< 2 Samuel 20 >

1 O sırada Benyamin oymağından Bikri oğlu Şeva adında kötü bir adam bir rastlantı sonucu Gilgal'daydı. Şeva boru çalıp, “İşay oğlu Davut'la ne ilgimiz Ne de payımız var” dedi, “Ey İsrailliler, herkes kendi evine dönsün!”
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 Bunun üzerine bütün İsrailliler Davut'u bırakıp Bikri oğlu Şeva'nın ardından gitti. Yahudalılar ise krallarına bağlı kalıp Şeria Irmağı'ndan Yeruşalim'e dek ona eşlik ettiler.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 Kral Davut Yeruşalim'deki sarayına varınca, saraya bakmak için bıraktığı on cariyeyi gözetim altına aldı, onların geçimini sağladı. Ancak yataklarına girmedi. Onlar da ölünceye dek göz altında dul kadınlar gibi yaşadılar.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Davut Amasa'ya, “Üç gün içinde Yahudalılar'ı yanıma çağır. Sen de burada ol” dedi.
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 Amasa Yahudalılar'ı çağırmaya gitti. Ama belirlenen zamanda dönmedi.
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 Bunun üzerine Davut Avişay'a, “Şimdi Bikri oğlu Şeva bize Avşalom'dan daha büyük kötülük yapacak” dedi, “Efendinin adamlarını al ve onu kovala. Yoksa kendine surlu kentler bulup bizden kaçar.”
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Böylece Yoav'ın adamları, Keretliler'le Peletliler ve bütün koruyucular Bikri oğlu Şeva'yı kovalamak için Avişay'ın komutasında Yeruşalim'den çıktılar.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 Givon'daki büyük kayanın yanına varınca, Amasa onları karşılamaya geldi. Yoav savaş giysisini giymişti. Giysinin üzerine bir kemer kuşanmış, kemere kınında duran bir kılıç bağlamıştı. Yoav ilerlerken kılıç kınından çıktı.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 Yoav Amasa'ya, “İyi misin, kardeşim?” diye sordu. Onu öpmek için sağ eliyle Amasa'nın sakalından tuttu.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Amasa Yoav'ın elindeki kılıcı farketmedi. Yoav kılıcı karnına saplayınca, Amasa'nın bağırsakları yere döküldü. İkinci vuruşa gerek kalmadan Amasa öldü. Bundan sonra Yoav'la kardeşi Avişay, Bikri oğlu Şeva'yı kovalamayı sürdürdüler.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 Yoav'ın adamlarından biri, Amasa'nın ölüsü yanında durup, “Yoav'ı tutan ve Davut'tan yana olan herkes Yoav'ın ardından gitsin” dedi.
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Amasa'nın ölüsü yolun ortasında kanlar içinde duruyordu. Yoav'ın adamı, ölüye yaklaşan herkesin orada durduğunu görünce, Amasa'yı yoldan sürükleyip tarlaya götürdü ve üzerine bir örtü attı.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 Ölü yoldan kaldırıldıktan sonra herkes Bikri oğlu Şeva'yı kovalamak için Yoav'ın ardından gitti.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Şeva bütün İsrail oymaklarından ve Berliler'in bölgesinden geçip Avel-Beytmaaka'ya geldi. Berliler de toplanıp onu izleyerek kente girdiler.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 Yoav'la bütün adamları varıp Avel-Beytmaaka Kenti'nde Şeva'yı kuşattılar. Topraktan kentin suruna bitişik bir yığın yaptılar ve suru devirmek için yıkmaya başladılar.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 O sırada bilge bir kadın kentin içinden seslendi: “Dinleyin! Dinleyin! Yoav'a buraya gelmesini söyleyin, onunla konuşacağım.”
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 Yoav kadına yaklaştı. Kadın, “Yoav sen misin?” diye sordu. Yoav, “Benim” diye yanıtladı. Kadın, “Kölenin sözlerini dinle” dedi. Yoav, “Dinliyorum” dedi.
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 Kadın konuşmasını şöyle sürdürdü: “Eskiden, ‘Avel Kenti'ne danışın’ derlerdi ve sorunları böyle çözerlerdi.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Biz İsrail'in esenliğini isteyen güvenilir kişileriz. Sense İsrail'e ana gibi kucak açan kentlerden birini yıkmaya çalışıyorsun. Neden RAB'bin halkını yok etmek istiyorsun?”
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 Yoav, “Asla!” diye yanıtladı, “Ne yıkmak, ne de yok etmek istiyorum.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 Durum öyle değil. Efrayim dağlık bölgesinden Bikri oğlu Şeva adındaki adam Kral Davut'a başkaldırdı. Yalnız onu verin, ben de kentten geri çekileyim.” Kadın, “Onun başı surun üzerinden sana atılacak” dedi.
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 Sonra kadın bilgece öğüdüyle bütün halka gitti. Halk Bikri oğlu Şeva'nın başını kesip Yoav'a attı. Bunun üzerine Yoav boru çaldı. Adamları kenti bırakıp evlerine gittiler. Yoav da Yeruşalim'e, kralın yanına döndü.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 Yoav İsrail ordusunun komutanıydı. Yehoyada oğlu Benaya ise Keretliler'le Peletliler'in komutanıydı.
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 Adoram angaryasına çalışanlardan sorumluydu. Ahilut oğlu Yehoşafat devlet tarihçisiydi.
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 Şeva yazman, Sadok'la Aviyatar kâhindi.
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 Yairli İra ise Davut'un kâhiniydi.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

< 2 Samuel 20 >