< 2 Krallar 17 >

1 Yahuda Kralı Ahaz'ın krallığının on ikinci yılında Ela oğlu Hoşea Samiriye'de İsrail Kralı oldu ve dokuz yıl krallık yaptı.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
2 RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı, ama kendisinden önceki İsrail kralları kadar kötü değildi.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
3 Asur Kralı Şalmaneser Hoşea'ya savaş açtı. Hoşea teslim olup haraç ödemeye başladı.
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
4 Ancak Asur Kralı Hoşea'nın hainlik yaptığını öğrendi. Çünkü Hoşea Mısır Firavunu So'nun desteğini sağlamak için ona ulaklar göndermiş, üstelik her yıl ödemesi gereken haraçları da Asur Kralı'na ödememişti. Bunun üzerine Asur Kralı onu yakalayıp cezaevine kapadı.
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
5 Asur Kralı İsrail topraklarına saldırdı. Samiriye'yi kuşattı. Kuşatma üç yıl sürdü.
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
6 Hoşea'nın krallığının dokuzuncu yılında Asur Kralı Samiriye'yi ele geçirdi. İsrail halkını Asur'a sürdü. Onları Halah'a, Habur Irmağı kıyısındaki Gozan'a ve Med kentlerine yerleştirdi.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
7 Bütün bunlar kendilerini Mısır Firavunu'nun boyunduruğundan kurtarıp Mısır'dan çıkaran Tanrıları RAB'be karşı günah işledikleri için İsrailliler'in başına geldi. Çünkü başka ilahlara tapmışlar,
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
8 RAB'bin İsrail halkının önünden kovmuş olduğu ulusların törelerine ve İsrail krallarının koyduğu kurallara göre yaşamışlardı.
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
9 Tanrıları RAB'bin onaylamadığı bu işleri gizlilik içinde yapmışlar, gözcü kulelerinden surlu kentlere kadar her yerde tapınma yerleri kurmuşlardı.
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
10 Her yüksek tepenin üzerine, bol yapraklı her ağacın altına dikili taşlar, Aşera putları diktiler.
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
11 RAB'bin onların önünden kovmuş olduğu ulusların yaptığı gibi, bütün tapınma yerlerinde buhur yaktılar. Yaptıkları kötülüklerle RAB'bi öfkelendirdiler.
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
12 RAB'bin, “Bunu yapmayacaksınız” demiş olmasına karşın putlara taptılar.
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
13 RAB İsrail ve Yahuda halkını bütün peygamberler ve biliciler aracılığıyla uyarmış, onlara, “Bu kötü yollarınızdan dönün” demişti, “Atalarınıza buyurduğum ve kullarım peygamberler aracılığıyla size gönderdiğim Kutsal Yasa'nın tümüne uyarak buyruklarımı, kurallarımı yerine getirin.”
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14 Ama dinlemediler, Tanrıları RAB'be güvenmeyen ataları gibi inat ettiler.
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
15 Tanrı'nın kurallarını, uyarılarını ve atalarıyla yaptığı antlaşmayı hiçe sayarak değersiz putların ardınca gittiler, böylece kendi değerlerini de yitirdiler. Çevrelerindeki uluslar gibi yaşamamaları için RAB kendilerine buyruk verdiği halde, ulusların törelerine göre yaşadılar.
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
16 Tanrıları RAB'bin bütün buyruklarını terk ettiler. Tapınmak için kendilerine iki dökme buzağı ve Aşera putu yaptırdılar. Gök cisimlerine taptılar. Baal'a kulluk ettiler.
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
17 Oğullarını, kızlarını ateşte kurban ettiler. Falcılık, büyücülük yaptılar. RAB'bin gözünde kötü olanı yaptılar, kendilerini kötülüğe adayarak O'nu öfkelendirdiler.
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
18 RAB İsrailliler'e çok kızdı, Yahuda oymağı dışında hepsini huzurundan kovdu.
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
19 Yahudalılar bile Tanrıları RAB'bin buyruklarına uymadılar. İsrailliler'in benimsediği törelere göre yaşadılar.
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
20 Bundan dolayı RAB İsrail soyundan olan herkesi reddetti. Çapulcuların eline teslim ederek onları cezalandırdı. Hepsini huzurundan kovdu.
