< 2 Samuel 15 >

1 Bundan sonra Avşalom kendisine bir savaş arabası, atlar ve önünde koşacak elli kişi hazırladı.
Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
2 Sabah erkenden kalkıp kent kapısına giden yolun kenarında dururdu. Davasına baktırmak için krala gelen herkese seslenip, “Nerelisin?” diye sorardı. Adam hangi İsrail oymağından geldiğini söylerdi.
Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
3 Avşalom ona şöyle derdi: “Bak, ileri sürdüğün savlar doğru ve haklı. Ne var ki, kral adına seni dinleyecek kimse yok.”
Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
4 Sonra konuşmasını şöyle sürdürürdü: “Keşke kral beni ülkeye yargıç atasa! Davası ya da sorunu olan herkes bana gelse, ben de ona hakkını versem!”
Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
5 Biri önünde yüzüstü yere kapanmak üzere yaklaştı mı, Avşalom elini uzatıp adamı tutar, öperdi.
Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
6 Davasına baktırmak için krala gelen İsrailliler'in hepsine böyle davrandı. Böylelikle İsrailliler'in gönlünü çeldi.
Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
7 Dört yıl sonra Avşalom krala, “İzin ver de Hevron'a gidip RAB'be adağımı yerine getireyim” dedi,
Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
8 “Çünkü ben kulun Aram'ın Geşur Kenti'nde yaşarken, ‘RAB beni Yeruşalim'e geri getirirse, O'na Hevron'da tapınacağım’ diye adak adamıştım.”
Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
9 Kral, “Esenlikle git” dedi. Ne var ki, Hevron'a giden Avşalom bütün İsrail oymaklarına gizlice ulaklar göndererek şöyle dedi: “Boru sesini duyar duymaz, ‘Avşalom Hevron'da kral oldu’ diyeceksiniz.”
Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
11 Yeruşalim'den çağrılan iki yüz kişi olup bitenden haberleri olmaksızın, iyi niyetle Avşalom'la birlikte gittiler.
Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
12 Avşalom kurbanları keserken, Davut'un danışmanı Gilolu Ahitofel'i de Gilo Kenti'nden getirtti. Böylece ayaklanma güç kazandı. Çünkü Avşalom'u izleyen halkın sayısı giderek çoğalıyordu.
Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
13 Bir ulak gelip Davut'a, “İsrailliler Avşalom'a yürekten bağlandı” dedi.
Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
14 Bunun üzerine Davut Yeruşalim'de kendisiyle birlikte olan bütün görevlilerine şöyle dedi: “Haydi kaçalım! Yoksa Avşalom'dan kaçıp kurtulamayacağız. Hemen gidelim! Yoksa Avşalom ardımızdan çabucak yetişip bizi yıkıma uğratır. Kenti de kılıçtan geçirir.”
Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
15 Kralın görevlileri, “Efendimiz kral ne karar verirse yapmaya hazırız” diye yanıtladılar.
Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
16 Böylece kral ardısıra gelen bütün ev halkıyla birlikte yola koyuldu. Ancak saraya baksınlar diye on cariyesini orada bıraktı.
Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
17 Kralla yanındakiler kentin en son evinde durdular.
Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
18 Bütün kulları, Keretliler'le Peletliler kralın yanından geçtiler. Gat'tan ardısıra gelmiş olan altı yüz Gatlı asker de kralın önünden geçti.
Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
19 Kral Gatlı İttay'a, “Neden sen de bizimle geliyorsun?” dedi, “Geri dön ve yeni kralla kal. Çünkü sen yurdundan sürülmüş bir yabancısın.
Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
20 Daha dün geldin. Bugün nereye gideceğimi kendim bilmezken, seni de bizimle birlikte mi dolaştırayım? Kardeşlerinle birlikte geri dön. Tanrı'nın sevgisi ve sadakati üzerinde olsun!”
Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
21 Ama İttay şöyle yanıtladı: “Efendim kral, yaşayan RAB'bin adıyla ve yaşamın hakkı için derim ki, ister yaşam, ister ölüm için olsun, sen neredeysen kulun ben de orada olacağım.”
Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
22 Davut İttay'a, “Yürü, geç!” dedi. Böylece Gatlı İttay yanındaki bütün adamları ve çocuklarıyla birlikte geçti.
Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
23 Halk geçerken, bütün yöre halkı hıçkıra hıçkıra ağlıyordu. Kral Kidron Vadisi'ni geçti. Halk da kırlara doğru ilerledi.
Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
24 Kâhin Sadok'la Tanrı'nın Antlaşma Sandığı'nı taşıyan Levililer de oradaydı. Tanrı'nın Sandığı'nı yere koydular. Bütün halk kentten çıkana dek Aviyatar sunular sundu.
Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
25 Sonra kral, Sadok'a, “Tanrı'nın Sandığı'nı kente geri götür” dedi, “RAB benden hoşnut kalırsa, beni geri getirir, sandığı ve konduğu yeri bana gösterir.
Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
26 Ama, ‘Senden hoşnut değilim’ derse, işte buradayım, bana uygun gördüğünü yapsın.”
Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
27 Kral Kâhin Sadok'la konuşmasını şöyle sürdürdü: “Sen bilici değil misin? Oğlun Ahimaas'ı ve Aviyatar oğlu Yonatan'ı yanına al; Aviyatar'la birlikte esenlikle kente dönün.
Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
28 Sizden aydınlatıcı bir haber alana dek ben kırda, ırmağın sığ yerinde bekleyeceğim.”
Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
29 Böylece Sadok'la Aviyatar Tanrı'nın Sandığı'nı Yeruşalim'e geri götürüp orada kaldılar.
Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
30 Davut ağlaya ağlaya Zeytin Dağı'na çıkıyordu. Başı örtülüydü, yalınayak yürüyordu. Yanındaki herkesin başı örtülüydü ve ağlayarak dağa çıkıyorlardı.
Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
31 O sırada biri Davut'a, “Ahitofel Avşalom'dan yana olan suikastçıların arasında” diye bildirdi. Bunun üzerine Davut, “Ya RAB, Ahitofel'in öğüdünü boşa çıkar” diye dua etti.
Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
32 Davut Tanrı'ya tapılan tepenin doruğuna varınca, Arklı Huşay giysisi yırtılmış, başı toz toprak içinde onu karşıladı.
Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
33 Davut ona, “Benimle birlikte gelirsen, bana yük olursun” dedi,
Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
34 “Ama kente döner ve Avşalom'a, ‘Ey kral, senin kulun olacağım; geçmişte babana nasıl kulluk ettiysem, şimdi de sana öyle kulluk edeceğim’ dersen, Ahitofel'in öğüdünü benim için boşa çıkarırsın.
Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
35 Kâhin Sadok ile Kâhin Aviyatar orada seninle birlikte olacaklar. Kralın sarayında duyduğun her şeyi onlara bildir.
Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
36 Sadok oğlu Ahimaas ile Aviyatar oğlu Yonatan da oradalar. Bütün duyduklarınızı onların aracılığıyla bana iletebilirsiniz.”
Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
37 Böylece Davut'un dostu Huşay Yeruşalim'e gitti. Tam o sırada Avşalom da kente giriyordu.
Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.

< 2 Samuel 15 >