıkıntılara katlanıyorum. Ama Tanrı'nın sözü zincire vurulmuş değildir.
Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
10 Bunun içindir ki, seçilmişler uğruna her şeye dayanıyorum. Öyle ki, onlar da sonsuz yüceliğin yanısıra Mesih İsa'da olan kurtuluşa kavuşsunlar. (aiōnios g166)
na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele. (aiōnios g166)
11 Şu güvenilir bir sözdür: “O'nunla birlikte öldüysek, O'nunla birlikte yaşayacağız.
Usemi huu ni wa kweli: “Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12 Dayanırsak, O'nunla birlikte egemenlik süreceğiz. O'nu inkâr edersek, O da bizi inkâr edecek.
Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
13 Biz sadık kalmasak da, O sadık kalacak. Çünkü kendi özüne aykırı davranamaz.”
Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe.”
14 Bu konuları imanlılara anımsat. Dinleyenleri felakete sürüklemekten başka yararı olmayan kelime kavgaları çıkarmamaları için onları Tanrı'nın önünde uyar.
Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
15 Kendini Tanrı'ya makbul, gerçeğin bildirisini doğru kullanan, alnı ak bir işçi olarak sunmaya gayret et.
Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
16 Bayağı, boş sözlerden sakın. Çünkü bunlara dalanlar tanrısızlıkta daha da ileri gidecekler.
Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
17 Sözleri kangren gibi yayılacak. Himeneos'la Filitos bunlardandır.
Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
18 Diriliş olup bitti diyerek gerçek yoldan saptılar. Şimdi de bazılarının imanını altüst ediyorlar.
Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
19 Ne var ki, Tanrı'nın attığı sağlam temel, “Rab kendine ait olanları bilir” ve “Rab'bin adını anan herkes kötülükten uzak dursun” sözleriyle mühürlenmiş olarak duruyor.
Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: “Bwana anawafahamu wale walio wake,” na “Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu.”
20 Büyük bir evde yalnız altın ve gümüş kaplar bulunmaz; tahta ve toprak kaplar da vardır. Kimi onurlu, kimi bayağı iş için kullanılır.
Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
21 Bunun gibi, kişi de kendini bayağı işlerden arıtırsa, onurlu amaçlara uygun, kutsal kılınmış, efendisine yararlı, her iyi işe hazır bir kap olur.
Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
22 Gençlik arzularından kaç. Temiz yürekle Rab'be yakaranlarla birlikte doğruluğun, imanın, sevginin ve esenliğin ardından koş.
Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
23 Saçma, cahilce tartışmalara girmeyi reddet. Bunların kavga doğurduğunu bilirsin.
Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
24 Rab'bin kulu kavgacı olmamalı. Tersine, herkese şefkatle davranmalı, öğretme yeteneği olmalı, haksızlıklara sabırla dayanmalıdır.
Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
25 Kendisine karşı olanları yumuşak huyla yola getirmeli. Gerçeği anlamaları için Tanrı belki onlara bir tövbe yolu açar.
ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
26 Böylelikle ayılabilir, isteğini yerine getirmeleri için kendilerini tutsak eden İblis'in tuzağından kurtulabilirler.
Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.

< 2 Timoteos 2 >