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
21 RAB İsrail'i Davut soyunun elinden aldıktan sonra, İsrailliler Nevat oğlu Yarovam'ı kral yaptılar. Yarovam İsrailliler'i RAB'bin yolundan saptırarak büyük günaha sürükledi.
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
22 İsrailliler Yarovam'ın işlediği bütün günahlara katıldılar ve bunlardan ayrılmadılar.
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
23 Sonunda RAB kulları peygamberler aracılığıyla uyarmış olduğu gibi, onları huzurundan kovdu. İsrailliler kendi topraklarından Asur'a sürüldüler. Bugün de orada yaşıyorlar.
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
24 Asur Kralı İsrailliler'in yerine Babil, Kuta, Avva, Hama ve Sefarvayim'den insanlar getirtip Samiriye kentlerine yerleştirdi. Bunlar Samiriye'yi mülk edinip oradaki kentlerde yaşamaya başladılar.
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
25 Oralara ilk yerleştiklerinde RAB'be tapınmadılar. Bu yüzden RAB aslanlar göndererek bazılarını öldürttü.
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
26 Asur Kralı'na, “Sürdüğün ve Samiriye kentlerine yerleştirdiğin uluslar Samiriye ilahının yasasını bilmiyorlar. O da üzerlerine aslanlar gönderiyor” diye haber salındı, “Bu yüzden aslanlara yem oluyorlar. Çünkü ülke ilahının yasasından haberleri yok.”
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
27 Bunun üzerine Asur Kralı şu buyruğu verdi: “Samiriye'den sürülen kâhinlerden birini geri gönderin, gidip orada yaşasın ve ülke ilahının yasasını onlara öğretsin.”
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
28 Samiriye'den sürülen kâhinlerden biri gelip Beytel'e yerleşti ve RAB'be nasıl tapınacaklarını onlara öğretmeye başladı.
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
29 Gelgelelim Samiriye kentlerine yerleşen her ulus kendi ilahlarını yaptı. Samiriyeliler'in yapmış olduğu tapınma yerlerindeki yapılara bu ilahları koydular.
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
30 Babil halkı Sukkot-Benot, Kuta halkı Nergal, Hama halkı Aşima,
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
31 Avva halkı ise Nivhaz ve Tartak adındaki ilahlarını yaptılar. Sefarvayim halkı ise oğullarını ilahları Adrammelek ve Anammelek'e yakarak kurban ettiler.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
32 Bir yandan RAB'be tapınıyor, öte yandan tapınma yerlerindeki yapılarda görev yapmak üzere aralarından rasgele kâhinler seçiyorlardı.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
33 Böylece hem RAB'be tapınıyorlar, hem de aralarından geldikleri ulusların törelerine göre kendi ilahlarına kulluk ediyorlardı.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
34 Bugün de eski törelerine göre yaşıyorlar. Ne RAB'be tapınıyorlar, ne de RAB'bin İsrail adını verdiği Yakup'un oğulları için koymuş olduğu kurallara, ilkelere, yasalara, buyruklara uyuyorlar.
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
35 RAB Yakupoğulları'yla antlaşma yapmış ve onlara şöyle buyurmuştu: “Başka ilahlara tapmayacak, önlerinde eğilmeyecek, onlara kulluk etmeyecek, kurban kesmeyeceksiniz.
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
36 Yalnızca ulu gücüyle her yere erişen eliyle sizleri Mısır'dan çıkaran RAB'be tapınacaksınız. O'nun önünde eğilip O'na kurban keseceksiniz.
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
37 Sizler için yazmış olduğu kuralları, ilkeleri, yasaları, buyrukları her zaman yerine getirmeye özen gösterecek ve başka ilahlara tapmayacaksınız.
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
38 Sizinle yaptığım antlaşmayı unutmayacak ve başka ilahlara tapmayacaksınız.
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
39 Yalnız Tanrınız RAB'be tapacaksınız. O sizi bütün düşmanlarınızın elinden kurtaracak.”
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
40 Ne var ki Samiriye'ye yerleşenler buna kulak asmadılar ve eski törelerine göre yaşamaya devam ettiler.
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
41 Bu uluslar aynı zamanda hem RAB'be, hem de putlarına tapıyorlardı. Çocukları ve torunları da bugüne dek ataları gibi yaşıyorlar.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.

< 2 Krallar 17 >