< 2 Krallar 13 >

1 Yahuda Kralı Ahazya oğlu Yoaş'ın krallığının yirmi üçüncü yılında Yehu oğlu Yehoahaz Samiriye'de İsrail Kralı oldu ve on yedi yıl krallık yaptı.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
2 Yehoahaz RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı ve Nevat oğlu Yarovam'ın İsrail'i sürüklediği günahlara katıldı. Bu günahlardan ayrılmadı.
Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
3 İşte bu yüzden RAB'bin İsrail'e karşı öfkesi alevlendi ve RAB onları uzun süre Aram Kralı Hazael'le oğlu Ben-Hadat'ın egemenliği altına soktu.
Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
4 Bunun üzerine Yehoahaz RAB'be yakardı. RAB onun yakarışını kabul etti. Çünkü İsrail'in çektiği sıkıntıyı, Aram Kralı'nın onlara neler yaptığını görüyordu.
Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
5 RAB İsrail'e bir kurtarıcı gönderdi. Böylece halk Aramlılar'ın egemenliğinden kurtuldu ve önceki gibi evlerinde yaşamaya başladı.
Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
6 Ne var ki Yarovam ailesinin İsrail'i sürüklediği günahları izlediler, bu günahlardan ayrılmadılar. Aşera putu da Samiriye'de dikili kaldı.
Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
7 Yehoahaz'ın elli atlı, on savaş arabası, on bin de yaya asker dışında gücü kalmamıştı. Çünkü Aram Kralı ötekileri harman tozu gibi ezip yok etmişti.
Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
8 Yehoahaz'ın krallığı dönemindeki öteki olaylar, bütün yaptıkları ve başarıları İsrail krallarının tarihinde yazılıdır.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
9 Yehoahaz ölüp atalarına kavuşunca, Samiriye'de gömüldü ve yerine oğlu Yehoaş kral oldu.
Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 Yahuda Kralı Yoaş'ın krallığının otuz yedinci yılında Yehoahaz oğlu Yehoaş Samiriye'de İsrail Kralı oldu ve on altı yıl krallık yaptı.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
11 RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı ve Nevat oğlu Yarovam'ın İsrail'i sürüklediği günahlardan ayrılmadı; onun yolunu izledi.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
12 Yehoaş'ın krallığı dönemindeki öteki olaylar, bütün yaptıkları, Yahuda Kralı Amatsya ile savaşırken gösterdiği başarılar İsrail krallarının tarihinde yazılıdır.
Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
13 Yehoaş ölüp atalarına kavuşunca, Samiriye'de İsrail krallarının yanına gömüldü ve tahtına Yarovam geçti.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
14 Elişa ölümcül bir hastalığa yakalandı. İsrail Kralı Yehoaş gidip onu ziyaret etti, “Baba, baba, İsrail'in arabası ve atlıları!” diyerek ağladı.
Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
15 Elişa ona, “Bir yayla birkaç ok al” dedi. Kral yayla okları aldı.
Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
16 Elişa, “Yayı hazırla” dedi. Kral yayı hazırlayınca, Elişa ellerini kralın elleri üzerine koydu.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
17 “Doğuya bakan pencereyi aç” dedi. Kral pencereyi açtı. Elişa, “Oku at!” dedi. Kral oku atınca, Elişa, “Bu ok Aramlılar'a karşı sizi zafere ulaştıracak RAB'bin kurtarış okudur” dedi, “Afek'te onları kesin bozguna uğratacaksınız.”
Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
18 Sonra, “Öbür okları al” dedi. İsrail Kralı okları alınca, Elişa, “Onları yere vur” dedi. Kral okları üç kez yere vurdu ve durdu.
Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
19 Buna öfkelenen Tanrı adamı Elişa, “Beş altı kez vurmalıydın, o zaman Aramlılar'a karşı kesin bir zafer kazanırdın” dedi, “Ama şimdi Aramlılar'ı ancak üç kez bozguna uğratacaksın.”
Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
20 Elişa öldü ve gömüldü. Her ilkbaharda Moav akıncıları İsrail topraklarına girerlerdi.
Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
21 Bir keresinde İsrailliler, ölü gömerken akıncıların geldiğini görünce, ölüyü Elişa'nın mezarına atıp kaçtılar. Ölü Elişa'nın kemiklerine dokununca dirilip ayağa kalktı.
Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 Aram Kralı Hazael Yehoahaz'ın krallığı boyunca İsrailliler'e baskı yaptı.
Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
23 Ama RAB, İbrahim, İshak ve Yakup'la yaptığı antlaşmadan ötürü, İsrailliler'e iyilik etti. Onlara acıyıp yardım etti. Yok olmalarına izin vermedi. Onları şimdiye kadar huzurundan atmadı.
Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
24 Aram Kralı Hazael ölünce yerine oğlu Ben-Hadat kral oldu.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Bunun üzerine İsrail Kralı Yehoaş, babası Yehoahaz'ın krallığı döneminde Hazael oğlu Ben-Hadat'ın savaşta ele geçirmiş olduğu kentleri geri aldı. Onu üç kez bozguna uğratıp İsrail kentlerine yeniden sahip oldu.
Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.

< 2 Krallar 13 >