< 2 Tarihler 4 >

1 Süleyman tunçtan bir sunak yaptırdı. Sunağın eniyle uzunluğu yirmişer arşın, yüksekliği on arşındı.
Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
2 Dökme tunçtan on arşın çapında, beş arşın derinliğinde, çevresi otuz arşın yuvarlak bir havuz yaptırdı.
Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
3 Havuzun dışı boğa kabartmalarıyla kuşatılmıştı. Her arşında onar tane olan bu kabartmalar iki sıra halindeydi ve gövdeyle birlikte dökülmüştü.
Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 Havuz üçü kuzeye, üçü batıya, üçü güneye, üçü de doğuya bakan on iki boğa heykeli üzerine oturtulmuştu. Boğaların sağrıları içe dönüktü.
Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
5 Havuzun çeperi dört parmak kalınlığındaydı; kenarları kâse kenarlarını, nilüferleri andırıyordu. Üç bin bat su alıyordu.
Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
6 Süleyman yıkama işleri için on kazan yaptırdı. Beşini sunağın güneyine, beşini kuzeyine yerleştirdi. Yakmalık sunuların parçaları bunlarda yıkanırdı. Havuz ise kâhinlerin yıkanması içindi.
Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
7 Süleyman tanıma uygun biçimde yaptırdığı on altın kandilliği tapınağın içine, beşi sağda, beşi solda olmak üzere yerleştirdi.
Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
8 Yaptırdığı on masanın beşini de tapınağın sağına, beşini soluna yerleştirdi. Ayrıca yüz altın çanak yaptırdı.
Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 Kâhinlerin avlusunu, büyük avluyla kapılarını yaptırdı. Kapıları tunçla kaplattı.
Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
10 Havuzu ise tapınağın güneydoğu köşesine yerleştirdi.
Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
11 Hiram kovalar, kürekler, çanaklar yaptı. Böylece Kral Süleyman için üstlenmiş olduğu Tanrı'nın Tapınağı'yla ilgili işleri tamamlamış oldu:
Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
12 İki sütun ve iki yuvarlak sütun başlığı, bu başlıkları süsleyen iki örgülü ağ,
zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
13 Sütunların yuvarlak başlıklarını süsleyen iki örgülü ağın üzerini ikişer sıra halinde süsleyen dört yüz nar motifi,
yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
14 On kazan ve ayaklıkları,
vishikio pamoja na masinia yake;
15 Havuz ve havuzu taşıyan on iki boğa heykeli,
hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
16 Kovalar, kürekler, büyük çatallar. Huram-Avi'nin Kral Süleyman için RAB'bin Tapınağı'na yaptığı bütün eşyalar parlak tunçtandı.
pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
17 Kral bunları Şeria Ovası'nda, Sukkot ile Seredata arasındaki killi topraklarda döktürmüştü.
Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
18 Süleyman'ın yaptırdığı eşyalar o kadar çoktu ki, kullanılan tuncun hesabı tutulmadı.
Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
19 Süleyman'ın Tanrı'nın Tapınağı için yaptırdığı altın eşyalar şunlardı: Altın sunak ve ekmeklerin Tanrı'nın huzuruna konduğu masalar,
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
20 İç odanın önüne yerleştirilen ve kurala uygun olarak yakılan saf altından kandilliklerle kandilleri,
vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
21 Çiçek süslemeleri, kandiller, maşalar. –Bunlar saf altındandı.–
maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
22 Saf altın fitil maşaları, çanaklar, tabaklar, buhurdanlar ve tapınağın altın kapıları. En Kutsal Yer'in ve ana bölümün kapıları da altındandı.
mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

< 2 Tarihler 4 >