< 2 Krallar 19 >

1 Kral Hizkiya olanları duyunca giysilerini yırttı, çul kuşanıp RAB'bin Tapınağı'na girdi.
Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
2 Saray sorumlusu Elyakim'i, Yazman Şevna'yı ve ileri gelen kâhinleri Amots oğlu Peygamber Yeşaya'ya gönderdi. Hepsi çul kuşanmıştı.
Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
3 Yeşaya'ya şöyle dediler: “Hizkiya diyor ki, ‘Bugün sıkıntı, azar ve utanç günü. Çünkü çocukların doğum vakti geldi, ama doğuracak güç yok.
Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
4 Yaşayan Tanrı'yı aşağılamak için efendisi Asur Kralı'nın gönderdiği komutanın söylediklerini belki Tanrın RAB duyar da duyduğu sözlerden ötürü onları cezalandırır. Bu nedenle sağ kalanlarımız için dua et.’”
Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
5 Yeşaya, Kral Hizkiya'dan gelen görevlilere şöyle dedi: “Efendinize şunları söyleyin: ‘RAB diyor ki, Asur Kralı'nın adamlarından benimle ilgili duyduğunuz küfürlerden korkma.
Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
6
Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
7 Onun içine öyle bir ruh koyacağım ki, bir haber üzerine kendi ülkesine dönecek. Orada onu kılıçla öldürteceğim.’”
Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
8 Komutan, Asur Kralı'nın Lakiş'ten ayrılıp Livna'ya karşı savaştığını duydu. Krala danışmak için oraya gitti.
Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
9 Kûş Kralı Tirhaka'nın kendisiyle savaşmak üzere yola çıktığını haber alan Asur Kralı, Hizkiya'ya yine ulaklar göndererek şöyle dedi:
Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
10 “Yahuda Kralı Hizkiya'ya deyin ki, ‘Güvendiğin Tanrın, Yeruşalim Asur Kralı'nın eline teslim edilmeyecek diyerek seni aldatmasın.
“Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
11 Asur krallarının bütün ülkelere neler yaptığını, onları nasıl yerle bir ettiğini duymuşsundur. Sen kurtulacağını mı sanıyorsun?
Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
12 Atalarımın yok ettiği ulusları –Gozanlılar'ı, Harranlılar'ı, Resefliler'i, Telassar'da yaşayan Edenliler'i– ilahları kurtarabildi mi?
Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
13 Hani nerede Hama ve Arpat kralları? Lair, Sefarvayim, Hena, İvva kralları nerede?’”
Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
14 Hizkiya mektubu ulakların elinden alıp okuduktan sonra RAB'bin Tapınağı'na çıktı. RAB'bin önünde mektubu yere yayarak
Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
15 şöyle dua etti: “Ey Keruvlar arasında taht kuran İsrail'in Tanrısı RAB, bütün dünya krallıklarının tek Tanrısı sensin. Yeri, göğü sen yarattın.
Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
16 Ya RAB, kulak ver de işit, gözlerini aç da gör, ya RAB; Sanherib'in söylediklerini, yaşayan Tanrı'yı nasıl aşağıladığını duy.
Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
17 Ya RAB, gerçek şu ki, Asur kralları birçok ulusu ve ülkelerini viraneye çevirdiler.
“Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao.
18 İlahlarını yakıp yok ettiler. Çünkü onlar tanrı değil, insan eliyle biçimlendirilmiş tahta ve taşlardı.
Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
19 Ya RAB Tanrımız, şimdi bizi Sanherib'in elinden kurtar ki, bütün dünya krallıkları senin tek Tanrı olduğunu anlasın.”
Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
20 Bunun üzerine Amots oğlu Yeşaya, Hizkiya'ya şu haberi gönderdi: “İsrail'in Tanrısı RAB şöyle diyor: ‘Asur Kralı Sanherib'le ilgili olarak bana yalvardığın için diyorum ki, “‘Erden kız Siyon seni hor görüyor, Alay ediyor seninle. Yeruşalim kızı ardından alayla baş sallıyor.
Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru.
Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
22 Sen kimi aşağıladın, kime küfrettin? Kime sesini yükselttin? İsrail'in Kutsalı'na tepeden baktın!
Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
23 Ulakların aracılığıyla Rab'bi aşağıladın. Bir sürü savaş arabamla dağların tepesine, Lübnan'ın doruklarına çıktım, dedin. Yüksek sedir ağaçlarını, seçme çamlarını kestim, Lübnan'ın en iç noktalarına, Gür ormanlarına ulaştım.
Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
24 Yabancı ülkelerde kuyular kazdım, sular içtim, Mısır'ın bütün kanallarını ayağımın tabanıyla kuruttum, dedin.
Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.”
25 “‘Bütün bunları çoktan yaptığımı, Çok önceden tasarladığımı duymadın mı? Surlu kentleri enkaz yığınlarına çevirmeni Şimdi ben gerçekleştirdim.
“‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
26 O kentlerde yaşayanların kolu kanadı kırıldı. Yılgınlık ve utanç içindeydiler; Kır otuna, körpe filizlere, Damlarda büyümeden kavrulup giden ota döndüler.
Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
27 Senin oturuşunu, kalkışını, Ne zaman gidip geldiğini, Bana nasıl öfkelendiğini biliyorum.
“‘Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
28 Bana duyduğun öfkeden, Kulağıma erişen küstahlığından ötürü Halkamı burnuna, gemimi ağzına takacak, Seni geldiğin yoldan geri çevireceğim.
Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu, na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’
29 “‘Senin için belirti şu olacak, ey Hizkiya: Bu yıl kendiliğinden yetişeni yiyeceksiniz, İkinci yıl ise ardından biteni. Üçüncü yıl ekip biçin, Bağlar dikip ürününü yiyin.
“Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
30 Yahudalılar'ın kurtulup sağ kalanları Yine aşağıya doğru kök salacak, Yukarıya doğru meyve verecek.
Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
31 Çünkü sağ kalanlar Yeruşalim'den, Kurtulanlar Siyon Dağı'ndan çıkacak. Her Şeye Egemen RAB'bin gayretiyle olacak bu.’
Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.
32 “Bundan dolayı RAB Asur Kralı'na ilişkin şöyle diyor: ‘Bu kente girmeyecek, ok atmayacak. Kente kalkanla yaklaşmayacak, Karşısında rampa kurmayacak.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kupanga majeshi kuuzingira.
33 Geldiği yoldan dönecek ve kente girmeyecek’ diyor RAB,
Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu, asema Bwana.
34 ‘Kendim için ve kulum Davut'un hatırı için Bu kenti savunup kurtaracağım’ diyor.”
Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”
35 O gece RAB'bin meleği gidip Asur ordugahında yüz seksen beş bin kişiyi öldürdü. Ertesi sabah uyananlar salt cesetlerle karşılaştılar.
Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
36 Bunun üzerine Asur Kralı Sanherib ordugahını bırakıp çekildi. Ninova'ya döndü ve orada kaldı.
Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
37 Bir gün ilahı Nisrok'un tapınağında tapınırken, oğullarından Adrammelek'le Şareser, onu kılıçla öldürüp Ararat ülkesine kaçtılar. Yerine oğlu Esarhaddon kral oldu.
Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.

< 2 Krallar 19 >