< 2 Tarihler 9 >

1 Saba Kraliçesi, Süleyman'ın ününü duyunca, onu çetin sorularla sınamak için Yeruşalim'e geldi. Çeşitli baharat, çok miktarda altın ve değerli taşlarla yüklü büyük bir kervan eşliğinde gelen kraliçe, aklından geçen her şeyi Süleyman'la konuştu.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Süleyman onun bütün sorularına karşılık verdi. Kralın ona yanıt bulmakta güçlük çektiği hiçbir konu olmadı.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 Süleyman'ın bilgeliğini, yaptırdığı sarayı, sofrasının zenginliğini, görevlilerinin oturup kalkışını, hizmetkârlarının ve sakilerinin özel giysileriyle yaptığı hizmeti, RAB'bin Tapınağı'nda sunduğu yakmalık sunuları gören Saba Kraliçesi hayranlık içinde kaldı.
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 Krala, “Ülkemdeyken, yaptıklarınla ve bilgeliğinle ilgili duyduklarım doğruymuş” dedi,
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 “Ama gelip kendi gözlerimle görünceye dek anlatılanlara inanmamıştım. Büyük bilgeliğinin yarısı bile bana anlatılmadı. Duyduklarımdan daha üstünsün.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 Ne mutlu adamlarına! Ne mutlu sana hizmet eden görevlilere! Çünkü sürekli bilgeliğine tanık oluyorlar.
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Senden hoşnut kalan, adına egemenlik sürmen için seni tahta oturtan Tanrın RAB'be övgüler olsun! Tanrın İsrail'i sevdiği, sonsuza dek korumak istediği için, adaleti ve doğruluğu sağlaman için seni İsrail'e kral yaptı.”
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Saba Kraliçesi krala 120 talant altın, çok büyük miktarda baharat ve değerli taşlar armağan etti. Krala armağan ettiği baharatın benzeri yoktu.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 Bu arada Hiram'ın adamlarıyla Süleyman'ın adamları Ofir'den altın, algum kerestesiyle değerli taşlar getirdiler.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
11 Kral, RAB'bin Tapınağı'yla sarayın basamaklarını, çalgıcıların lirleriyle çenklerini bu algum kerestesinden yaptırdı. Yahuda bölgesinde daha önce böylesi görülmemişti.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
12 Kral Süleyman Saba Kraliçesi'nin her isteğini, her dileğini yerine getirdi. Kraliçenin kendisine getirdiklerinden daha fazlasını ona verdi. Bundan sonra kraliçe adamlarıyla birlikte oradan ayrılıp kendi ülkesine döndü.
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Süleyman'a bir yılda gelen altının miktarı 666 talantı buluyordu.
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 Tüccarların ve alım satımla uğraşanların getirdiği altın bunun dışındaydı. Arabistan'ın bütün krallarıyla İsrail valileri de Süleyman'a altın, gümüş getiriyorlardı.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 Kral Süleyman dövme altından her biri altı yüz şekel ağırlığında iki yüz büyük kalkan yaptırdı.
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 Ayrıca her biri üç yüz şekel ağırlığında dövme altından üç yüz küçük kalkan yaptırdı. Kral bu kalkanları Lübnan Ormanı adındaki saraya koydu.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 Kral fildişinden büyük bir taht yaptırıp saf altınla kaplattı.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 Tahtın altı basamağı, bir de altın ayak taburesi vardı. Bunlar tahta bağlıydı. Oturulan yerin iki yanında kollar, her kolun yanında birer aslan heykeli bulunuyordu.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 Altı basamağın iki yanında on iki aslan heykeli vardı. Hiçbir krallıkta böylesi yapılmamıştı.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 Kral Süleyman'ın kadehleriyle Lübnan Ormanı adındaki sarayın bütün eşyaları saf altından yapılmış, hiç gümüş kullanılmamıştı. Çünkü Süleyman'ın döneminde gümüşün değeri yoktu.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 Kralın gemileri Hiram'ın adamlarının yönetiminde Tarşiş'e giderdi. Bu gemiler üç yılda bir altın, gümüş, fildişi ve türlü maymunlarla yüklü olarak dönerlerdi.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 Kral Süleyman dünyanın bütün krallarından daha zengin, daha bilgeydi.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Tanrı'nın Süleyman'a verdiği bilgeliği dinlemek için dünyanın bütün kralları onu görmek isterlerdi.
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 Onu görmeye gelenler her yıl armağan olarak altın ve gümüş eşya, giysi, silah, baharat, at, katır getirirlerdi.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Süleyman'ın atlarla savaş arabaları için dört bin ahırı, on iki bin atlısı vardı. Bunların bir kısmını savaş arabaları için ayrılan kentlere, bir kısmını da kendi yanına, Yeruşalim'e yerleştirdi.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Fırat Irmağı'ndan Filist bölgesine, oradan da Mısır sınırına dek uzanan bölgedeki bütün krallara egemendi.
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 Onun krallığı döneminde Yeruşalim'de gümüş taş değerine düştü. Sedir ağaçları Şefela'daki yabanıl incir ağaçları kadar bollaştı.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Süleyman'ın atları Mısır'dan ve bütün öbür ülkelerden getirilirdi.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Süleyman'ın yaptığı öbür işler, başından sonuna dek, Peygamber Natan'ın tarihinde, Şilolu Ahiya'nın peygamberlik yazılarında ve Bilici İddo'nun Nevat oğlu Yarovam'a ilişkin görümlerinde yazılıdır.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Süleyman kırk yıl süreyle bütün İsrail'i Yeruşalim'den yönetti.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Süleyman ölüp atalarına kavuşunca babası Davut'un Kenti'nde gömüldü. Yerine oğlu Rehavam kral oldu.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Tarihler 9 >